Travelogue_tz
JF-Expert Member
- Sep 28, 2010
- 855
- 1,224
Wana JF,
Taarifa hii nimeipata sehemu na nimeona tushirikishane kwa nia ya kupata ushahidi zaidi juu ya Masharti ambayo Serikali ya China imetoa kwa Tanzania katika kile kilichotajwa kuwa Misaada isiyo na masharti magumu kwa nchi yetu.
Naomba wenye taarifa juu ya hili JF watuweke wazi, maana maaana China ya Mao na Tanzania ya Myerere sio za sasa. Kuna mabadiliko makubwa sana ya sera za kiuchumi.
Taarifa hii nimeipata sehemu na nimeona tushirikishane kwa nia ya kupata ushahidi zaidi juu ya Masharti ambayo Serikali ya China imetoa kwa Tanzania katika kile kilichotajwa kuwa Misaada isiyo na masharti magumu kwa nchi yetu.
"MAPYA ZAIDI YA MIKATABA KATI YA CHINA NA TANZANIA YAANZA KUBAINIKA"
Hebu soma kwa makini moja Kati ya mikataba 17 ya China na Tanzania waliyoisaini kufuatia ziara ya Rais wa China nchini Xi Jinping.
Taarifa kutoka vyanzo vya kuaminika vimebainisha masharti ambayo yameambatana na Moja ya Mkataba ulisainiwa ambao umelenga katika UJENZI WA BANDARI YA BAGAMOYO.
Mosi, Ili kufanikisha ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo Serikali ya Tanzania itachukua mkopo wa fedha toka serikali ya Uchina.
Pili, Makampuni ya China na Injinia wao ndio watapaswa kupatiwa tenda ya ujenzi wa mradi huo.
Tatu; Serikali ya watu wa China watatakiwa kuendesha bandari bandari hiyo kwa muda wa miaka 50 ili Kurudisha mkopo uliotolewa kwa ajili ya ujenzi wa mradi huo.
Nne; Itatakiwa kuwa kwa umbali wa Kilometa 200 za mraba Kusini, Mashariki, Magharibi na Kaskazini kusiwepo na na bandari ya namna hiyo wala kuendeleza bandari ya namna hiyo.
Kwa maana hiyo bandari ya Dar es Salaam ,Tanga na Mtwara kwa mantiki hii hazitapanuliwa wala kuboreshwa ili kutoa nafasi ya Bandari ya Bagamoyo iwe ya kwanza kwa ubora na hii itadumu kwa kipindi cha miaka 50.
Tano; Upanuzi wa bandari wa Gati 14 wa Bandari ya Dar es Salaam umesimamishwa au utasimamishwa ili kuipa ama kuheshimu na kulinda mkataba wa wachina kwa bandari ya BAGAMOYO
Hizo ni baadhi ya dondoo za mkataba mmoja tu.
Naomba wenye taarifa juu ya hili JF watuweke wazi, maana maaana China ya Mao na Tanzania ya Myerere sio za sasa. Kuna mabadiliko makubwa sana ya sera za kiuchumi.