Msanii Joseph Haule (Prof. Jay) ajiunga CHADEMA

Msanii Joseph Haule (Prof. Jay) ajiunga CHADEMA

Prof J aliisha kwisha long time ago, sasa ni historia tu. Ukimuona pale rose garden mpaka bia alikuwa anaomba. Njoo rose garden upate story zake.
Ulichoandika ni sawa na upeo wa akili yako, maana kutumika kama condom na CCM au Clouds FM ndiyo kuwa kwenye kiwango.
 
Msanii maarufu wa bongo flava Joseph Haule aka Proffesor Jay, leo hii amejiunga na chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA na kukabidhiwa kadi yake ya uanachama mjini Dodoma.

View attachment 94612 View attachment 94613

mleta hoja anasema msanii maarufu ahamia chadema,jamani hivi kweli j kwa sasa bado unaweza kusema ni msanii maarufu mi nadhani ingekuwa msanii aliyeishiwa kimziki ahamia ajiunga chadema.kwa sasa j hata jot hamfikii kimziki.
 
nani kakwambia kwamba kinondoni tunataka wanamziki watuongoze usitukosee heshima aenge huko na utoto wake kinondoni tunataka watu makini siyo kichwa kama cha j.

Kinondoni yenyewe huijui, unarupoka tu, unakaa kinondoni unauliza ilipo Mango? mijitu mingine bana...
 
Prof Jay ni jembe,ana busara,mtu makini,mstaarabu,mpambanaji na kioo halisi cha jamii.... njoo Kinondoni Jizze utapita bila kupingwa..........
 
mleta hoja anasema msanii maarufu ahamia chadema,jamani hivi kweli j kwa sasa bado unaweza kusema ni msanii maarufu mi nadhani ingekuwa msanii aliyeishiwa kimziki ahamia ajiunga chadema.kwa sasa j hata jot hamfikii kimziki.
Joto hasira...
 
sasa wana ruvuma tumempata kamanda wetu atekayekuwa anapeperusha bendera ya M4C kwa punchlines za kufa mtu.nchimbi na komba jipangeni sawasawa.
 
hili ni jembe hakika najua wengine watabeza lakini hili jembe limekwenda sehemu panapo stahili
 
kina cha maji hakipimwi kwa miguu yote miwili mwabie ajaribu kama hajaishia kura 10.
yaani kwa sasa ameshapata zaidi ya kura 1000 fasta, masela wa lizaboni, mfaranyaki, mjimwema, msamala na hata mabatini, chezea songea wewe? Nchimbi atafute jimbo lingine na si songea mwaka 2015!
 
Nilikuwa nasubiri kwa hamu sana kujua upande aliosimama huyu mpambanaji wa kweli katika tasnia ya bongofleva, hatimaye leo nimefahamu.....HONGERA SANA Prof J, huu ni uamuzi wa busara sana hasa kwa hadhi na jina lako katika sanaa, hiki ulichokifanya ni wazi kuwa umeamua kuishi na kutenda kadiri ya mistari ya tungo zako.

We ni mpiganaji na mkongwe katika fani ya muziki wa kizazi kipya, kama ambavyo umekuwa ukipaza sauti yako kupigania maslahi yenu, kwa majukwaa ya burudani, ni vema sasa ukatumia majukwaa ya kisiasa kutanua wigo wakuwatetea walalahoi wa taifa hili (na wasanii wenzako), kama ambavyo SUGU anafanya....
Taifa linatutegemea sana vijana, linatuhitaji sana vijana kupambana ili kuleta mabadiliko ya kweli na yenye manufaa kwa wote.

Mheshimiwa Joseph Mbilinyi- SUGU, amewaonesha njia ni vema wasanii wote wa muziki wa kizazi kipya, wanaharakati wanaoufahamu vema muziki huu ulikotoka wakajitokeza wazi na kumuunga mkono kama ambavyo leo Prof J ameafanya.
Kina SOLO THANG, DOLLA SOUL, MR PAUL, LADY JD, SOGGY DOG ANTER, na wengine wakitambo kile jitokezeni na nyie.

KILA LA HERI PROF J!
 
Dah! Kesho utasikia amefunguliwa kesi kwa kosa la kuvaa suruali ya kijeshi.
"Chezea magamba weye"

yaweza ikawa Hata kusakwa ili roho yake iachanishwe na mwili ili kuweka kitisho kwa wasanii wengine wanaojipanga kuja CHADEMA kama vile Afande sele.
 
nani kakwambia kwamba kinondoni tunataka wanamziki watuongoze usitukosee heshima aenge huko na utoto wake kinondoni tunataka watu makini siyo kichwa kama cha j.

tafadhali kakasamu tupe vigezo vya mtu makini
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom