JUAN MANUEL
JF-Expert Member
- Nov 26, 2010
- 8,324
- 17,911
Hii obsession na watu wenye kufanana na Watusi,haki ya nani!itawatoa roho.ukiiangalia sana hii picha ya cargo air port huyu mke wa mengi amezungukwa na wanyarwanda kila aliyekuwa karibu nae kuna mdada mkaka na wengine sijui walinzi wote pua ndefu
Siku ukifika Kondoa,ukawaona warangi,utasema sio RAIA.
Nenda mafinga,ukaone wachina walivyojichimbia msituni,wana kiwanda cha ambao,wanavuna tu,harafu angalia ndugu zako wabongo wanavyotumikishwa.
Au nenda hapo urafiki,ubungo,ukaone hari za maisha ya wabongo.hata wakati wa kula wanatengwa,wawekezaji wanakula nje ya kiwanda,mbongo analazimishwa alie ndani ya bwaro chafu kama zizi
La nguruwe.
Unafikiri mwekezaji pale urafiki ni mnyarwanda?la hasha,yupo China man! Pale.
Mwenyeji wa Tunduma unafikiri atakuwa anafanana na RAIA wa nchi gani?lazima itakuwa anafanana,na anautamaduni kama watu wa Zambia.pale Tunduma,wenyeji wanasomesha watoto wao upande wa Zambia,hata lugha ya kiwemba,inazungumzwa sana.
Twende kigoma,unataka waha wafanane na nani?wafanane na wewe mzaramo,msukuma,au msandawe?wakati wapo karibu na jamii za Kirundi na kitusi!acha ufala,kwa taarifa yako tu,lugha ya waha,inafanana kabisa na kinyarwanda,ni kama kisukuma na kinyamwezi.
Sasa MTU anaasili ya Kigoma,Kagera,biharsmulo,ngara,unataka awe mfupi na pua bapa,kama wazaramo na Wakwere wa bagamoyo?
Wamasai wapo Kenya na TZ,tumeishawahi kuwa na waziri mkuu mmasai,mbona wao hamuwasemi,hatujawai kuwa na kiongozi mnyarwanda.Ass hole