Msaada wa sheria haraka jamani

makelejasitta

Member
Jan 25, 2017
24
3
Niliuziwa kiwanja tukagonganishwa watu wawili huko simiyu,Mimi nikawa nimewahi kujenga nyumba pale baadae akaja mwenzangu na yeye anadai kauziwa,kumbe aliyemuuzia alishafanyaga ujanja mapema kabla Mimi sijauziwa akajifanya kapoteza ile ofa ya kiwanja,akaenda polisi akaandikiwa loss riport,kwa hiyo mwenzangu aliyeuziwa na copy ya ofa aliyoipata kupitia loss riport,issue ikaenda mahakama ya mwanzo akashinda na ikaamuliwa kwamba Mimi niliyejenga nirudishiwe gharama za nyumba,baadae aliyeniuzia akakata rufaa mahakama ya wilaya ilipofika kule kesi ikafutwa kwamba hukumu ile haikutendewa haki harafu haikupaswa isikilizwe mahakama ya mwanzo Bali ilipaswa kwenda mahakama ya ardhi,ikaelekezwa kwa yeyote mwenye lalamiko aende katika sehemu ihusikayo na mambo ya ardhi yaani kwenye mabaraza ya ardhi au mahakama ya ardhi.wakakaa kimpya,mpaka Leo

Sasa Mimi nipo DSM tangu mwezi 12.Leo nimeambiwa yule MTU kapeleka mchanga pale kwenye nyumba yangu.kisheria natakiwa nichukue hatua gani,naomba mnisaidie wanasheria tafadhari
Ili kufikia asubuhi kama wanaendelea kujenga Mimi nijue cha kufanya
 
Gonga tu mlango wa wakili aliye jirani yako utapata msaada wenye manufaa, maana ni suala la kuchukua hatua za haraka hili .
 
mwenzangu hapo juu katoa mawasiliano ebu mcheki uwasiliane nae kwa msaada
swali mliuziana vipi bila mwenekiti pamoja na mashaidi? je mahakamani hamukuenda kubadili jina la hati ya kiwanja?
 
Masuala ya kuuziana ardhi huongozwa na kanuni iitwayo "Buyer be awere" yaani mnunuzi ni LAZIMA kujiridhisha uhalali wa mmiliki wa kiwanja n.k km wew ndiye uliuziwa wa kwanz kwa mmiliki halali na kwa mkataba wa kimaandishi na mashahidi. Waweza omba order ya mahakama kustopisha uo ujenzi then unaendeleza shauli kwny mabaraza ya ardhi.
 
mwenzangu hapo juu katoa mawasiliano ebu mcheki uwasiliane nae kwa msaada
swali mliuziana vipi bila mwenekiti pamoja na mashaidi? je mahakamani hamukuenda kubadili jina la hati ya kiwanja?
Mimi nimenunua kutoka kwa Rafiki yangu jina anaitwa baraka tunaaminiana sana,yeye naye alikinunua kwa MTU jina anto ila huyu anto alikinunua kwa mmliki wa kwanza jina suda.tatizo anto alipouziwa akapewa offer na nyaraka zingine zote ila hawakubadilisha jina baadae akamuuzia baraka,akakabizishwa kwa suda wakakubaliana kwamba wakafanye transifer kutoka suda moja kwa moja kwenda kwa baraka.sema yule jamaa alikuwa anzamzungusha kwenda kufanya transifer.sasa baraka akaenda masomoni akaondoka hawajamaliza kufanya hiyo transfer akiwa anajua hakuna tatizo,akaacha maagizo waanze kukiendeleza kile kiwanja aliowaacha pale nyumbani,wakaanza ujenzi,kabla hajaimaliza ile nyumba akapata ajila mkoa wa Dodoma.baadae alivyorudi nyumbani akaniambia sasa aniachie niendeleze nikakubali nikamuuliza kina ile offer IPO ila transfer bado kina jina la yule mmiliki wa kwanza yaani suda.twende ukajilidhishe tukaenda mpaka kwa suda.suda akathibitisha alishawauzia Siku nyi ngi kidogo.basi nikaamini.akaiacha sasa ile offer.nikaenda nayo ardhi wakasema hakina tatizo.nikamlipa yule Jamaa najua hakuna tatizo.nikaendelea na ujenzi mpaka nikamaliza.

Kumbe huyo suda ndiye katufanyia mchezo alipoona hawajabadilisha muda mrefu.kaenda polisi katoa maelezo eti alipoteza offer hivyo akapewa loss riport basi akarudi ardhi akamuuzia MTU mwingine.

Nilishangaa MTU analeta mchanga kwenye nyumba yangu kuja kurudi ardhi,kiwanja kina mgogoro wa wamiliki wawili.


Sijui nifanyaje ili haki yangu isipotee
 
Ulienda kwenye bazara la ardhi? Kama uamuzi ulishatolewa na haukuwepo nenda kaombe injunction kuzuia shughuli zozote kwenye hiko kiwanja mpka kesi ya msingi itakapoisha. Ila jitahidi kupata wakili atakuwa na msaada sana kwako.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom