Msikiti uliopewa Jina la Yesu

Kurunzi

JF-Expert Member
Jul 31, 2009
9,283
9,913
Ilianzia katika mvutano wa kisheria kati ya jumuia ya Kiislamu na Kanisa la Waadventista wa Sabato (SDA) kuhusu umiliki wa ardhi.

Mvutano huo uliokuwepo kwa miongo kadhaa, ulimalizika mwezi Oktoba mwaka huu na Mahakama ya Mazingira mjini Kisumu iliamua kuwa ardhi hiyo ni milki ya Jamii ya Kiislamu.

Katika jitihada za kujenga daraja la mahusiano kati ya jamii ya Kiislamu na kanisa, imechagua jina la msikiti ambalo limevuta hisia za wengi katika mitandao ya kijamii.

Msikiti ambao umejengwa kwenye ardhi iliyokuwa kwenye mgogo eneo la Kaloleni katika Kaunti ya Kisumu unaitwa 'Msikiti wa Yesu Kristo mwana wa Maria ( The Mosque of Jesus Christ the son of Mary)

Lakini kwa nini jina hili la kipekee?

Abdul Rashid ni Mwadhini ameliambia gazeti la The Standard la Kenya kuwa '' Tumekuwa na mvutano wa muda mrefu kuhusu ardhi na hii ni moja ya sababu zilizotufanya kuchagua jina hili. Sisi hatuna uadui na Wakristo,'' alisema.

Amesema kuwa Waislamu pia wanaamini Yesu na kuwa alikuwa sambamba na manabii wanne akiwemo Mtume Muhamad (S.A.W).

''Waislamu wanaamini katika Yesu Kristo . Uchaguzi wa jina pia ni shukrani ya Yesu Kristo ambaye tunaamini atarudi tena," Rashid aliliambia gazeti la The Standard.

Hatua hii imegusa hisia za watu nchini Kenya wengine wakihoji je, huu ni Msikiti na Kanisa kwa wakati mmoja? Wengine wameifurahia hatua hiyo

BBC.
Screenshot_20201227-105659.jpg


Sent from my Infinix X650B using JamiiForums mobile app
 
Mdogo mdogo ipo siku waislam watatubu wote na kuachana na mambo ya bokoharam, Is na alshabab.
 
Sifa za jengo kuitwa Kanisa ni zipi?
Na msikiti ni zipi?
Na synagogue ni zipi?
Sio kila waliposali watu wa wakati wao miaka hiyo huitwa kwa jina la jengo la dini yako. Wayahudi walimwabudu Mungu bila jina la Dini! Walikuwa wanamwamudu Mungu wa Jacob tu, Mungu wa mababu zao! Dini zimejipambanua kwa kukwiba kwiba tamaduni za wayahudi, na mainly kwa maslahi ya kucontrol human behavior.
 
Sasa kati ya wakisto na waislam wapi wanamfata yesu?
Wakristo ndio wanaomfuata Yesu, Ndio maana wakaitwa wa-kristu.Sinagogi sio Msikiti! Na wala hayakutumika kusujudu Bali kusali na wala hayakua na alama za mwezi wala nyota juu! Mwishowe mtasema na hekalu pia ni misikiti!
20201227_133233.jpg
 
Wakristo ndio wanaomfuata Yesu, Ndio maana wakaitwa wa-kristu.Sinagogi sio Msikiti! Na wala hayakutumika kusujudu Bali kusali na wala hayakua na alama za mwezi wala nyota juu! Mwishowe mtasema na hekalu pia ni misikiti!View attachment 1660296
Hii ni baada ya editing..lakini sinagogi ni msikiti wa wayahudi..

Maana kila kukicha watu wana edit pale penye mashaka..

Kama yesu alikuwa anasali kwa kupiga magoti na kusujudu,,

Je, ni akina nani wanasujudu?

Jibu hoja.

Kama yesu alikuwa akivua viatu akiingia ktk sinagogi,,

Je, akina nani wanavua viatu wakiingia kusali?

Kama yesu alikuwa haonyeshi alama ya msalaba,,

Nani basi aliyeta msalaba?

Kama yesu alikuwa haswali kwenye madawati na viti,
Je ni nani basi aloyeleta mambo ya kusali kwa kukaa kwenye madawati?

Kama yesu alisema toeni kelele za vinanda vyenu..

Akina nani basi walileta nyimbo kwenye sinagogi?
 
Hii ni baada ya editing..lakini sinagogi ni msikiti wa wayahudi..

Maana kila kukicha watu wana edit pale penye mashaka..

Kama yesu alikuwa anasali kwa kupiga magoti na kusujudu,,

Je ni akina nani wanasujudu?

Jibu hoja.

Kama yesu alikuwa akivua viatu akiingia ktk sinagogi,,

Je akina nani wanavua viatu wakiingia kusali?

Kama yesu alikuwa haonyeshi alama ya msalaba,,

Nani basi aliyeta msalaba?

Kama yesu alikuwa haswali kwenye madawati na viti,
Je ni nani basi aloyeleta mambo ya kusali kwa kukaa kwenye madawati?

Kama yesu alisema toeni kelele za vinanda vyenu..

Akina nani basi walileta nyimbo kwenye sinagogi?
Mvaa pekosi kwenye ubora wko
 
Ilianzia katika mvutano wa kisheria kati ya jumuia ya Kiislamu na Kanisa la Waadventista wa Sabato (SDA) kuhusu umiliki wa ardhi.

Mvutano huo uliokuwepo kwa miongo kadhaa, ulimalizika mwezi Oktoba mwaka huu na Mahakama ya Mazingira mjini Kisumu iliamua kuwa ardhi hiyo ni milki ya Jamii ya Kiislamu.

Katika jitihada za kujenga daraja la mahusiano kati ya jamii ya Kiislamu na kanisa, imechagua jina la msikiti ambalo limevuta hisia za wengi katika mitandao ya kijamii.

Msikiti ambao umejengwa kwenye ardhi iliyokuwa kwenye mgogo eneo la Kaloleni katika Kaunti ya Kisumu unaitwa 'Msikiti wa Yesu Kristo mwana wa Maria ( The Mosque of Jesus Christ the son of Mary)

Lakini kwa nini jina hili la kipekee?

Abdul Rashid ni Mwadhini ameliambia gazeti la The Standard la Kenya kuwa '' Tumekuwa na mvutano wa muda mrefu kuhusu ardhi na hii ni moja ya sababu zilizotufanya kuchagua jina hili. Sisi hatuna uadui na Wakristo,'' alisema.

Amesema kuwa Waislamu pia wanaamini Yesu na kuwa alikuwa sambamba na manabii wanne akiwemo Mtume Muhamad (S.A.W).

''Waislamu wanaamini katika Yesu Kristo . Uchaguzi wa jina pia ni shukrani ya Yesu Kristo ambaye tunaamini atarudi tena," Rashid aliliambia gazeti la The Standard.

Hatua hii imegusa hisia za watu nchini Kenya wengine wakihoji je, huu ni Msikiti na Kanisa kwa wakati mmoja? Wengine wameifurahia hatua hiyo

BBC.View attachment 1660159

Sent from my Infinix X650B using JamiiForums mobile app


مسجد عيسى بن مريم =Masjid Issa Bin Maryam

The Mosque of jesus Christ Son of Merry

Msifikiri hilo jina la Jesus ndio yule yesu aliesulubiwa, mkae mjue hilo. Aliekusudiwa hapo ni Issa/Yesu OG. Na si yesu fake.
 
Back
Top Bottom