Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 269,634
- 697,845
Unapogeuka kuwa adui wa hadhira ni kheri ufe kuliko kuendelea kuwa hai...hakuna gundu baya kama kuchukiwa na hadhira.. Fikiria kila roho ikupe laana yake.. Huo ni msiba mara saba kama roho tisa za paka
Unajua tuna watu wengi sana wamesoma lakini hawajaelimika
Haijalishi umesoma mabuku mangapi
Haijalishi umemaliza vyuo vingapi
Haijalishi umefaulu mitihani mingapi
Haijalishi umetunukiwa shahada ngapi
Swali muhimu... Je umeelimika?
Tuna watu wengi tu wenye uelewa kimo cha mbilikimo pamoja na kutumikia muda mwingi kwenye elimu, wamefaulu darasani wamefeli mitaani...
Chuo halisi cha kufaulu ni chuo cha maisha halisi
Musiba ana misiba mingi sijui ataanza na upi na kumaliza na upi
Ana msiba wa maadui aliojitengenezea
Ana msiba wa wale wote aliowatukana na kuwakejeli
Ana msiba wa wale wote aliowazushia tuhuma mbalimbali
Ana msiba wa kesi zilizoko mahakamani
Ana msiba wa wale wote ambao kupitia matamshi na matendo yake waliumia na kuumizwa kwa namna moja ama nyingine
Ana msiba wa hatima yake
Juu ya yote ana msiba wa mbeleko, mfadhili na mlinzi wake...!!!
Madhila yake yatakuwa ni bandika bandua..
Kila jambo lina nyakati zake
Kuna wakati wa kulia na kuna wakati wa kucheka
Ukilia leo kesho utacheka na kinyume chake!!!
Unajua tuna watu wengi sana wamesoma lakini hawajaelimika
Haijalishi umesoma mabuku mangapi
Haijalishi umemaliza vyuo vingapi
Haijalishi umefaulu mitihani mingapi
Haijalishi umetunukiwa shahada ngapi
Swali muhimu... Je umeelimika?
Tuna watu wengi tu wenye uelewa kimo cha mbilikimo pamoja na kutumikia muda mwingi kwenye elimu, wamefaulu darasani wamefeli mitaani...
Chuo halisi cha kufaulu ni chuo cha maisha halisi
Musiba ana misiba mingi sijui ataanza na upi na kumaliza na upi
Ana msiba wa maadui aliojitengenezea
Ana msiba wa wale wote aliowatukana na kuwakejeli
Ana msiba wa wale wote aliowazushia tuhuma mbalimbali
Ana msiba wa kesi zilizoko mahakamani
Ana msiba wa wale wote ambao kupitia matamshi na matendo yake waliumia na kuumizwa kwa namna moja ama nyingine
Ana msiba wa hatima yake
Juu ya yote ana msiba wa mbeleko, mfadhili na mlinzi wake...!!!
Madhila yake yatakuwa ni bandika bandua..
Kila jambo lina nyakati zake
Kuna wakati wa kulia na kuna wakati wa kucheka
Ukilia leo kesho utacheka na kinyume chake!!!