Msaada"" wenu"" wakuu?

Msaada"" wenu"" wakuu?

VIkisha komaa hata ufanye nini mtu wangu, its over, unakuwa tu unatuliza symptoms zake.

Ponea yake nikuvitibu mapema (early stages)

UKiwa stage ya kati kati unakuta unapoona vinaamka baada ya miezi au mwaka.

Ili ikiwa konki, aisee utaliwa pesa sanaaaa kutafuta dawa

Stage yako, ni kumantain symptoms, Endelea kutumia dawa za kuituliza lakini pia kula mapema na milo mitatu, kunywa maji sana, lakini pia acha dagaa kabisa, maharage, vidonge vya maumivu ukiwa umeshiba na maji mengi
Sawa mkuu vitu hvyo maharage mekundu nikigusa tu balaa linaanza vtu vya uchachu nyanya n.k ndo usipime
 
Nimeona kuna kiazi mmoja anadai akimbilie kwa Yesu
 
Tiba Ni:-
  • Acha kula vile vyakula ambavyo ni visababishi au vichochezi vya vidonda vya tumbo.​
  • Usipende kukaa na njaa kwa muda mrefu​
  • Kunywa uji wa dona/sembe usio na mchanganyiko wowote​
  • Baada ya siku 7 utakuwa sawa.​
 
Pole sana OTHMAN BEY kwa changamoto unayopitia ya vidonda vya tumbo, najua vinaweza kuwa kero kubwa sana na kukufanya ushindwe kufanya mambo yako vizuri. Ni vizuri kuona wenzako wanakupa ushauri mbalimbali hapa, inaonyesha jinsi gani tunavyojaliana.

Kama walivyosema wengine, mambo ya lishe na namna unavyokula ni muhimu sana. Jaribu kuepuka vyakula vyenye asidi nyingi, viungo vingi, na vile vinavyokubana au kukuletea maumivu (kama Eli Cohen alivyoelezea kuhusu maharage au nyanya). Pia, kuepuka kukaa na njaa kwa muda mrefu na kujaribu kula kwa wakati maalum ni ushauri mzuri sana. Uji wa dona au ule wa mtama usio na sukari nyingi au maziwa unaweza kusaidia kutuliza tumbo.

Pia, jaribu kuepuka msongo wa mawazo kadri uwezavyo, kwani stress huweza kuchochea vidonda vya tumbo. Na kuhusu vinywaji, maji mengi na juisi zisizo na asidi (kama vile tikiti maji au bamia) ni nzuri kuliko soda au vinywaji vyenye kafeini nyingi.

Jambo la muhimu zaidi ni kuhakikisha umemwona daktari ili upate uchunguzi sahihi na ushauri wa kitaalamu. Daktari anaweza kukupa dawa sahihi za kutibu vidonda hivyo na kukushauri vizuri zaidi kulingana na hali yako. Huenda kuna sababu maalum ya vidonda vyako ambayo daktari tu ndiye anaweza kuigundua.

Nakutakia afya njema na upone haraka! Tuko pamoja.
 
Sawa kaka nitaufanyia kaz ushauri wako!
Kama sasa hivi umeshakula ?

Kula saa moja au mbili asubuhi

Sita au saba kamili mchnaa

Saa kumi tafuna visnacks

Usiku isipite saa mbili na nusu.

Hakikisha pia kuwa gap ya kula na kulala inazidi nusu hadi lisaaa.
 
Back
Top Bottom