Mshtuko baada ya mlinzi wa Ruto kuanguka kutoka kwenye gari lililokuwa kasi

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Feb 24, 2012
5,019
9,891
Jumatatu, Mei 16, DP alikuwa katika kaunti ya Kajiado ambapo yeye, pamoja na mgombea mwenza wake aliyeteuliwa hivi karibuni Rigathi Gachagua na viongozi wengine walikuwa wakijipigia debe.

Hata hivyo, walipokuwa wakiondoka Rongai, wenyeji waliachwa kwa mshangao baada ya mmoja wa wasaidizi wa Ruto kuanguka kutoka kwa gari lililokuwa likienda kasi ambalo halikujishughulisha na kusimama ili kuangalia ikiwa aliumia.

Mlinzi huyo aliyekuwa akining'inia kando ya mlango wa gari hilo la kifahari alianguka chini na magari machache ya msafara wa Ruto yakampita alipokuwa akihangaika kujiinua.

Ilichukua msaada wa mwendesha pikipiki ambaye alisimama na kufanikiwa kusimamisha gari na kupata mlinzi wa gari.

Kwa bahati nzuri hakupata majeraha mabaya na aliweza kutembea hadi kwenye gari.

Naibu rais alipitia kaunti ya Kajiado siku ya Jumatatu na kuzuru miji ya Ongata Rongai, Kware, na Kiserian ambako alitangaza azma yake ya urais.

"Kipaumbele chetu kama Kenya Kwanza ni kurekebisha uchumi, kusaidia wafanyabiashara wadogo, kubuni nafasi za kazi na kupanua fursa za kiuchumi kwa kila Mkenya.

Tulishiriki ujumbe wetu wa mpango wa kiuchumi wa kuanzia chini kwenda juu na watu na wafanyabiashara wa Mji wa Ongata Rongai, Kaunti ya Kajiado," alisema.

Haya yanajiri siku chache baada ya Mbunge wa Mathira Ragathi Gachagua kuteuliwa kuwa mgombea mwenza wa Naibu Rais William Ruto katika Uchaguzi Mkuu ujao wa Agosti 9.

Muungano wa Kenya Kwanza ulimchagua Gachagua baada ya mjadala wa saa 17 uliofanyika katika makao rasmi ya Ruto Karen Nairobi asubuhi ya Jumamosi, Mei 14.

Alipokuwa akitangaza kuteuliwa kwake Jumapili, Mei 15 alasiri, Ruto alimtaja mbunge huyo kuwa mzungumzaji mahiri, mwanasiasa aliyefanikiwa kuchaguliwa ambaye ni mpiganaji mwenye kanuni, uthabiti na asiye na woga kwa nia ifaayo.
1.jpg
 
Back
Top Bottom