Msiba wa Prof Samuel Steven Mushi

Hakuna kipya ila tu siku yake imefika

Angekuwa baba yako unge comment hivyo? This is sad news na sisi tuliokwisha fiwa na wazazi ukubwani tunajua ni jinsi gani hii ina majonzi kwa wanafamilia. Sometime you better not comment at all kwani hujalazimishwa.

Nawapa pole sana wote mlioguswa na msiba huu.
Bwana alitoa na Bwana ametwaa jina lake na lihimidiwe.
 
R.I.P Prof. Mushi

Mungu ailaze 'roho' yako mahala pema peponi..Amina
Naomba nisionekane kama nadhihaki jamani ila mara nyingi sisi binadamu huwa tunamlazimisha MUNGU awalaze watu peponi badala ya kumuachia afanye YEYE anavyoona inafaa kwake! MUNGU ailaze roho ya marehemu mahala pale panapostahili!!!
 
Raha ya Milele umpe ee bwana, Na Mwanga wa Milele umwangazie, Apumzike kwa amani. Amina.
 
R.I.P my beloved Prof. Mushi, you will fondly be remembered by all your students, me being one of them. I remember back in 1990s when you taught us Introduction to Political Science PS 100 and how jovial you were backthen during lectures and how good it was to have had the privilege of being taught by the first black African Professor of the Faculty of Arts at the UDSM. regards to other momentous prominent professors Chachage and Andrew Kiondo who went there ahead of you to prepare for your arrival. R.I.P.
 
Yes kifo kipo tangu enzi,ila kila kitokeapo watu wa klabu huguswa kila mtu kwa namna yake kutegemea ukaribu na umuhimu wa marehemu kwa ndugu,jamaa na jamii kwa ujumla.kifo cha Prof.Mushi kimewatachi wengi hasa wanafamilia,jamaa na wanafunzi wake wote.
 
R.I.P my beloved Prof. Mushi, you will fondly be remembered by all your students, me being one of them. I remember back in 1990s when you taught us Introduction to Political Science PS 100 and how jovial you were backthen during lectures and how good it was to have had the privilege of being taught by the first black African Professor of the Faculty of Arts at the UDSM. regards to other momentous prominent professors Chachage and Andrew Kiondo who went there ahead of you to prepare for your arrival. R.I.P.

Yaah PS 100, umenikumbusha mbali.....nimesikitika sana kwa kifo cha mwalimu wangu wa first yr option yr PS100....nili deserve B flat na ulinipa B flat...wengi walikuona kigwasu kwa kunyima maksi tukikulinganisha enzi hizo na Dr Lyimo AS 100, au yule mzungu wa sociology nimesahau jina....ulikuwa mpole darasani...ukiingia kwenye kipindi...presha yangu ilikuwa inabaki kama kawaida...hukufanana na chachage ambaye akiingia darasani unajiona mtuhumiwa japo hujui kosa lako....nitakukumbuka daima lakini zaidi sana mawazo yako yaliyotolewa kwa upole na unyenyekevu mkubwa...huku ukiwa umeshusha miwani
kwaheri mwalimu wangu
kwa heri baba

kama nitakwenda ulipo tutaonana tena mwalimu

mix with yours
 
Msiba huu umenigusa sana mimi binafsi, nimewahi kufanya kazi na Prof. Mushi. Mimi ni miongoni mwa walimu waanzilishi wa Dar es salaam Prime High School, shule mali ya marehemu. Prof katika uhai wake alikuwa mpenda kujisomea, na mtulivu. Alikuwa hamuonei haya mtu yeyote hata kidogo. Mara ya mwisho nilimuona akitoa mawazo yake kuhusu kujiuzuru kwa Rostam, aliwaambia CCM wasiishie kujivua gamba chamani tu, waisafishe serikali yao pia. CCM,nawasihi wauchue huo kama wasia wa mzee huyu. Masikini sitamuona wala kumsikia tena Prof.Samuel Mushi!
 
Poleni sana,

Msiba huu umenigusa sana,maana huyu Prof.S.S.Mushi alikuwa mwalimu wangu nilipokuwa ninasoma pale UDSM kwenye miaka ya 1999,na pia ninamshukuru Mungu leo tarehe 27.07.2011,Mungu alinipa neema ya kuhudhuria na kutoa heshima zetu kwa mwanazuoni huyu mahiri,wageni mashuhuri waliokuwepo ni Makamu wa Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Rais Mstaafu Mkapa na waziri Mkuu mstaafu Fedrick Sumaye,pamoja na wahadhiri waandamizi mbalimbali,kweli ilikuwa ni huzuni kubwa,na nilipata nafasi ya kutoa mkono wangu wa pole,kwa mjane wa Prof.Samuel S.Mushi na watoto wake.Mazishi yatafanyika Bunju mahali iliko shule yake inayoitwa Dar es salaam Prime Secondary school,
Bwana alitoa na bwana ametwaa jina la Bwana lihidimiwe.R.I.P Prof. S.S .MUSHI .Amen
 
Back
Top Bottom