Msaada wa haraka, mama amebambikiwa kesi

X_INTELLIGENCE

JF-Expert Member
Mar 25, 2014
9,680
12,255
Wana JF mimi na familia yangu tunaitaji msaada wenu kisheria juu ya kesi inayo mkabili mama yetu.

Kuna mambo ya mila ambayo yalisababisha sisi tuwe mbali na bibi yetu mzaa mama, yaani tulimpenda kama bibi ila tulikuwa hatushirikiani nae kwalolote

Siku moja bibi alikuja nyumbani wakayasuluhisha tulimpokea tukaishi nae nyumbani, bibi yetu ana nyumba sita hapa mjini ila sisi kutokana na kutoelewana sana na bibi mama hakupenda kwenda kuishi kwenye nyumba za bibi

Kutokana na mapatano yetu na bibi hatimae tulianza kuishi na bibi nyumbani kwetu tulipo panga, bibi yetu ana watoto sita 6 ambapo mama yetu ndio wa kwanza.

Kutokana na hali ngumu ya maisha aliyotukuta nayo bibi pale nyumbani aliamua kumwambia mama kuwa yupo tayari kuuza nyumba zake 2 ili aweze kutusaidia, mama alikubaliana nae.

Mama akatafuta mnunuaji wa zile nyumba ambazo bibi alilizia kuziuza zile nyumba ziliuzwa milioni 50, bibi alienda mahakamani ili kukamilisha mauziano ambapo alikiri kukubari kuuza nyumba zake na mama yetu ndie mrithi wake ambapo yeye mama yetu alisimama kama shahidi.

Nyumba ziliuzwa kisha bibi akamwambia mama anunue kiwanja ajenge nyumba, mama alifanya kama alivyoagizwa huku bibi akimsisitiza kuwa hati zote za hii nyumba mpya aandike majina yake {mama aandike majina yake} ili wajomba zetu na mama zetu wadogo wasije kuhusika kwenye hiyo nyumba mpya.

Baada ya zile fedha kutumika kwenye ujenzi na matumizi mengine ya pale nyumbani, zilibakia kiasi kidogo kama milioni 8 ivi.

Siku moja bibi alimuita mama akamwambia nimekupa kila unachokita mwanangu naomba uwe mrithi wa huu mfuko wangu wa UCHAWI, mama alikataa kata kata hapo ndio ugomvi baina ya mama na bibi ulipo rudi upya.

Bibi aliondoka nyumbani akaenda kwa wanae wengine ambao hawakuhusishwa kwenye mauzo ya zile nyumba mbili, akawaambia kuwa mama yetu kamshawishi kuuza nyumba bila idhini yake.

Wakashirikiana wamefungua kesi ambayo inamuendesha sana mama angu.

Kwa yeyote atakaeguswa na hili tatizo tafadhali tunaomba msaada wa sheria kwani mama alilala mahabusu akafikishwa mahakamani tukamtolea zamana mahakama iliamua kuwa mama arudishe zile fedha milion 50 ambazo matumizi yote yalikuwa yanatoka kwa idhini ya bibi.
 
Mbona hiyo case ni nyepesi sana na kama mkimpata lawyer mahiri mtawashinda kabisa hawo wajomba na mama wadogo, kimsingi wao hawahusiki na hiyo nyumba aliyojengewa mama yenu na bibi yenu, ile hati ya nyumba iliyokuwa na jina la mama yenu ndio msingi na ngao kubwa kwenu.

Hao ndugu wanadai nyumba ambayo hawana uhusiano wowote ule nayo,hiyo nyumba ni ya mama yenu kutokana na jina la mama yenu kuandikwa ktk hati za nyumba.Wao kama ndugu hawana power yeyote ya kugeuza fikra za mahakama kuwa na wao wanahusika ktk hiyo nyumba.Mwenye jina ndio mwenye nyumba na mahakama haitoweza kuwanyang'anyeni hiyo nyumba kwani kisheria ni mali yenu pamoja na mama yenu.

Ka hamna hela za kumpata lawyer mzuri jaribuni hata kwenda udsm kitengo cha law ili hata mpate mwanafunzi wa masuala ya litigation law ili awasaidieni kwa bure bila malipo yeyote yale.Nyie hamna haja ya kumtafuta heavy weight lawyer yeyote yule hiyo case yenu ni rahisi sana hata mwanafunzi aliye mzuri darasa la sheria ataiweza hiyo case na mtafaulu.

Murage Msherwampamba Goodluck.
 
Hiyo nyumba si imeandikwa kwa jina la mama yenu? Na bibi si aliuza nyumba zake kwa hiari na maandishi yapo? Hapo hakuna kesi ya maana, mali ni ya mama yenu. Tena kesi kama hiyo (madai) haikuwa halali mama ashikiliwe mahabusu. Hebu sema kesi yenyewe iko mahakama gani na madai yao au shtaka hasa ni nini
 
Hiyo nyumba si imeandikwa kwa jina la mama yenu? Na bibi si aliuza nyumba zake kwa hiari na maandishi yapo? Hapo hakuna kesi ya maana, mali ni ya mama yenu. Tena kesi kama hiyo (madai) haikuwa halali mama ashikiliwe mahabusu. Hebu sema kesi yenyewe iko mahakama gani na madai yao au shtaka hasa ni nini

wamemfungulia kesi ya wizi wa kuamini mlalamikaji akiwa ni bibi kuwa mama ameuza nyumba kwa kumshawishi yeye bibi hakuta na vile vile kuhusu matumizi ya fedha
 
Dragoon

Hii sammary ya Mkuu Dragoon nimeipenda muitiliye mkazo na mtashinda tuu,na hilo la suala la mkoba wa uchawi nendeni kwa baraza la wazee wa kabila lenu hilo litaweza tatuliwa kutokana na tamaduni na history ya kabila lenu.Murage Msherwampamba.Peace and good luck again.
 
