Kuna wakili toka sauzi anakuja kuweka ishu sawa....
Wakili toka sauzi atafanya nini? unajua watz wengine ni ma boflo sana, wanafikiri ukikodi wakili toka sauzi atasaidia kuliko wakili wa hapo dsm. kwa kesi ya homicide kama hii, wakili wa sauzi hatamsaidia kabisa, hao wa sauzi wanafaa kwa kesi za kibiashara labda napo kidogo tu.
kwa mazingira ya juu juu, kesi dhidi yake ingekuwa manslaughter, lakini kuna uwezekano wa murder kwasababu wanasema kanumba alikuwa na mapovu, kama postmortem itafanywa vizuri, pengine ayo mapovu na soda iliyokuwa chini aliwekewa sumu, wengine wanasema hivyo, au labda kalitumwa na watu kammalize. lakini kama issue haitakuwa hivyo, huyu mtoto atakaa hapo miaka hata kumi haifiki, atatumikia miaka michache tu ya manslaughter, kwasababu death came as a result of a fight, na kisheria, kifo chochote kinachotokana na ugomvi huangukia kwenye manslaughter, inategemea atakavyojitetea ugomvi ulikuwaje na yeye alifanya nini, anaweza kupewa hata kutumikia jela miaka mitatu au chini ya saba. kila kesi huamuliwa kwa fact zake. lakini kwa sasa, hadi upelelezi uje utimie, na yeye aje afungiwe/asomewe commital to the High court, inaweza chukua miaka si chini ya miwili, so kwasasa atakaa ndani miaka si chini ya miwili kwa uzoefu ninavyoelewa. baada ya kuwa committed to the High court ndo ataweza pewa adhabu hiyo ya manslaughter. cha muhimu ni kwamba hatanyongwa kabisa kwenye kesi yenye mazingira kama haya, haitakuwa murder, ni manslaughter. period.
Namwonea huruma sana, kwasababu ni mtoto mdogo, hata maisha hajayajua, ana miaka 18, kuja kutoka hapo atakuwa na miaka si chini ya 25. ramani yake ya maisha yote imekufa, na future yake ya usanii ndo imeishia hapo,...sidhani kama hata akija kutoka atakujaendelea na usaniii, kwasababu amekutana na mkosi. itamsumbua sana, hata kuja kuolewa ni ngumu kwasababu watu wanamwona kama ana balaaa....hapo ndo huwa nachukia umaarufu....ukiwa na mema unatambulika na kila mtu, ukiwa na mabaya unatambulika na kila mtu pia. Pole sana mdogo wangu Lulu.