Mshikaji analalamika mpenzi wake anapenda pesa

Mshikaji analalamika mpenzi wake anapenda pesa

Usitudharau haya yote ni maisha hatukupenda kuishi hivi
sijawadharau, ni tafsiri yako tu. Hakuna anayependa kuishi kwa shida ila tumeumbiwa kuhangaika kwa ajili yetu na viumbe vingine vilivyopo na vijavyo. Hakuna kisingizio.
 
Tatizo watu hawajui kuwa kuna watu kuipata hiyo elfu sita kwa siku ni mbinde.Wewe ukisema elfu sita haitoshi lunch wengine hiyo wanakula Siku nzima na wengine wanaitafuta siku nzima hawaipati.Level za maisha zinatofautiana kama wewe umejaaliwa acha dharau kwa wasionacho
 
elfu sita analalamika???? elfu sita hata lunch haitoshi khaaa si amwambie beibe kua hana hizo hela kuliko kumchoresha!!!

Huwa nyuma ya keyboard na smartphone mtu aweza kuandika anachoweza, ukisema 6,000 hata lunch hautoshi, kuna mwingine hiyo 6,000 ni budget ya siku na mwingine hata hajui ataipataje leo...!!
 
aachane na mapenzi mpaka atakapokuwa tayari kiakili na kiuchumi. Na kama 6,000 ni nyingi ina maana yuko daraja la chini la kijamii na kiuchumi. Atumie muda wake kujikwamua badala ya kutaka kuzuia mafuriko kwa mkono. Hata mpenzi asipoomba hela ya saluni mapenzi ya mjini bado yanahitaji hela. Sasa wanakutana wapi? kwenye viambaza au chini ya miti? Acheni kulialia bana tafuteni hela. Tatizo wengine wanakulia kwenye zile jamii ambazo ukishabalehe na kuweza kununua kitanda tu unakuwa umefaa kuoa. Unakuta nyumba ina baba, mama, wana, wakamwana na wajukuu. Chai wanakunywa saa 6, usiku wanakula kijipane cha samaki na ugali......... ni shida.

Lakini kumbuka kila mtu Ana "haki" ya kupenda na kupendwa. Unataka kusema vile mtu ana kipato kidogo basi aachane na mahusiano?
 
Jamani mshikaji analalamika sana kwamba msichana wake a napenda hela sana, eti hela ya saluni tu anataka shilingi elfu Sita (TSHS 6,000).

Tumsadieje huyu jamaa kwenye haya mahusiano?

Elfu sita,au umekosea ni elfu sitini?
 
Elfu sita,au umekosea ni elfu sitini?

6,000 Tsh. ($ 3 approx.) Takwimu zinaonyesha kuwa bado asilimia fulani ya watanzania wanaishi chini ya $ 1 (2,000 Tsh) kwa siku. Sidhani kama unatakiwa kushangaa hili.
 
6,000 Tsh. ($ 3 approx.) Takwimu zinaonyesha kuwa bado asilimia fulani ya watanzania wanaishi chini ya $ 1 (2,000 Tsh) kwa siku. Sidhani kama unatakiwa kushangaa hili.

Alafu wewe!! Nilijua tu lazima utetee hili, muone vile, hujui nimekumiss?
 
Jamani mshikaji analalamika sana kwamba msichana wake a napenda hela sana, eti hela ya saluni tu anataka shilingi elfu Sita (TSHS 6,000).

Tumsadieje huyu jamaa kwenye haya mahusiano?
Thread Zingne, Ni Kucheka Tuu!!![emoji2] [emoji2] [emoji2] !!!! Ila Mapenzi Yana Kanuni Zake Pia, Labda Ungesema Jamaa Ajui Kanun Zake Tumuelezee.
 
6,000 Tsh. ($ 3 approx.) Takwimu zinaonyesha kuwa bado asilimia fulani ya watanzania wanaishi chini ya $ 1 (2,000 Tsh) kwa siku. Sidhani kama unatakiwa kushangaa hili.

Hakika buku 6 ni nyingi sana
 
Alafu wewe!! Nilijua tu lazima utetee hili, muone vile, hujui nimekumiss?

Teh teh... lazima nitetee coz uchumi wa watu unatofautiana, sioni sababu za kushangaa kitu ambacho kipo katika nchi yetu, kwenye jamii zetu na hata kaya zetu. Leo kwa vile tumebahatika kujikwamua, tusisahau bado kuna wengine hawajajikwamua.

FYI, nimechoka kukumiss coz hutaki tena kunichum kama zamani...hata hunipendi tena...
 
Huyo mshikaji wako ni lofa
na huyo shemeji ako sh 6000 anasuka "twende kilioni" au "mdomo wa kuku"?
Akitaja Ela Ya Kusukia, Jama Atompa!!! Hiyo 6000 Ni Ya Credit, Maana Anamjua Jamaa Ni Mbahili Kaamua Kumzuga. Si Unaona 6000 Tuu Kesi....Ya Kusukia Itakuaje??
 
Lakini kumbuka kila mtu Ana "haki" ya kupenda na kupendwa. Unataka kusema vile mtu ana kipato kidogo basi aachane na mahusiano?
hakuna haki bila wajibu. kupenda ni kitendo. Hisia nani mwenye uwezo wa kuzisoma huko moyoni? ukitenda ndo tunaamini umependa. huna hela basi vumilia ule kwa macho.
 
Teh teh... lazima nitetee coz uchumi wa watu unatofautiana, sioni sababu za kushangaa kitu ambacho kipo katika nchi yetu, kwenye jamii zetu na hata kaya zetu. Leo kwa vile tumebahatika kujikwamua, tusisahau bado kuna wengine hawajajikwamua.

FYI, nimechoka kukumiss coz hutaki tena kunichum kama zamani...hata hunipendi tena...

Sasa wanasubiri nini kujikwamua? Basi waendelee na sabuni tu hadi wajikwamue.

We unazingua bwana, pilipili manga miezi mitatu anakuwa hayupo, so tulikuwa tunatafuta mlinzi nitakayekuwa nabaki nae, jitolee basi.
 
hakuna haki bila wajibu. kupenda ni kitendo. Hisia nani mwenye uwezo wa kuzisoma huko moyoni? ukitenda ndo tunaamini umependa. huna hela basi vumilia ule kwa macho.

Ni kwavile like hutolewa moja tu, ila duuh umemaliza kila kitu.
 
hakuna haki bila wajibu. kupenda ni kitendo. Hisia nani mwenye uwezo wa kuzisoma huko moyoni? ukitenda ndo tunaamini umependa. huna hela basi vumilia ule kwa macho.

I see, lakini mbona watanzania asilimia fulani wana earn less than 6,000Tsh per day. Mbona nao wanaoana na kulalana kama kawa...

I stand to be corrected, but everyone deserves to love and be loved, regardless of their economic status.
 
Sasa wanasubiri nini kujikwamua? Basi waendelee na sabuni tu hadi wajikwamue.

We unazingua bwana, pilipili manga miezi mitatu anakuwa hayupo, so tulikuwa tunatafuta mlinzi nitakayekuwa nabaki nae, jitolee basi.
Sote ni watanzania bi atoto, we come from humble beginnings. Hatuna sababu ya kuwaona walio na kidogo kuwa hawana haki.

Si uliona kuwa Manga ML ni zaidi? Kumbatia mto sasa...
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom