Msamaha na Kisasi

Nyoka akikugonga kisigino na kukuachia sumu ukajitibu ukapona inabidi akija tena umpe kisigino agonge mara ya pili kwa sababu shambulio la kwanza halikufanikiwa

Come on bro 🤦
Mkuu umenichekesha kweli,dah! Pointing hii inalenga kuhalalisha kisasi
 
Hapa tunaamua kuyapokea maumivu tunaugulia weee halafu tunayaacha yapite.Tunaanza kujifariji,kama ulinidhulumu nitajisemea mbona hiki kinatafutwa TU,au hakuna atayezikwa na Mali nk.
Tukifanya hivi maumivu yanaisha ila kumbukumbu itabakia
Mbona haya ni mateso sasa dah
 
My friends, ladies and gentlemen,
ni muhimu sana kusamehe na kusahau, kwasababu mbingu si hasira wataingia watakatifu tu.

Maisha hayana extra time,
chagua upande sasa, ili hatimae uwe na uhuru kamili, ujasiri usiotikisika na uwe na uhakika wa kusimamia unachokiamini kibinafsi na mbele ya jamii. Kua neutral ni unafiki na ubinafsi wa kindezi mno.

ondoka kwenye Giza na sheria kali za agano la kale, na uingie kwenye Nuru katika agano jipya lenye sheria zilizohuishwa. Kung'ang'ana na habari ya visasi dhidi ya ubaya uliotendewa kabla, ni kujitafutia maradhi ya kimwili na kiroho, lakini pia ni maandalizi ya kujiangamiza kwa makusudi kijami, kisiasa na kiuchumi.

ni muhimu sana kuchukuliana kibinadamu na kusonga mbele bila manung'uniko na itapendeza zaidi 🐒
 
Utusamehe... Makosa yetu... Kama nasi tuwasamehevyo walio... Tukosea.......
Amina........
Ambao hawatoi msamaha hawaendi.... Mbinguni
 
Msamaha.... Ila hua sisahau nikimsamehe mtu.... Sijui ni mimi tu¡ ila hata huyo niliemsamehe tunacheka vizuri tu¡
Achana na neno kusahau ambalo haiwezekani
Je unapokua unacheka
Hua na moyo mweupe au unafiki?
 
Daima mimi ni ntu wa kisasa. Ntu akinfanyia ubaya nami humlipa kwa ubaya na kuuzidisha kidogo.

Ukiwa ntu wa wa kumsamehe sana watu wanakuona kama mataqo yao.
 
My friends, ladies and gentlemen,
ni muhimu sana kusamehe na kusahau, kwasababu mbingu si hasira wataingia watakatifu tu.
Kusamehe tunasemehe ila kusahau ni uongo ubongo kazi yake ni kuhifadhi kumbukumbu ziwe nzuri au mbaya

Ili uamini hili
unaweza kuona tukio fulani
Ubongo ukakukumbusha kua hii sio mara ya kwanza kuona

na hapo wewe kama wewe ulikua umesahau ila Ubongo unakukumbusha baada ya kuona mfanano wa tukio
so kusahau sio rahisi na sidhani kama inawezekana
Maisha hayana extra time,
chagua upande sasa, ili hatimae uwe na uhuru kamili, ujasiri usiotikisika na uwe na uhakika wa kusimamia unachokiamini kibinafsi na mbele ya jamii. Kua neutral ni unafiki na ubinafsi wa kindezi mno.
Eeh chagua upande ishii
Hapa umejuja kama shemasi 🐒
 
Kusamehe ni jambo moja kusahau ni jambo lingine...

Naweza kusamehe ila kusahau hapana..
Wala sio tatizo lako nadhani kila mtu yupo hivi
Samehe kwa dhati usibebe kinyongo
Ila kusema usahau labda kicwa uki format
 
Kisasi ni haqq ila fikiria Je? baada kulipa kisasi nitapata nafuu na hasira zangu.kushuka..?au ndo nitazidisha matatizo.? je.? hayo matatizo yanaepukika..?

NITACHANGIA VZR.:
 
Kisasi ni haqq ila fikiria Je? baada kulipa kisasi nitapata nafuu na hasira zangu.kushuka..?au ndo nitazidisha matatizo.? je.? hayo matatizo yanaepukika..?
Mimi sijui kuhusu standard za kisasi
Wewe mkosewa ndiyo upime kama ulipe kwa njia gani bila kujiweka mtatani

Au chagua msamaha
NITACHANGIA VZR.:
Karibu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…