1kush africa
JF-Expert Member
- Dec 13, 2016
- 10,137
- 14,233
Dah pole sanaa mdogo wangu!Ila bro ile Pm yako sijaweza kuifungua co Pm yangu inazingua maana ata baada ya kuirestart simu bado imegoma kufnguka so yale material ulionitumia bado sijafanikiwa kuyasoma mkuu
Ila shukuru hapo hujatoa mahali, je ungekuwa umetoa mahali?
Mda mwingine kuyumba kwetu kiuchumi huwa inakuwa sababu moja wapo ya hawa mabinti kutukimbia hasa tunapokuwa tushaanza relation,,
Wenzetu huwa hawakai na kitu moyoni,, huwezi amini yale yote yaliyotea kabla na baada, ameshaongea kwao,, kuna wale mama wadogo, mashangazi na mabibi wameshapitisha uamuzi kuwa aachane na wewe, ila hawezi kukwambia kuwa ameshauriwa ivo,,
Cha kufanya mdogo wangu kama wewe una hofu na Mungu anza kusali, hii itakupa mguvu mpya kidogo kuona unapunguza mzigo uliopo kichwani,, alafu jaribu kuwasimulia wakubwa wako kama makaka zako,, hao watakupa ushauri utakao kujenga vizuri kuanzia sasa, alafu hao hao kaka zako utagundua kuwa wapo waliopitia hayo uliyopita wewe na mda mwingine huenda wao waliumizwa zaidi yako sema ndo ivo walipigana wakatoka ktk hicho kifungo huru,,
Mawazo hayataisha leo wala kesho hadi pale utakapopata tulizo la nafsi yako, na hata ukipata bado utakuwa unakumbuka kumbuka haya yaliyokea, kwa sababu ulishamwingiza moyoni, na ukumbuke kumtoa mtu moyon hasa mpenzi si kitu rahisi kama vile unavodhani,, ila kikubwa unahitaji kujichanganya sana na marafiki ili kupunguza msongo wa mawazo,, hata kg nahisi zimepungua kwako.
Jaribu kukumbuka kabla ya kuwa naye je ulikuwa unapata pesa na inakaa? Je matumizi yaliongezeka sanaa? Kama jibu ndiyo basi tambua kwamba nia yako haikuwa mbaya ila ni kwamba hukujiandaa kubeba mahitaji yake yote,, sasa na yeye alivoona ivo uvumilivu ukamshinda na saa nyingine alisingizia akatibiwe kwao labda alihisi kuendelea kukaa hapo angezidi kuumia zaidi,, hawa viumbe wanafikri mara nyingi kuliko sisi,,
Mdongo wangu huyo hakuwa fungu lako ndo maana umempigania kadri ulivojaliwa, mda mwingine ulijinyima na pia ulikopa mahala flani na pia amekuachia madeni kadhaa japo unayajaribu kuyalipa lakini ndo ivo,, japo si kweli kama una madeni mengi [emoji23]
Ila bado na wewe sijajua mapungufu yako yapi maaana hizi kesi za upande mmoja huwa tunatoa majibu kwa upande huo huo,, ila kama na yeye angeongea yake basi huenda tungegundua mengi zaidi ambayo yamejificha,
PITIA HII KWANZA ALAFU UTOE COMMENT YAKO KIJANA,,
Nna mengi ya kuandika mdogo wangu basi tuuuu huku kutype kunaninyima uhuru wa kuandika hapa,