Msaada wa kisheria katika hili jambo

Amaizing Mimi

JF-Expert Member
Feb 2, 2019
477
1,066
Habari za muda wana JF.

Naomba nijikite kwenye mada moja kwa moja.

Jana watoto wa kakaangu walikuwa wanachunga ng'ombe huko kijijini kwetu.sasa kuna wanafunzi wawili wakawa wanarudi nyumbani kutoka shuleni.

Wale watoto wa kaka wakaanza kuwafukuza.(umri wa wale watoto wa kaka ni miaka 12 na 13). Wakati wanafukuza wakatokea watu wengine, wale watoto ikabidi wakimbie waache mifugo.wale jamaa wakaswaga ng'ombe hadi polisi,kufika polisi wale jamaa wakatoa maelezo kuwa wale watoto walikuwa wanataka kuwabaka wanafunzi.Leo kaka ameenda polisi akaambiwa awapeleke wale watotokwanza(wachungaji wa ng'ombe).

Kaka amefanya hivyo sasa baada ya kuongea sana polisi wanataka millioni tatu ili wkufuta kesi na pia ili kaka arudishiwe ng'ombe wake.

Naomba msaada namna ya kumnasua kaka ni hizi gharama maana milioni tatu ni hela nyingi mno.
 
Habari za muda wana JF.Naomba nijikite kwenye mada moja kwa moja.
Jana watoto wa kakaangu walikuwa wanachunga ng'ombe huko kijijini kwetu.sasa kuna wanafunzi wawili wakawa wanarudi nyumbani kutoka shuleni.
Wale watoto wa kaka wakaanza kuwafukuza.(umri wa wale watoto wa kaka ni miaka 12 na 13). Wakati wanafukuza wakatokea watu wengine,wale watoto ikabidi wakimbie waache mifugo.wale jamaa wakaswaga ng'ombe hadi polisi,kufika polisi wale jamaa wakatoa maelezo kuwa wale watoto walikuwa wanataka kuwabaka wanafunzi.Leo kaka ameenda polisi akaambiwa awapeleke wale watotokwanza(wachungaji wa ng'ombe).
Kaka amefanya hivyo.sasa baada ya kuongea sana polisi wanataka millioni tatu ili wkufuta kesi na pia ili kaka arudishiwe ng'ombe wake.
Naomba msaada namna ya kumnasua kaka ni hizi gharama maana milioni tatu ni hela nyingi mno.
kabla sijatoa mawazo yangu naomba kujua haya; 1:kwa nini hao watoto wa kaka walikuwa wanafukuza wanafunzi? 2:hao wanafunzi ni jinsia gani na umri gani? 3:kwa nini walikimbia na kuacha mifugo kama hakukuwa na kitu chochote kilichotokea?
4:Waliotaka kubakwa mazingira yalikuwaje?walitishiwa?walivutwa kichakani? au ilikuwaje? 5:na wamefunguliwa kesi ya kosa gani?
6:kama washtakiwa wameshafika kituoni au kukamatwa sasa kwa nini mifugo endelee kushikiliwa labda kama walikuwa wanachunga katika maeneo yasiyo ruhusiwa.
Binafsi naomba ufafanuzi wa hivyo vitu ili niweze kutoa mawazo yangu,pia uko mko gani? nafikiri ni vyema upate msaada wa kisheria(wakili)mapema.
 
Mtoe faini ili iwe fundisho kwa watoto wa kiume wenye tabia mbaya.
 
Habari za muda wana JF.

Naomba nijikite kwenye mada moja kwa moja.

Jana watoto wa kakaangu walikuwa wanachunga ng'ombe huko kijijini kwetu.sasa kuna wanafunzi wawili wakawa wanarudi nyumbani kutoka shuleni.

Wale watoto wa kaka wakaanza kuwafukuza.(umri wa wale watoto wa kaka ni miaka 12 na 13). Wakati wanafukuza wakatokea watu wengine, wale watoto ikabidi wakimbie waache mifugo.wale jamaa wakaswaga ng'ombe hadi polisi,kufika polisi wale jamaa wakatoa maelezo kuwa wale watoto walikuwa wanataka kuwabaka wanafunzi.Leo kaka ameenda polisi akaambiwa awapeleke wale watotokwanza(wachungaji wa ng'ombe).

Kaka amefanya hivyo sasa baada ya kuongea sana polisi wanataka millioni tatu ili wkufuta kesi na pia ili kaka arudishiwe ng'ombe wake.

Naomba msaada namna ya kumnasua kaka ni hizi gharama maana milioni tatu ni hela nyingi mno.
hapo kunaharufu ya rushwa, Ng'ombe waliokamatwa hawana uhusiano na tukio hivyo hakuna sababu ya kuwashikilia.

kuhusu kutoa pesa, polisi hawana mamlaka ya kuamua nani kafanya kosa. Ikiwa wanahitaji kujua mtendaji wa kosa wawapeleke hao watoto mahakamani. Maana mahakama ndio inawajibu huo.

hapo kinachotafutwa nirushwa tuu maana kesi yenyewe haina mashimo eti walikuwa wanataka. Lakini ushahidi upi? hapo nihakuna lolote.

Pesa msitoe waambie polisi wawapeleke mahakamani hakuna chaajabu zaidi ya rushwa hapo.
 
Polisi wa Bongo ni njaa tupu, wanapenda rushwa mnoo, hata utu hawana, afu hawaoni hata aibu case ya kubumba wanataka takrima daaah.

 
Back
Top Bottom