Last edited by a moderator:
sijajua ni kwanini kesi hiyo imegeuzwa kuwa ya jinai hali kwakuisikiliza tu ni kessi ya madai. kabla yakutoa ushauri napenda kusema polisi wakula hela. ushauri wangu ni kuwa tafuteni mwanasheria wa haki za binadamu pale kinondoni,magomeni na maeneo ya mwenge. kesi hiyo irudishwa baraza la ardhi la kata na kisha liende wilaya na baadaye mahakama kuu. hawo wajomba hawana locus standae ya kuisntitute case dhidi ya mama yenu labda kama huyo bibi atakuwa amewapa hati ya kesheria inayowaruhusu wao washitake kwaniaba yake.
 
MASEETO

Kama unamwelekeza aende Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu, basi kituo cha msaada wa sheria kipo Kinondoni Kanisani >>> barabara ya dunga kupitia hombus>>> kona ya kwanza kushoto baada ya kumaliza ukuta wa kabisa la TAG.

Wanatoa huduma jumatatu, jumanne, alhamisi na ijumaa kuanzia saa tatu kamili asubuhi mpaka saa sita kamili mchana.

Gharama ni shilingi elfu 2.
 
Last edited by a moderator:
Hii sammary ya Mkuu Dragoon nimeipenda muitiliye mkazo na mtashinda tuu,na hilo la suala la mkoba wa uchawi nendeni kwa baraza la wazee wa kabila lenu hilo litaweza tatuliwa kutokana na tamaduni na history ya kabila lenu.Murage Msherwampamba.Peace and good luck again.

asante kwa ushauri wako Mungu akubariki sana
 
Kama unamwelekeza aende Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu, basi kituo cha msaada wa sheria kipo Kinondoni Kanisani >>> barabara ya dunga kupitia hombus>>> kona ya kwanza kushoto baada ya kumaliza ukuta wa kabisa la TAG. Wanatoa huduma jumatatu, jumanne, alhamisi na ijumaa kuanzia saa tatu kamili asubuhi mpaka saa sita kamili mchana. Gharama ni shilingi elfu 2.

asante nitaufanyia kazi ushauri wako
 
MASEETO

bibi ndio mlalamikaji hawakilishwi na mtu yeyote ila wanae wanalalamika kifamilia kuhusu fedha ambazo mama alikuwa anapokea maagizo ya kuzitumia kwa bibi...kuwa na wao wangepewa au kuhusishwa kwenye uhuzaji...
 
Last edited by a moderator:
Eddy pamoja na kwenda kisheria pia jaribu kuwaona wachugaji msaada wa KIMUNGU unahitajika pia hapo ur chasing a ghost take my words
 
Nashindwa kuelewa kwa nini huyo bibi asingeruhusu tu mukae kwenye hiyo nyumba yake aliyouza badala ya kuuza na kutoa hela mkajenge nyingine. Pia kama nyumba ilikuwa ya bibi yenu, naona kama huyo bibi yenu hakuwafanyia fair watoto wake wengine maana kama ni urithi kila mtoto anastahili apate haki yake. Ndio maana wajomba zenu na mama wadgo wamepata mwanya wa kuungana na bibi yenu kumkandamiza mama yenu kwasababu wanahis alidhulumu mali ya familia kwa manufaa yake binafs. Tuwe makini sana kwenye mali za familia ili kuepuka migogoro isiyo ya lazma. Na sis watoto ni vema tukatumia nafasi zetu vizuri kuwashauuri wazaz pindi wazazi wetu wanapotaka kuuza mali za wazazi wao bila kuwashirikisha ndgu zao wa damu. Kuna mengi sana ya kujifunza hapa.
 
Nashindwa kuelewa kwa nini huyo bibi asingeruhusu tu mukae kwenye hiyo nyumba yake aliyouza badala ya kuuza na kutoa hela mkajenge nyingine. Pia kama nyumba ilikuwa ya bibi yenu, naona kama huyo bibi yenu hakuwafanyia fair watoto wake wengine maana kama ni urithi kila mtoto anastahili apate haki yake. Ndio maana wajomba zenu na mama wadgo wamepata mwanya wa kuungana na bibi yenu kumkandamiza mama yenu kwasababu wanahis alidhulumu mali ya familia kwa manufaa yake binafs. Tuwe makini sana kwenye mali za familia ili kuepuka migogoro isiyo ya lazma. Na sis watoto ni vema tukatumia nafasi zetu vizuri kuwashauuri wazaz pindi wazazi wetu wanapotaka kuuza mali za wazazi wao bila kuwashirikisha ndgu zao wa damu. Kuna mengi sana ya kujifunza hapa.

mAMA WA WATU WALA HAJAKOSA UMAKINI,

angefanya umakini gani zaidi ya kuhakikisha kuwa mambo yote yanafuata mkondo wa sheria kama yalivyofanyika.

Nadhani kuna kitu umekiruka. Bibi ni mchawi na aliyafanya yote hayo ili mmama wa watu akubali kurithi mikoba, na nahisi hata ugonvi wa mwanzo ulitokana na hilo la kurithi uchawi.

kesi nyepesi ila inabidi mama ajue jinsi ya kujitetea na jinsi ya kumbana mamake (bibi) maswali pale kwa pilato
 
Back
Top Bottom