Msaada wa tabibu bingwa wa Vidonda vya Kisukari

Msaada wa tabibu bingwa wa Vidonda vya Kisukari

Sarikiaeli

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2020
Posts
971
Reaction score
1,606
Habari ya uzima wakuu ! Naomba msaada wa haraka, kwa ajili ya ndugu yangu, sawa kichwa cha habari hapo juu.

Ndugu yangu, amepatwa na changamoto kubwa ya ugonjwa wa kisukari, unaombatana na vidonda vikubwa hasa miguu yote!

Hivyo, naomba ushauri wenu wakuu mahali hapa, hasa kwa wenye ushuhuda wa watu walipona vidonda vinavyotokana na ugonjwa wa kisukari cha kurithi.

Asante sana kwa ushirikiano.
 
Hivyo vidonda vina muda gani tangu vitokee?
Mguu mmoja ni zaidi ya mwaka, kilitibiwa na kuonekana kupona kwa nje; kumbe kwa ndani wadudu waliendelea kuongezeka na sasa kumejitokeza kwa nje na kuna tishio la kukata sehemu ya mguu mmoja huo 😭
 
Mguu mmoja ni zaidi ya mwaka, kilitibiwa na kuonekana kupona kwa nje; kumbe kwa ndani wadudu waliendelea kuongezeka na sasa kumejitokeza kwa nje na kuna tishio la kukata sehemu ya mguu mmoja huo 😭

Pia, na mguu wa pili, nao umetoa kidonda kikubwa hivi karibuni na kupata taabu sana kutembelea kwa sasa 😭
 
Habari ya uzima wakuu ! Naomba msaada wa haraka, kwa ajili ya ndugu yangu, sawa kichwa cha habari hapo juu.

Ndugu yangu, amepatwa na changamoto kubwa ya ugonjwa wa kisukari, unaombatana na vidonda vikubwa hasa miguu yote!

Hivyo, naomba ushauri wenu wakuu mahali hapa, hasa kwa wenye ushuhuda wa watu walipona vidonda vinavyotokana na ugonjwa wa kisukari cha kurithi.

Asante sana kwa ushirikiano.

Nyongeza ni kwamba, ugonjwa wa kisukari huo, umepelekea tatizo kubwa la KUSHINDWA kufanya kazi kwa figo ZOTE mbili kwa ndugu yangu; na hivyo anapata huduma ya kuchuja sumu [dialysis], mara tatu kwa wiki kwa zaidi ya mwaka 1+ 😭
 
Pole sana hebu pitia hapa

Vidonda vitokanavyo na ugonjwa wa sukari (diabetic wounds/ulcers) vinahitaji uangalizi wa hali ya juu kwa sababu hupona polepole na vinaweza kuwa hatari. Tiba asilia zinaweza kusaidia, lakini ni muhimu zitumike kwa tahadhari na sambamba na ushauri wa daktari.

1. Asali ya Asili (Raw Honey)

Ina antibacterial na anti-inflammatory properties.

Tumia asali safi kwenye kidonda, funika kwa bandeji safi.

Badilisha kila siku au kila baada ya masaa 12.

2. Aloe Vera

Inapunguza uvimbe na huongeza kasi ya ukuaji wa ngozi mpya.

Tumia gel halisi ya aloe vera (kutoka kwenye mmea), paka juu ya kidonda mara 2 kwa siku.


3. Mafuta ya Nazi (Virgin Coconut Oil)

Huzuia kuvu na bakteria.

Paka kiasi kidogo kwenye kidonda kilichosafishwa.

4. Majani ya Mprapai (Papaya) Mbichi

Enzymes kwenye papaya huondoa seli zilizokufa.

Saga majani au tunda bichi la mpapai, paka juu ya kidonda, funika kwa bandeji.

5. Neem (Muarobaini)

Dawa ya asili dhidi ya bakteria.

Saga majani na tumia kama dawa ya kupaka au loweka maji ya neem kuosha kidonda.

1. Safisha kidonda kila siku kwa maji safi ya uvuguvugu na chumvi kidogo.

2. Usifunge kidonda sana – litahitaji hewa ili kupona.

3. Epuka sukari kupanda – vidonda haviwezi kupona kama sukari iko juu.

4. Usikate ngozi au kucha karibu na kidonda bila ushauri wa daktari.

5. Nenda hospitali mara moja ikiwa kidonda kinatoa harufu, kina rangi nyeusi, au kina maumivu makali.
 
Mgonjwa yupo Dar Es Salaam.
Kuna mtu yupo Sinza kwa Lemi, pharmasist alimsaidia mtu wa hiyo shida. Kama upo interested nikupe mawasiliano yake, ukutane nae, umweleze shida labda na mgonjwa awepo. Kisha utaamua mwenyewe amtibu au hapana.

Namba siwez kuweka hapa, hajaniambia nimtangaze
 
Kuna mtu yupo Sinza kwa Lemi, pharmasist alimsaidia mtu wa hiyo shida. Kama upo interested nikupe mawasiliano yake, ukutane nae, umweleze shida labda na mgonjwa awepo. Kisha utaamua mwenyewe amtibu au hapana.

Namba siwez kuweka hapa, hajaniambia nimtangaze

Asante sana kwa maelezo Bill na tutafanyia kazi ushauri wako.
 
Pole sana hebu pitia hapa

Vidonda vitokanavyo na ugonjwa wa sukari (diabetic wounds/ulcers) vinahitaji uangalizi wa hali ya juu kwa sababu hupona polepole na vinaweza kuwa hatari. Tiba asilia zinaweza kusaidia, lakini ni muhimu zitumike kwa tahadhari na sambamba na ushauri wa daktari.

1. Asali ya Asili (Raw Honey)

Ina antibacterial na anti-inflammatory properties.

Tumia asali safi kwenye kidonda, funika kwa bandeji safi.

Badilisha kila siku au kila baada ya masaa 12.

2. Aloe Vera

Inapunguza uvimbe na huongeza kasi ya ukuaji wa ngozi mpya.

Tumia gel halisi ya aloe vera (kutoka kwenye mmea), paka juu ya kidonda mara 2 kwa siku.


3. Mafuta ya Nazi (Virgin Coconut Oil)

Huzuia kuvu na bakteria.

Paka kiasi kidogo kwenye kidonda kilichosafishwa.

4. Majani ya Mprapai (Papaya) Mbichi

Enzymes kwenye papaya huondoa seli zilizokufa.

Saga majani au tunda bichi la mpapai, paka juu ya kidonda, funika kwa bandeji.

5. Neem (Muarobaini)

Dawa ya asili dhidi ya bakteria.

Saga majani na tumia kama dawa ya kupaka au loweka maji ya neem kuosha kidonda.

1. Safisha kidonda kila siku kwa maji safi ya uvuguvugu na chumvi kidogo.

2. Usifunge kidonda sana – litahitaji hewa ili kupona.

3. Epuka sukari kupanda – vidonda haviwezi kupona kama sukari iko juu.

4. Usikate ngozi au kucha karibu na kidonda bila ushauri wa daktari.

5. Nenda hospitali mara moja ikiwa kidonda kinatoa harufu, kina rangi nyeusi, au kina maumivu makali.
Ubarikiwe Kurunzi kwa ushauri kwetu familia.
 
Wakuu ! Bado nipo hapa kupokea msaada wa ushauri na maoni, kwa ajili yetu ya ndugu yangu na kwa faida wengine wanaopita hapa inaweza fursa kwao JF Member
 
Back
Top Bottom