Msekwa amvaa Nape

Msekwa amvaa Nape

Goli la mkono ndiyo mwisho wa tanzania
 
Nape Nnauye ni Katibu mkuu mwenezi Itikadi wa CCM, yeye ndiye msemaji rasmi wa CCM kitaifa.
Alichosema Nape ndio kauli rasmi ya CCM.

Kauli Hii itagharimu uhai wote wa maisha ya kisiasa ya Nape.. Itamgharimu sana..!
 
Lakini alichosema Nape ndio ukweli ambao CCM imekuwa ikifanya kule Zanzibar kwenye urais na huku Tanganyika kwenye majimbo mengi ya uchaguzi. Hata kwenye chaguzi za serikali za mitaa magoli mengi ya mkono yalifungwa na ushahidi uko wazi kwani kuna baadhi ya maeneo walikoshinda wapinzani badala ya kuwaapisha waliwaapisha wale wa CCM. Kuna mtaa hapa DSM wananchi walilazimiaka kumtafuta wakili ili kumwapisha kiongozi aliyeshinda wa CHADEMA baada ya serikali kutotaka kumwapisha wakipanga kumpa wa CCM. Hicho alichosema Nape ndipo ambacho tukitegemee mwaka huu sehemu nyingi majimboni, kwenye urais kule Zanzibar na Muungano. Kosa la Nape ni kuwa ametoa siri ya mchezo mchafu wanaoufanya. Hata huyo Msekwa anasema tu lakini ukweli anaujua kuwa CCM imekuwa inafunga magoli mengi ya mkono. Kule Kagera kuna jimbo ambalo walitangaza matokeo kwa mitutu ya bunduki ili kulazimisha ushindi. Kuna mifano mingi sana ya magoli ya mikono yanayofungwa na CCM katika chaguzi mbali mbali na hii ni kwasababu Refa ni mmoja wa wachezaji wa timu ya CCM. Hata uandikishaji wapiga kura kule Zanzibar ni goli la mkono linapigwa ili kuwaacha wananchi wengi na kuwaandikisha mamluki watakaokipigia kura CCM ha huku Tanganyika maeneo mengi ambako uandikishaji umeshafanyika, maelfu ya wananchi wameachwa kuandikishwa.
 
Nikikitizama kichwa cha Nape huwa naona mataputapu yalivyojaa humo..
 
wazee wenye busara wameliona hilo ni kosa, tukubali Nape aliteleza.
 
lastman

Ivi kati ya msekwa na nape nani ni msemaji wa chama? mm naamini kauli ya msemaji ndiyo imetoka chumbani kabisa. labda nape alaumiwe kwa kusema siri za chama hadharani
Hata mimi nakubaliana na wewe. Nape ni msemaji wa chama na chama hakijakanusha
 
lastman

Ivi kati ya msekwa na nape nani ni msemaji wa chama? mm naamini kauli ya msemaji ndiyo imetoka chumbani kabisa. labda nape alaumiwe kwa kusema siri za chama hadharani
Huo ndo ukweli kaka jamaa amevujisha mipango yao
 
Last edited by a moderator:
Haiwezekeni mchezaji makini aliejindaa kwa mechi afunge bao kwa mkono. Goli kama hilo litafutwa na refa. Naomba wananchi wapuuzie maneno ya upuuzi kama hayo.

Kufunga goli la mkono ni faul na moja kwa moja litakataliwa na refa ambayo ni Tume ya Uchaguzi. Kauli mbaya kama hizo zinaweza kufanya Wananchi kukosa imani na Serikali na kuleta machafuko na ninaamini haya ninayoyasema ndio msimamo wa chama changu.

Pius Msekwa.2.07.2015 (ITV, kipindi cha Mzelendo).


Huyu nape sijui alipataje hii post.


Nape ni kilaza by Nature.alijisahau akatoa siri za ndani hadharani. tatizo lake hajui kwamba enzi za CCM yashika hatamu zimepitwa na wakati. unajua hivi ndio vitu haswa vinavyojadiliwa kwenye vikao vya siri vya CCM ndio maana kila mwenye akili ndani ya ccm aliweweseka kwa maneno haya ya Kilaza Nape Nnauye. hapa ni kama baba amejificha ndani hataki mdai wake ajue kama yupo na anampa maagizo mwanaye kwamba yeyoye akija amwambie hayupo na hammad anakuja mdai na kumuuliza mtoto "baba yako yupo nyumbani?" mtoto anajibu "Ameniambia niseme hayupo"
 
Wote ni walewale,huyu msekwa imemkera kwa sababu kijana kafichua ukweli, kwa kusema siri ya wanene (baraza la mawaziri). tunaona huku mtaani wanavyogawa madila,10,000/= na kuwadanganya wanainchi kuwa upinzani uchaguzi huu watapata madiwani wa kutosha na si wabunge na Rais.Haya wanayasema kwa vile wanauhakika mnyama BVR atawabeba.
 
Nape ni vuvuzela...Hastahili hata kujadiliwa humu
 
Msekwa anafanya damage control. Tunajua ndio mchezo wao siku zote, Nape hakuitoa kauli ile kwa bahati mbaya.
 
Nashangaa mpaka hivi sasa kwanini vyama vya upinzani vimekubali kushiriki uchaguzi mwezi wa kumi bila RAIS kutimiza ahadi yake ya kupeleka muswada wa dharula bungeni wa kuunda TUME HURU YA UCHAGUZI na pia KURUHUSU INDEPENDENT CANDIDATES!! Ni ukweli ulio wazi kuwa CCM haiwezi kuondolewa madarakani kwa KURA BILA KUWA NA tume huru!!! Kukubali uchaguzi mwezi wa kumi bila TUME huru ni kujinyonga kisiasa!!!!
 
Nape kaongea ukweli, hilo halina ubishi... Mikina Msekwa hii inaishi kwa mazoea ya kudanganya!

Mnaweza kushangaa mwisho wa siku Nape akaingia mbinguni, mara nyingi anasema kweli. Ila mwnyekiti wa tume ya uchaguzi ni mzee ambae hata kanisani anaheshimika lakini ni bure kabisa. Mpaka sasa hivi hakutengeneza maisha yake akaachana na siasa? Kama ya dunia hajamaliza ya mbinguni atayawahi kweli?
 
Muacheni Nape aseme ya mwisho mwisho, kwani baada ya octoba hatasikika tena!!
 
Nape ni mcharuko aongee tu ila atatujua sisi ni nani oktoba na goli lake hilo la mkono.
 
Back
Top Bottom