Msiba wa King Majuto: Aibu yako Kikwete, aibu yetu Watanzania...

Ki
Taifa lipo msibani!

Ni msiba wa kitaifa kuondokewa na mfalme wa sanaa nchini, King Majuto. Hakuna haja ya maelezo mengi maana historia yake inajitetea!

Nimetazama nyakati za mwisho wakati anapambania uhai wake Tanzania na India. Pongezi kwa waliofanya jitihada za kumuwezesha kumudu gharama za matibabu ikiwemo Serikali na wadau wengine.

Kifo cha mzee wetu kimetuacha na aibu. Aibu zaidi kwa Rais Mstaafu wa JMT, Jakaya M. Kikwete.

Ni mara nyingi kabla ya maradhi yake Mzee Majuto amekuwa akiomba kwa unyenyekevu apatiwe msaada wa Trekta ili aweze kufanya kilimo cha nguvu.. Aliamini kilimo kitamfaa katika nyakati zake za mwisho kwa maana sanaa haikumfaa vya kutosha.

Si mara moja au mbili alituma direct ombi lake kwa Rais aliye madarakani wakati huo JK aangalie uwezekano wa kumsaidia lakini mpaka anafikwa na mauti hilo halikuwezekana.

Kama Rais wa nchi na wasaidizi wake wameshindwa kusaidia hilo, wanajisikiaje leo wanapoenda kumuaga?

Nakumbuka alisema amesikia na atalifanyia kazi. Nilitarajia BASATA wangeangalia namna ya kutumia sanaa yake kumfanikishia lengo lake.

Hayo yangetokea, pengine mzee angeweza kumudu gharama za matibabu na kupunguza risk ya kufariki mapema. Pengine angekuwa na furaha akastaafu zake sanaa akala mema.. Pengine mambo yangekuwa tofauti.. Pengine, pengine..

Watanzania tuone aibu kwa hili na liwe funzo kwa yajayo.

Rest in Peace King Majuto.
Kifo hakina huruma ikifika saa ya mja haizuiliki kuna huyu bwana Steve Jobs hakuhitaji msaada wa rais kupata matibabu na alifariki kwa ugonjwa.
 
Yule mzee amefanya kazi ya maigizo kwa muda wote.

Kaingia mikataba.

Kafanya matangazo.

Kalamba deals na Al Riyami.

Kaonyeshwa Channel 10.

VHS na DVDs zimeuzwa.

Steps walikua naye.

Ana muvi alizoitwa kama mshiriki.

Unamlaumu Kikwete kwa kutotoa trekta?
Unatulaumu waTanzania?

Kuna waTz wangapi hawana jukwaa la kumlalamikia raisi?
Unaona Majuto anastahili kuliko watu wote?
Umeziangalia fursa alizowahi kua nazo?
Mimi Ndio Nashanga "Ameondoka" Uchumi Wake Upo Chin Sanaaa Wkat Kaanza Sanaa Miaka Ming Nyumaa...Au Ndio Namna Kila Mtu Anavyozichanga Karata Zake?
 
Jk nae ni binadamu kama wewe anasahau afu kuna siku alimwambia majuto anaenda kumuombea msaada kwa magu
 
Hakuna lolote.. tumuache mzee wa watu apumzike.

Kwani wasanii si mnapata pesa nyingi tu..? Jijengeeni utaratibu wa kujisevia na kuwekeza..sidhani kama kuna mtu mwenye jukumu la kukununulia au kukupa tu kisicho chako...tuache lawama za kimaskini..
Tena kwenye shughuli zao anamuona mtu anakwenda kutunza mamilioni halafu baadae mtu huyo huyo anaomba pesa za matibabu
 
Ina maana Majuto hakuwa akipata pesa kutokana na kazi zake?
Kapata nyingi sana na kampuni alizofanya nazo kazi zimeorodheshwa hapo juu!

Neel Salt
DSTV (Maisha Magic)
Al Riyami
Super Banco
Airtel
LAPF (staafu kwa ufahari)
ASAS dairies (pipi za Ivori na ivori cocoa powder)
Azam (Maziwa)


...to mention a few.

King Majuto hakuwa mtu wa kuomba msaada wa matibabu iwapo mikataba yote hiyo ingemlipa vizuri. Aliliongelea sana hilo Mhe. Mwakyembe
 
We naye fyatu tu, msanii badala ya kuomba sheria bora za usimamizi wa kazi zao aombe tractor kweli?? Hivi wasanii wote wakiomba matractor nani atatuburudisha?, sema hapa serikali inapaswa kuona aibu mana kwa msanii mkubwa kama yule kufa masikini ni udhaifu wa serikali kutokua na sheria zinazowanufaisha wasanii, mfano jana taifa zaidi ya asilimia 60 watu walivaa bidhaa zenye nembo ya Simba feki, Club haikunufaika na chochote zaidi ya viingilio, ila wote tungekuwa tumenunua bidhaa halisi za Simba team yetu ingefika mbali kiuchumi.

Bado tuna sera mbovu sana, tena mtu anauuza bidhaa (jezi,skafu, culture n,k) feki mbele ya askari na hakamatwi.
 
Taifa lipo msibani!

Ni msiba wa kitaifa kuondokewa na mfalme wa sanaa nchini, King Majuto. Hakuna haja ya maelezo mengi maana historia yake inajitetea!

Nimetazama nyakati za mwisho wakati anapambania uhai wake Tanzania na India. Pongezi kwa waliofanya jitihada za kumuwezesha kumudu gharama za matibabu ikiwemo Serikali na wadau wengine.

Kifo cha mzee wetu kimetuacha na aibu. Aibu zaidi kwa Rais Mstaafu wa JMT, Jakaya M. Kikwete.

Ni mara nyingi kabla ya maradhi yake Mzee Majuto amekuwa akiomba kwa unyenyekevu apatiwe msaada wa Trekta ili aweze kufanya kilimo cha nguvu.. Aliamini kilimo kitamfaa katika nyakati zake za mwisho kwa maana sanaa haikumfaa vya kutosha.

Si mara moja au mbili alituma direct ombi lake kwa Rais aliye madarakani wakati huo JK aangalie uwezekano wa kumsaidia lakini mpaka anafikwa na mauti hilo halikuwezekana.

Kama Rais wa nchi na wasaidizi wake wameshindwa kusaidia hilo, wanajisikiaje leo wanapoenda kumuaga?

Nakumbuka alisema amesikia na atalifanyia kazi. Nilitarajia BASATA wangeangalia namna ya kutumia sanaa yake kumfanikishia lengo lake.

Hayo yangetokea, pengine mzee angeweza kumudu gharama za matibabu na kupunguza risk ya kufariki mapema. Pengine angekuwa na furaha akastaafu zake sanaa akala mema.. Pengine mambo yangekuwa tofauti.. Pengine, pengine..

Watanzania tuone aibu kwa hili na liwe funzo kwa yajayo.

Rest in Peace King Majuto.
Ccm haina msaada wowote kwa wasanii zaidi ya kuwatumia kipindi cha kampeni
 
Yule mzee amefanya kazi ya maigizo kwa muda wote.

Kaingia mikataba.

Kafanya matangazo.

Kalamba deals na Al Riyami.

Kaonyeshwa Channel 10.

VHS na DVDs zimeuzwa.

Steps walikua naye.

Ana muvi alizoitwa kama mshiriki.

Unamlaumu Kikwete kwa kutotoa trekta?
Unatulaumu waTanzania?

Kuna waTz wangapi hawana jukwaa la kumlalamikia raisi?
Unaona Majuto anastahili kuliko watu wote?
Umeziangalia fursa alizowahi kua ?
Huyu bibie analalamika kila kitu!
Mwache!
43F75D3A-2BEA-4375-A862-43C7557D3FA8.jpeg
 
Watanzania mna hasira! Hahaha..

Okay nawatoa kwenye lawama, nabakisha ya JK na BASATA..

Kama mngenisoma vizuri, mngeelewa mantiki yangu.

Kikwete hata asingempa trekta, kwa nafasi yake bado alikuwa anao uwezo wa kuagiza mamlaka za chini yake ziangalie namna ya kumnufaisha au kuwanufaisha wasanii na kazi zao..

Hii mikataba mnaitaja taja tu lakini wasanii wanapigwa kinoma na hawana ubavu wa kujitetea. Mamlaka zina nguvu ya kuhakikisha hawaonewi!

Hili ni dongo kwa mamlaka. Msome katika urari huo!
 
Taifa lipo msibani!

Ni msiba wa kitaifa kuondokewa na mfalme wa sanaa nchini, King Majuto. Hakuna haja ya maelezo mengi maana historia yake inajitetea!

Nimetazama nyakati za mwisho wakati anapambania uhai wake Tanzania na India. Pongezi kwa waliofanya jitihada za kumuwezesha kumudu gharama za matibabu ikiwemo Serikali na wadau wengine.

Kifo cha mzee wetu kimetuacha na aibu. Aibu zaidi kwa Rais Mstaafu wa JMT, Jakaya M. Kikwete.

Ni mara nyingi kabla ya maradhi yake Mzee Majuto amekuwa akiomba kwa unyenyekevu apatiwe msaada wa Trekta ili aweze kufanya kilimo cha nguvu.. Aliamini kilimo kitamfaa katika nyakati zake za mwisho kwa maana sanaa haikumfaa vya kutosha.

Si mara moja au mbili alituma direct ombi lake kwa Rais aliye madarakani wakati huo JK aangalie uwezekano wa kumsaidia lakini mpaka anafikwa na mauti hilo halikuwezekana.

Kama Rais wa nchi na wasaidizi wake wameshindwa kusaidia hilo, wanajisikiaje leo wanapoenda kumuaga?

Nakumbuka alisema amesikia na atalifanyia kazi. Nilitarajia BASATA wangeangalia namna ya kutumia sanaa yake kumfanikishia lengo lake.

Hayo yangetokea, pengine mzee angeweza kumudu gharama za matibabu na kupunguza risk ya kufariki mapema. Pengine angekuwa na furaha akastaafu zake sanaa akala mema.. Pengine mambo yangekuwa tofauti.. Pengine, pengine..

Watanzania tuone aibu kwa hili na liwe funzo kwa yajayo.

Rest in Peace King Majuto.
Kwetu huwa tunafanya sherehe mzee wa makamo yale kufariki. Maana umri uliobakia ulikua ni umri wa kushambuliwa na magonjwa, hivyo kumfanya ateseke maishani mwake
 
Back
Top Bottom