ShesRise_1
JF-Expert Member
- Aug 21, 2025
- 15,152
- 35,333
Kuna msemo unasema, hakikisha unachagua upande
Usiwe vuguvugu
Kama ni moto, kuwa moto
Kama ni baridi, kuwa baridi
Japo watu wengi husema usijulikane kirahisi, ila tambua kuna hasara ya kutokujulikana
So unapokosewa, unapoudhiwa au kuumizwa, hakikisha unajulikana umesimama upande gani
Hii tabia ya kujifanya neutral kila wakati kuna muda sio nzuri
Jifunze kujua ni wapi uwe baridi, ni wapi uwe moto, na mara chache sana ujue ni wapi uwe vuguvugu
Kama mada inavyosema...
Msamaha au Kisasi?
Kama umekosewa na umeumizwa, halafu una uwezo wa kusamehe, samehe
Lakini samehe kwa dhati kabisa, kutoka ndani ya moyo
Kwa sababu ukisamehe, amani ya kwanza ataipata wewe kabla hata hajanufaika huyo uliyemsamehe
Sio unasema umesamehe halafu kila siku unanung'unika, unalalama na kurudia lile tukio
Hapo hujasamehe
Unajidanganya mwenyewe
Na huo unafiki wa kuonekana umesamehe wakati bado umebeba mzigo ndani, unaweza kukugharimu kihisia na hata kuharibu mambo mengine kwenye maisha yako
So kama umeamua kusamehe, samehe kweli
Usiwe vuguvugu
Lakini kama umechagua kisasi, ina maana kwako msamaha hauna tija, haukupi amani na unaamini kulipa kisasi ndio haki
Kuna dini inasema kisasi ni haki ya aliyekosewa
Kuna dini nyingine inasema samehe saba mara sabini
Yule aliyechagua kisasi amechagua kuamini kisasi ni haki yake
Na ukweli ni kwamba ana hoja, kwa sababu ni yeye pekee anayejua ameumizwa kwa kiwango gani
Lakini swali linabaki...
Baada ya kulipa hicho kisasi, una uhakika utapata amani, au ndio utaanza kuishi na majuto?
Mfano ukaona adhabu anayostahili aliyekukosea ni kumuua
Je, baada ya hapo utajisikia vizuri, au ndio utaanza kuishi na trauma ya kumwaga damu?
Unaweza ukaamini una haki ya kulipa kisasi
Lakini hakikisha kisasi chako hakiondoki na furaha yako hakichukui amani yako, wala hakiharibu destiny yako
Swali la mjadala👇
Wewe unaamini katika msamaha au kisasi?
Kwa nini umechagua upande huo?
Au wewe ni vuguvugu?
Na kama ni vuguvugu, unaelewa gharama za kutokuwa na msimamo?
ShesRise_1 🤚
Usiwe vuguvugu
Kama ni moto, kuwa moto
Kama ni baridi, kuwa baridi
Japo watu wengi husema usijulikane kirahisi, ila tambua kuna hasara ya kutokujulikana
So unapokosewa, unapoudhiwa au kuumizwa, hakikisha unajulikana umesimama upande gani
Hii tabia ya kujifanya neutral kila wakati kuna muda sio nzuri
Jifunze kujua ni wapi uwe baridi, ni wapi uwe moto, na mara chache sana ujue ni wapi uwe vuguvugu
Kama mada inavyosema...
Msamaha au Kisasi?
Kama umekosewa na umeumizwa, halafu una uwezo wa kusamehe, samehe
Lakini samehe kwa dhati kabisa, kutoka ndani ya moyo
Kwa sababu ukisamehe, amani ya kwanza ataipata wewe kabla hata hajanufaika huyo uliyemsamehe
Sio unasema umesamehe halafu kila siku unanung'unika, unalalama na kurudia lile tukio
Hapo hujasamehe
Unajidanganya mwenyewe
Na huo unafiki wa kuonekana umesamehe wakati bado umebeba mzigo ndani, unaweza kukugharimu kihisia na hata kuharibu mambo mengine kwenye maisha yako
So kama umeamua kusamehe, samehe kweli
Usiwe vuguvugu
Lakini kama umechagua kisasi, ina maana kwako msamaha hauna tija, haukupi amani na unaamini kulipa kisasi ndio haki
Kuna dini inasema kisasi ni haki ya aliyekosewa
Kuna dini nyingine inasema samehe saba mara sabini
Yule aliyechagua kisasi amechagua kuamini kisasi ni haki yake
Na ukweli ni kwamba ana hoja, kwa sababu ni yeye pekee anayejua ameumizwa kwa kiwango gani
Lakini swali linabaki...
Baada ya kulipa hicho kisasi, una uhakika utapata amani, au ndio utaanza kuishi na majuto?
Mfano ukaona adhabu anayostahili aliyekukosea ni kumuua
Je, baada ya hapo utajisikia vizuri, au ndio utaanza kuishi na trauma ya kumwaga damu?
Unaweza ukaamini una haki ya kulipa kisasi
Lakini hakikisha kisasi chako hakiondoki na furaha yako hakichukui amani yako, wala hakiharibu destiny yako
Swali la mjadala👇
Wewe unaamini katika msamaha au kisasi?
Kwa nini umechagua upande huo?
Au wewe ni vuguvugu?
Na kama ni vuguvugu, unaelewa gharama za kutokuwa na msimamo?
ShesRise_1 🤚