Stavros Myles
JF-Expert Member
- Jun 7, 2020
- 350
- 390
Hi kwa wanateknolojia wa Jf.Niende moja kwa moja kwenge tatizo lililonikumba. Betri (CMOS Battery) ndogo ya CPU ya Hp iliisha nikafanya mkakati wa kuisaka lakini nikiwa kwenye mchakato nikasema ngoja niiwasbe hii Deaktop hivhivi bila yakuwa na betri.
Nilifanikiwa kuitumia Desktop kwa siku mbili. Siku ya tatu wakati naiwasha niliskia sauti ya kitu kilichoungua (Paaaaa ) ikiambatana na harufu ya kitu kilichokuwa kinaungua, niliwahi kuzima kwenye Socket ya ukutani.
Siku iliyofuata nilijaribu kuiwasha tena, hapa niliambulia sauti ya mfululizo iliyokuwa inaruka sekunde moja then inapiga tena (tena ilikuwa inaambatana na rangi nyekundu kutoka kwenye LED). Sauti hii (Beeping sound) ilikuwa inatoka mara nne mfululizo then inaanza tena.
Nili google na kuingia kwenye support site ya hp, baada ya kuingia huko nilipata ufumbuzi wa muda mchache, mara ya kwanza nilijua shida uwenda ilikuwa ni RAM, baada ya kuitoa RAM na kusafisha slots za RAM na kuirudishia RAM mahali ilipokuwa tatizo liliendelea. Nilijaribu kuangalia processor kama ilikuwa imecheza lakini bado haikuwa hivyo. Nikaona bora nisafishe air vents za CPU, hata baada ya kutumia kitambaa kisafi kutoa/kufuta vumbi still tatizo lilibaki palepale.
Kitu pekee nilichokuja kukimalizia kuangalia ilikuwa ni sehemu ya power source, hii baada ya kuifungua sikufanikiwa kugundua shida yoyote kwani kila waya ulikuwa uko tightly held kwenda kwenye mahali ambapo ilitakiwa kuwepo nilifunga lakini tatizo bado liliendelea kuwepo.
Nilijaribu hata ku 'unplug' power source then nilibonyeza sehemu ya kuwashia CPU kwa sekunde 15 lakini mambo yalikuwa yale yale.
Leo nimejaribu kuiwasha tena mambo yamejirudia yale yale, ila kama bahati nimefanikiwa kuipata harufu yakitu ambacho kilikuwa kama kinaungua sehemu ya Power Supply. Sina assurance kwamba Power Supply inaweza kuwa imeungua kabisa au shida ni betri. Kama unaweza kunipa hints za signs za kuungua kwa Power Supply nitashukuru sana .
Nawasilisha.
Nilifanikiwa kuitumia Desktop kwa siku mbili. Siku ya tatu wakati naiwasha niliskia sauti ya kitu kilichoungua (Paaaaa ) ikiambatana na harufu ya kitu kilichokuwa kinaungua, niliwahi kuzima kwenye Socket ya ukutani.
Siku iliyofuata nilijaribu kuiwasha tena, hapa niliambulia sauti ya mfululizo iliyokuwa inaruka sekunde moja then inapiga tena (tena ilikuwa inaambatana na rangi nyekundu kutoka kwenye LED). Sauti hii (Beeping sound) ilikuwa inatoka mara nne mfululizo then inaanza tena.
Nili google na kuingia kwenye support site ya hp, baada ya kuingia huko nilipata ufumbuzi wa muda mchache, mara ya kwanza nilijua shida uwenda ilikuwa ni RAM, baada ya kuitoa RAM na kusafisha slots za RAM na kuirudishia RAM mahali ilipokuwa tatizo liliendelea. Nilijaribu kuangalia processor kama ilikuwa imecheza lakini bado haikuwa hivyo. Nikaona bora nisafishe air vents za CPU, hata baada ya kutumia kitambaa kisafi kutoa/kufuta vumbi still tatizo lilibaki palepale.
Kitu pekee nilichokuja kukimalizia kuangalia ilikuwa ni sehemu ya power source, hii baada ya kuifungua sikufanikiwa kugundua shida yoyote kwani kila waya ulikuwa uko tightly held kwenda kwenye mahali ambapo ilitakiwa kuwepo nilifunga lakini tatizo bado liliendelea kuwepo.
Nilijaribu hata ku 'unplug' power source then nilibonyeza sehemu ya kuwashia CPU kwa sekunde 15 lakini mambo yalikuwa yale yale.
Leo nimejaribu kuiwasha tena mambo yamejirudia yale yale, ila kama bahati nimefanikiwa kuipata harufu yakitu ambacho kilikuwa kama kinaungua sehemu ya Power Supply. Sina assurance kwamba Power Supply inaweza kuwa imeungua kabisa au shida ni betri. Kama unaweza kunipa hints za signs za kuungua kwa Power Supply nitashukuru sana .
Nawasilisha.