MSIMAMO WANGU
1. Changu ni changu, cha mume/mpenzi wangu tunashea.
2. Mwanaume bahili akae mbali na mimi.
3. Sina huruma na pesa ya mwanaume, labda atakaekuwa mume wangu wa ndoa.
4. Ntafanya majukumu yote kama mpenzi/mke wake, lakini when it comes to my money asahau, imeandikwa "mwanamke atazaa kwa uchungu na mwanaume atakula kwa jasho" so let him provide.
5. Ni marufuku mambo ya joint a/c eti mmoja wetu anaweza kutoa pesa pasipo saini ya mwingine sitaki.
6. Pesa zangu ni zangu ata password simpi, bora nimpe Mama yangu ata nikifa ajifutie nazo machozi.
7. Hata kama nina pesa kuliko yeye, mwanaume ni lazima awajibike, sio pesa yake awanufaishe wengine, maana kuna wanaume ndani wabahili ila nje wanahonga balaa.
8. Nyumba tutasaidiana kujenga, na itakuwa na jina langu au kama tutakuwa na watoto nao tutawaweka humo. Kaka tayari unayo/unazo basi uhakikishe zinakuwa na majina ya watoto pindi tutakapowapata.
9. Ni marufuku ndugu wa mume kujihusisha na mali zetu, narudia tena ni marufuku ndugu wa mume kujisogeza karibu na mali zangu mm na mume wangu! Hizi haziwahusu kabisa tena mkae mbali.
10. Nikitangulia mbele za haki kabla yako ole wako uoe mwanamke mwingine, nitakutokea ndotoni hadi ujute.
NIMEMALIZA