Rais wa baba yako na ukoo wenu
Maneno machafu hayatabadilisha ukweli lowasa hata akivikwa koti gani hawezi kuwa sawa na magufuli. katika nchi hii angalau ccm unaweza kukiita ni chama kinachofuata demokrasia, ni chama cha kila mtu. hata lowasa kiliweza kumvumilia na kukaa naye lakini pia rais kikwete busara zake zitukuzwe. hajawahi kukana urafiki wake na lowasa na ameonesha kwamba mtu anaweza kuwa rafiki yako na ukamkaribisha mkanywa nae chai nyumbani kwako lakini bado si kigezo cha kumpa uongozi. chadema kwa miaka yote kimeonekana kilikuwa kinaongozwa na ng'ombe watupu. haiwezekani chama chenye kuungwa mkono na karibu nusu ya wananchi wote kinakuja kufanya mambo ya kipuuzi kiasi hicho, kumpa mtu ridhaa ya kuwaongoza akiwa mwanachama wenu wa siku 2 tu. pengine kwa kutoka kwake kaskazini ni tiketi ya kuaminiwa haraka na wanakaskazini wenzake.
hatimaye nimekubali hata kama utakuwa na karama ya uongozi kwa kiasi gani ikitokea huna elimu nzuri ya makarasi itafikia tu pahala utajichanganya (mbowe). labda shetani asaidie ili lowasa ashinde, lakini ikitokea kinyume chake tlp au udp ya mapesa itakuwa afadhali. cdm mnashindwa kutumia akili hata kwa vitu vidogo sana. fikirieni mtajitetea vipi na suala hili, hamuoni aibu? je, tuliokuwa na bahati mbaya ya kutotoka kaskazini?
1. mgombea urais - arusha
2. mwenyekiti - kilimanjaro
3. katibu mkuu - manyara/arusha
4. mwenyekiti wanawake taifa - kilimanjaro
5. mwenye chama (mtei) - arusha/moshi
ccm wakisema mnafikiri wanawaonea. jipimeni