Habari zenu wana Jamvi :;
Kwanza namshukuru Mwenyezi Mungu kwa baraka na rehema zake kwangu. Kwa ufupi nimepitia ktk kipindi cha majaribu..iko. hivi, :Nilikuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi na dada fulani, ambao mie niliuona ni serious relationship,ambayo nilitegemea kunifikisha kwenye ndoa, if God wished. Nilimaliza degree yangu hapo mlimani miaka miwili ilopita;baadaye nilikwenda Italy kwa masters yangu..kabla ya kusafiri nilianzisha uhusiano na dada fulani aliyekuwa anamalizia degree ya medicine,na kwakweli nilimpenda na niliamini naye alinipenda. Kwa kipindi chote nilipokuwa chuoni huko tuliwasiliana na nilimtumia pesa nyingi tu kuliko hata nilivyowatumia ndugu zangu. Nilivyorudi mwanzoni mwa mwaka huu, alikuwa kesha badilika kimwenendo na tabia., akawa ni mtu wa kupenda kujirusha, kwenda night clubs hata nikimuonya hanielewi tena. Kwahakika hata life standard and stile yake ilibadilika kutokana na pesa nilizokuwa nikimtumia. Muda si mrefu nikapata habari kuwa anauhusiano wa kimapenzi na kijana fulani ati anafanya ikulu. Nilifuatilia nikapata uhakika. Niliumia sana na katika harakati za kutaka arudishe gari dogo nililomnunulia, nilimfata Moshi alikokuwa amekwenda, ofcourse nilimfata huko baada ya kusikia kuwa akirudi dar atakaa siku moja then atakuwa safarini China. Basi nilikwenda huko na akanikimbia, niliamua kurudi. Nilipofika maeneo ya Korogwe nilipata ajali mbaya ya gari na niliponea chupuchupu kwani gari yangu ilikuwa ikiwaka moto ndipo walitokea wasamaria wema wakanichomoa. Yule dada alipata taarifa yeye na hata wazazi wake, lakini kwakipindi chote nilichokuwa hospitalini sikuwahi pokea hata SMS ya kunipa pole. Ndugu zangu imefikia hatua sasa sitaki kujikubali na hali hii. Nimejitahidi kusamehe na kusahau, lakini ninashindwa.ukweli nahitaji msaada wa ushauri na faraja ya wote walioguswa na mkasa huu.
Kwanza namshukuru Mwenyezi Mungu kwa baraka na rehema zake kwangu. Kwa ufupi nimepitia ktk kipindi cha majaribu..iko. hivi, :Nilikuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi na dada fulani, ambao mie niliuona ni serious relationship,ambayo nilitegemea kunifikisha kwenye ndoa, if God wished. Nilimaliza degree yangu hapo mlimani miaka miwili ilopita;baadaye nilikwenda Italy kwa masters yangu..kabla ya kusafiri nilianzisha uhusiano na dada fulani aliyekuwa anamalizia degree ya medicine,na kwakweli nilimpenda na niliamini naye alinipenda. Kwa kipindi chote nilipokuwa chuoni huko tuliwasiliana na nilimtumia pesa nyingi tu kuliko hata nilivyowatumia ndugu zangu. Nilivyorudi mwanzoni mwa mwaka huu, alikuwa kesha badilika kimwenendo na tabia., akawa ni mtu wa kupenda kujirusha, kwenda night clubs hata nikimuonya hanielewi tena. Kwahakika hata life standard and stile yake ilibadilika kutokana na pesa nilizokuwa nikimtumia. Muda si mrefu nikapata habari kuwa anauhusiano wa kimapenzi na kijana fulani ati anafanya ikulu. Nilifuatilia nikapata uhakika. Niliumia sana na katika harakati za kutaka arudishe gari dogo nililomnunulia, nilimfata Moshi alikokuwa amekwenda, ofcourse nilimfata huko baada ya kusikia kuwa akirudi dar atakaa siku moja then atakuwa safarini China. Basi nilikwenda huko na akanikimbia, niliamua kurudi. Nilipofika maeneo ya Korogwe nilipata ajali mbaya ya gari na niliponea chupuchupu kwani gari yangu ilikuwa ikiwaka moto ndipo walitokea wasamaria wema wakanichomoa. Yule dada alipata taarifa yeye na hata wazazi wake, lakini kwakipindi chote nilichokuwa hospitalini sikuwahi pokea hata SMS ya kunipa pole. Ndugu zangu imefikia hatua sasa sitaki kujikubali na hali hii. Nimejitahidi kusamehe na kusahau, lakini ninashindwa.ukweli nahitaji msaada wa ushauri na faraja ya wote walioguswa na mkasa huu.