a4afrika
JF-Expert Member
- Apr 13, 2012
- 1,762
- 1,785
Tofauti yangu nami ni kuwa Mimi huwa nashindwa kuongea kwenye matukio rasmi, ila kwenye vikao vya chini ya miti mtaani vya kupandishiana hoja bila kuzingatia protocol yoyote wala formality, hapo watasubiri.Natumai mmekuwa na wakati mzuri sana wa mapumziko ya leo. Mimi ni kijana mwenye umri wa miaka 33 ni mfanyakazi kwenye halmashauri X. Nimekuwa na changamoto zifuatazo
1. Nakosa amani watu wanapoweka attention kwangu
2. Nashindwa kuchangia mada ama hoja mezani
3. Nashindwa kukaa na watu kwa muda mrefu mara nyingi natamani niwe peke yangu tu
4. Nashindwa kufanya maamuzi sahihi hata kwa jambo dogo
5. Nashindwa kunusa hatari iliyopo mbele yangu
6. Nashindwa kuanzisha mada
7. Nimepoteza morali ya ujuzi niliosomea na nimekuwa mweupe kichwani
8. Sikubaliki kwa ninayoyafanya
NB: Unaruhusiwa kutumia hata chatgpt
BInafsi nimekubali Kuishi nilivyo, na humchukia anayefikiria naweza Kuishi tofauti na hivi. Nafurahia nilivyo.