Uko sahihi!!WaTz tunapenda kuishi bila mipango, mtu unatoka nyumban kwenda mjini kununua viatu ila ukifika mjini unaanza kununua viatu nguo machungwa mashuka mapazia, wakati lengo lilikuwa kununua viatu tu.
Nataka kusema kwamba, ulitoka na gari nyumban kwenda kubadilisha balljoints, umefika garage fundi anakujaza upepo ufanye service na vitu vingine ambavyo hukupanga, wewe nawe unajaa upepo unasahau mwenzako anakujaza ili aongeze kukupiga pesa tu na wakati huo huo si mtaalam wa aina ya gari yako.
Hadi kufika hapo gari umeiharibu kwa kuruhusu fundi akurekebishie vitu ambavyo havikuwa kwenye mpango wako. Mkae mkijua haya magari akina benz, subaru, audi, range, ford, mazda, outlander nk. Si kila fundi anaweza kuyagusa basi ukiruhusu ayaguse mwambie aishie kwenye kubadili matairi na taa tu.
Hukumstua mkuu?Mafundi wa kibongo usipo kua makini wanaua gari yako. Na mbaya zaidi ukijifanya rafiki nae. Kuna siku nipo kwa fundi nikakuta kuna mteja kabla yangu nikasema nasubilia mpk umalizane na uyo. Kumbe mm nausoma mchezo wake kwenye ile gari mteja kaja na oil na filter na break pads zake zote mpya.Mteja akamwamini fundi Daaah nilicho shuhudia ni maafa au majanga ya kikatili kabisa. Uwezi amini fundi akubadilisha chochote kabisa kwenye ile gari. Kisha akachukua kadi ya service akamjazia kilometers 5000 tena kana kwamba kabadili.zile pads z zamani kapiga msasa tu. Kisha vile vitu kaenda kuuza dukani kwa bei ya hasara. Mteja kaja kalipa pesa za fundi kasepa zake.Gari linaenda kuua engine hv hv tu. Kwa njaa z fundi.
Kazi ni kipimo cha utu
Dah pole sana mkali. Hizi gari za Ulaya inabidi uwe unajua unachoenda kufanya kwa fundi, na sio yeye ndio akuamulie.Mad Max ile Volvo niliipeleka jamaa wanifanyie checkup na kubadili balljoint, baada ya gari kukaa sawa, wakasema transmission oil imepungua, nikasita, nikawaambis ikipungua 4l haiwezi kwenda, wakalazimisha iongezwe, hadi hapa tunapoongea, gari imepaki haiendi.
Ni garage yenye jina kubwa sana iko maeneo ya Makumbusho.
Hapa bado natafakari hatua sahihi za kuona namna ya kuirudisha barabarani. Hapo kwenye hiyo garage ilitafunwa takribani 2.5M na gari iliyoenda iko sawa isipokua kugonga chini, imefia hapo.
Rafiki yangu nae ana Aud, ilienda na tatizo la leakage, hapa nnapoandika huu uzi, imeshabadilishwa vitu vingi na ndio maradhi yanaongezeka.
Wale walivuruga sana kaka, na inavyoonekana walichanganya oili isiyo na kiwango. Sada hivi naona imeathiri torque converter, folk shift na zile selonoid, kwa ufupi gearbox ingine au hii hii ifanyiwe major repair itakayonigharim zaidi.Dah pole sana mkali. Hizi gari za Ulaya inabidi uwe unajua unachoenda kufanya kwa fundi, na sio yeye ndio akuamulie.
Kwanini usianze kwa kupiga OBD diagnosis, hafu kisha itafute transmission sahihi ubadirishe kwa kuanzia hapo
Kuna gearbox hazina dipstick.
Duuuuh uhuni wa kiwango cha lami,,an hawana huruma kabisaaa na gari ya mtu na mfuko wake bongo nyoso *****
Plugs mafundi wengi zinawashinda sababu hawajui namba sahihi ya plug zinazotakiwa kukaa kwenye gari husika. Mfano, gari la Toyota Ractis (2005), Plug yake original ni SK16HR11, sasa unakuta fundi anasema weka plug, kumbe kanunua SK16HR20, gari itakua inatetemeka mwanzo mwisho, na haina nguvu. Tujitahidi kutumia AI kuwasaidia mafundi angalau waache kubahatisha bahatishaMkuu mimi niliwahi nunulishwa vifaa almost milion na upuuzi pale gerezani haki kumbe shida ni plugs tu.... Na hizo plugs baada ya kujua ni shida nilinunulishwa kila aina ya plug. Kuna fundi alisema ni gearbox kidogo ninunue gearbox nyingine kumbe shida sio gearbox ni hizo hizo plug gari inatetemeka kama inakataa gear. Na hao ni mafundi wa garage maarufu hapa dar.
Fundi anaweza kufanya gari uichukie anakutia hasara na wala hajalim
Nafikiri anaitwa LEGEYule jamaa sijui anatumia ID GANI hapa ningemtag! Yupo Mwenge mtaalamu sana