Samahani wakuu naomba kueleweshwa nilifunguliwa kesi Kuhusu mirathi, kesi ya madai kuanzia mahakama ya mwanzo nikashinda, mdai akakata rufaa mahakama ya wilaya Napo akashindwa, akakata rufaa mahakama kuu, pia akashindwa.
Katika hukumu mahakama zote iliamriwa nilipwe gharama, lakini sikuweza kudai gharama Kwa muda huo kwani mdai alikuwa anakata rufaa mahakama ya juu. NI miaka 4 sasa imepita toka hukumu ya madai ya mahakama kuu iliyonipa ushindi lakini nilishindwa kudai gharama wakati huo kwani alipoona ameshindwa, mdai aligeukia kunifungulia kesi ya jinai, nayo imekwisha Kwa hakimu kuniona sina hatia.
Pamoja na hapo hajaridhika wamekata rufaa mahakama ya juu na kesi bado inaendelea.
Je, naweza kuanza kudai gharama za kesi zile za madai Kwa sasa NI miaka 4 imepita au nimechelewa?? Au nisubiri adi hii rufaa ya jinai itamatike?
Katika hukumu mahakama zote iliamriwa nilipwe gharama, lakini sikuweza kudai gharama Kwa muda huo kwani mdai alikuwa anakata rufaa mahakama ya juu. NI miaka 4 sasa imepita toka hukumu ya madai ya mahakama kuu iliyonipa ushindi lakini nilishindwa kudai gharama wakati huo kwani alipoona ameshindwa, mdai aligeukia kunifungulia kesi ya jinai, nayo imekwisha Kwa hakimu kuniona sina hatia.
Pamoja na hapo hajaridhika wamekata rufaa mahakama ya juu na kesi bado inaendelea.
Je, naweza kuanza kudai gharama za kesi zile za madai Kwa sasa NI miaka 4 imepita au nimechelewa?? Au nisubiri adi hii rufaa ya jinai itamatike?