Msafara wa Magufuli Arusha

Msafara wa Magufuli Arusha

Alikuja hapa mererani mchana mahali alipokuwa anajinadi waliweka na makatapila akawa anayatumia kama sera yake.
Kilichonishangaza kuna jamaa m1 alikuwa na gari yake ya ndizi aliambiwa akae pembeni eti msafara wa rais unapita akabishana nao wakambeba na gari yake wakaenda kumueka selo mpaka jioni wakampiga na faini ya 50,000 kisa eti kakataa kuwa magufuli ni rais.
Kilichonikera zaidi anatumia serikali kama vile ndio rais tayari.
 
Sio msafara wa Mgombea urais huyo ni wazir wa ujenzi tunapaswa kuelewa hapo jaman, na pia alikua Arusha kikazi
 
Leo jioni mida ya Saa kumi jioni nikiwa hapa Usa River, ulipita msafara mkubwa wa Waziri wa Ujenzi Ndugu Magufuli akiwa na escort nzito kama vile tayari ni Rais akisindikizwa kwa ving'ora na difenda na pikipiki za polisi.

Katika Msafara huo alikuwepo pia Mkuu wa Mkoa wa Arusha pamoja na Manyara na RPC wa Arusha na magari mengine kama 20 ya serikali.

Nauliza, hivi inaruhusiwa kwa mgombea Urais kupewa escort nzito kiasi hiko pamoja na msafara kiasi cha kutokaa foleni au ndio matumizi mabaya ya madaraka.?

Kwasababu CCM ni chama dola,CCM inapaswa kufa sambamba na mifumo yake yote kuu kuu iliyopitwa na wakati.
 
Alikuja hapa mererani mchana mahali alipokuwa anajinadi waliweka na makatapila akawa anayatumia kama sera yake.
Kilichonishangaza kuna jamaa m1 alikuwa na gari yake ya ndizi aliambiwa akae pembeni eti msafara wa rais unapita akabishana nao wakambeba na gari yake wakaenda kumueka selo mpaka jioni wakampiga na faini ya 50,000 kisa eti kakataa kuwa magufuli ni rais.
Kilichonikera zaidi anatumia serikali kama vile ndio rais tayari.

Huu ni uongo ulio kithiri. Tafakari upya....
 
Huu ni upuuzi mgombea urais alafu bado anapewa media time..ulinzi na cheo..only in tanzania huu ni upuuzi
 
Kimsingi, lililovunjwa ni Bunge, fahamu baraza la mawaziri lipo na pia serikali bado ipo madarakani, hivyo mh magufuli bado ni waziri na ana haki zote kama waziri. Lakini pia ufahamu serikali (dola) bado ipo madarakani, na dola ni nani? CCM, na mgombea wa ccm ni nani? Magufuli, mwacheni aanze kuzoea escort kabla hajaingia magogoni bana!
 
Kama ameweza kutumia Ndege ya Serikali kujitambulisha na Speech yake kuwekwa kwenye Tovuti ya Ikulu ....hayo pia yanawezekana.
 
umekurupuka mkuu, Makamu wa Rais alikuwepo; bavicha bana, mnajisikia raha tu kupost madudu
 
Hapa mkuu umepotosha jamii. lakini wananzengo wamekushtukia, maana ulona msafara wa makamu wa rais akitokea mererani kuweka jiwe la msingi kwa ujenzi wa barabara. Jamani tuwe wapembuzi makini kabla ya kukurupuka. Magufuli nae alikuwepo katika msafara huo wa makamu wa rais
 
Kila mgombea mteule wa nafasi ya urais lazima apewe ulinzi
 
hapa Usa River, ulipita msafara mkubwa wa Waziri wa Ujenzi Ndugu Magufuli
Kuwa waziri lazima uwe mbunge. Bunge lilishavunjwa. Magufuli sio mbunge, sio Waziri. Rekebisha hapo kwanza.
 
Back
Top Bottom