Msaada wa mawazo

Msaada wa mawazo

Vaislay

JF-Expert Member
Joined
Jun 26, 2011
Posts
4,532
Reaction score
1,840
Nilikuwa nasoma na kusikia ishu za kina Vicky Kamata lakini leo limefika mikononi...

Mdogo wangu alitaraji kufunga ndoa hivi soon shughuli zoote mnazozijua za maandalizi zilifika ukingoni...
Siku nne zilizopita nilipata simu ya Mume mtarajiwa akiniambia alikuta mesej ya mdogo wangu akitumiwa na daktari aliyemtibu kipindi flani akiwa anaumwa...ikisema " swit mbona umekiwa kimya mda mrefu"
mume akuuliza mke mtaraji kulikoni bibie akachomoa...
mume akaelewa...sasa gafla yule mume kaibuka kusitisha ndoa kwa madai tu hataki kuolea watu...
Ndugu wa familia tumejaribu kuongea na binti amtake radhi mwenzie binti nae kaibuka hataki kosa wanaume anajidai mkoloni..

Vichwa vinasugua na nywele kunyonyoka hatujui hata lakufanya garama zilizotumika kuandaa..michango ya watu yaaaani.....hoooooiiii

nisaidieni mawazo kunusuru hili balaaa...ndoa imebakiza siku chache tu ...
 
Hamna ndoa hapo hata wakioana leo hawatadumu
 
Mshaurini huyo binti kukubali kosa na kuomba radhi naamini mwanaume atamwelewa.
Lakini akijifanya kukomaa atapotea ...
Lakini wanawake wa siku hizi wanaangalia maslai tu
 
Mshaurini huyo binti kukubali kosa na kuomba radhi naamini mwanaume atamwelewa.
Lakini akijifanya kukomaa atapotea ...
Lakini wanawake wa siku hizi wanaangalia maslai tu

kama kupotea ameshapotea,hilo la kuomba msamaha tumeongea mpaka ....yaani sijui ni nini hiki
 
Kwa sasa hivi nyie mnachofikiria tu ni your family reputation and nothing else. Kama wanaona kuna tabia hawaendani, wapeni muda kidogo waone kama wataweza kucopy. Wakishindwa rudisheni tu michango ya watu (utekelezaji wa hili ni mgumu uuuh). But haina maana pia watu waoane leo, afu after siku 2 waachane while dalili mbaya mshaziona
 
anataka kumuolea doc... ata mimi ningekimbia mbio, ugonjwa tu katoka na daktari, gari likiaribika atatoka na fundi garage, hapo sio pa kukaa....

khaaaa! umenifanya nicheke bila kupenda
 
Kwa sasa hivi nyie mnachofikiria tu ni your family reputation and nothing else. Kama wanaona kuna tabia hawaendani, wapeni muda kidogo waone kama wataweza kucopy. Wakishindwa rudisheni tu michango ya watu (utekelezaji wa hili ni mgumu uuuh). But haina maana pia watu waoane leo, afu after siku 2 waachane while dalili mbaya mshaziona

yaani hawa watu uhusiano wao kama ni mtoto basi angekuwa darasa la tano sahizi ( nikimaanisha uhusiano wao ulikuwa wa muda mrefu tu) kwa muda wote huo naimani wanafahamiana vizuri tu...kama kukwaruzana walishakwaruzana sana tu..kwanini hili limewashinda?

Binti akiulizwa kama anamtaka huyo doc anasema hamtaki na hana uhusiano nae...

labda tuwape muda tena...
 
Mwacheni mume akatafute atkae mpenda Huyo dk hatomuacha Huyo binti, ndoa ni kifungo jamani
 
yaani hawa watu uhusiano wao kama ni mtoto basi angekuwa darasa la tano sahizi ( nikimaanisha uhusiano wao ulikuwa wa muda mrefu tu) kwa muda wote huo naimani wanafahamiana vizuri tu...kama kukwaruzana walishakwaruzana sana tu..kwanini hili limewashinda?

Binti akiulizwa kama anamtaka huyo doc anasema hamtaki na hana uhusiano nae...

labda tuwape muda tena...

Sasa inakuwaje wanaanza kusumbuana huku mwishoni kabisa. Afu inaonekana kila mtu hataki kujishusha hapo. Nyie jaribuni kuwaita wote wawili, kaeni nao chini then mjue ni nini tatizo haswa. From there mtaamua kusuka au kunyoa
 
Kitendo cha mwanamke kufanya kosa nikamwambia afu akakataa wakati ni kweli HUWA NASIKIA KUTAPIKA, Inaonekana huyo mdogo wako ana tabia mbaya , sio kila mwanamke huwa anatakiwa kuolewa rudisheni michango ya watu.
 
Sasa inakuwaje wanaanza kusumbuana huku mwishoni kabisa. Afu inaonekana kila mtu hataki kujishusha hapo. Nyie jaribuni kuwaita wote wawili, kaeni nao chini then mjue ni nini tatizo haswa. From there mtaamua kusuka au kunyoa

yaani kama upo...kila mtu yuko juu
mwanaume anasema hata wakikaa chini wote wataongea nini kipya..
ni mvurugano mtupu..

ushauri wako mzuri...itabidi tulazimishe uwepo wa wote..
 
huyo jamaa mungu wake mkubwa!! bora kayaona kabla hajafunga ndoa.

Grand PA
 
Huyo mwanaume kafanya jema, kaona mbali. Namsapoti.

Mchukueni binti yenu mwambieni aanze upya, hela za watu mrudishe sio kuwaza kula na kunywa kumbe mnafurahia bomu litakalokuja kulipuko ASAP.
 
If I got the chance ya kuongea na huyo bwana harusi ningemwambia, 'Kaka, kimbia!'. Kama mwanamke ameonyesha utata hivyo kbla ya ndoa, mwanaume anaenda kuolewa huyo. Anyway hiyo sio mada.

Weka vitu kwenye mizani, umuhimu wa hii ndoa kuendelea na reputation ya familia yenu na the scandal. Lipi bora? Huyo mwanaume anaweza akamuoa, sawa. Lakini je, unadhani itakuwa rahisi kwake kusahau hii ishu? Wont it backfire later? Seems like a timed bomb huh?

Wapeni muda wenyewe wajifikirie. Sogezeni mbele hiyo harusi. Let them sort this one out themselves. Kwani wakishaoana mtakuepo? Wakiona wanaweza kuendelea fine. Otherwise thank God kaepusha balaa.
 
Mhhhh! Poleni sana! Majanga tena si madogo.
 
Back
Top Bottom