Pap Joh
Member
- Aug 18, 2019
- 69
- 48
Habarini ndugu zangu wanaJf,
Naomba niende moja kwa moja kwenye mada, kama ifuatavyo:
Mimi ni kijana wa kiume, kwa sasa nipo Dodoma na umri wangu ni 27.
Nimefikia hatua ya kuamua kutoka huku nilipo na kwenda Dar, kwa ajili ya utafutaji wa maisha. Kwa kifupi nimejipanga vizuri, kuhakikisha napiga hatua fulani za kimaendeleo, kwenye yale ninayotegemea kwenda kuyafanya. Hivyo namuomba Mwenyezi Mungu tu anifanyie wepesi...
Sasa shida kubwa ninayoiona mbele yangu, ni kukosa ndugu/jamaa ambaye angeweza kunipatia msaada huo wa makazi. Hivyo nimetafakari sana, kisha nikaona hakuna ubaya kama nikija kwenu wanandugu wa JF kuomba msaada huo wa makazi.
Naomba kupata msaada wa makazi, kwa muda usiozidi miezi miwili tu. Na katika kipindi hiko chote, itakuwa ni msaada wa kupata sehemu ya kujihifadhi tu, kuhusu mambo ya kula na mengineyo NITAJITEGEMEA. Ila pia Mungu akinijali kufikia malengo yangu mapema, basi nitakuwa nami natoa mchango wangu wa kulipia baadhi ya bill mfano maji, umeme n.k
Kuhusu tabia:
Binafsi sina utamaduni wa kutumia kilevi cha aina yoyote ile. Ila pia sina kabisa tabia ya tamaa....
Hivyo naweza kuhitimisha kwa kusema, naweza kuishi na watu vizuri.
Tafadhalini sana wadau wa Jf, naombeni msaada wenu wapendwa....hali yangu sio nzuri kabisa.
Asante.
Naomba niende moja kwa moja kwenye mada, kama ifuatavyo:
Mimi ni kijana wa kiume, kwa sasa nipo Dodoma na umri wangu ni 27.
Nimefikia hatua ya kuamua kutoka huku nilipo na kwenda Dar, kwa ajili ya utafutaji wa maisha. Kwa kifupi nimejipanga vizuri, kuhakikisha napiga hatua fulani za kimaendeleo, kwenye yale ninayotegemea kwenda kuyafanya. Hivyo namuomba Mwenyezi Mungu tu anifanyie wepesi...
Sasa shida kubwa ninayoiona mbele yangu, ni kukosa ndugu/jamaa ambaye angeweza kunipatia msaada huo wa makazi. Hivyo nimetafakari sana, kisha nikaona hakuna ubaya kama nikija kwenu wanandugu wa JF kuomba msaada huo wa makazi.
Naomba kupata msaada wa makazi, kwa muda usiozidi miezi miwili tu. Na katika kipindi hiko chote, itakuwa ni msaada wa kupata sehemu ya kujihifadhi tu, kuhusu mambo ya kula na mengineyo NITAJITEGEMEA. Ila pia Mungu akinijali kufikia malengo yangu mapema, basi nitakuwa nami natoa mchango wangu wa kulipia baadhi ya bill mfano maji, umeme n.k
Kuhusu tabia:
Binafsi sina utamaduni wa kutumia kilevi cha aina yoyote ile. Ila pia sina kabisa tabia ya tamaa....
Hivyo naweza kuhitimisha kwa kusema, naweza kuishi na watu vizuri.
Tafadhalini sana wadau wa Jf, naombeni msaada wenu wapendwa....hali yangu sio nzuri kabisa.
Asante.