Msaada tunaomba Mhe. Paul Makonda atusaidie, Kampuni ya Jog imechukua fedha za wawekezaji

Nilikwenda ofisini kwao wakaniambia wanaandaa semina nilipie 6000 nikapiga hesabu mara 500 nikakuta wanaingiza 3000000 nikajua hawa ni matapeli
 
Mwaka jana wakati tumekuja tz, tulienda ziara mkoa fulani nilikuja na Waarabu kutoka UAE. Huo mkoa tuliofikia kwa mdogo wetu ambae ni mkulima, tukakutana na Company kama hiyo ambayo kama sikosei Inaitwa Macleans Benecibo. Hivi kuna mtu yeyote anaweza kunihabarisha kuhusu ile company??
 
Tumejaribu kufanya hivyo Pwani (Mkuranga) wakatuambia tuje Dar manake Kampuni ipo huku na wakurugenzi wanaishi huku. Dar nako wanasema ni kama hawaoni jinai.

Thanks
Hawaoni jinai?? Ni chombo kipi kinatafsiri sheria????
 
Ukiitwa firsan ujue wewe ndio fursa MTU kirahis tu unatoa m9 kwa kauli za motivational speaker

Ungefuatilia kwanza kujua hyo kampun imewah Fanya mrad gan mkubwa au was kat na ikafanikiwa


Ndio yaleyale watu wamefugishwa sungura na mwishowe wakaachwa

Mwingne humu alifugishwa majoka huko bagamoyo sasa yanataka kumla yeye


WATANZANIA TUWE TUNAFUATILIA MAMBO KUZIJUA KAMPUNI ZA HOVYO KAMA HAO JOG
Mkuu umemaliza haha haa....
 
Nashukuru kwa ujumbe.

Lakini pia ninapoleta hapa jamvini kumbuka hata kama mimi sitapata haki yangu au kusikilizwa nitakuwa nimewasaidia hata wengine ambao pengine kampuni hii imeanza kuwatapeli.

Kumbuka Mkurugenzi mmojawapo Jackson Bwire alienda Clouds kutangaza kampuni wakati tayari sisi tumeanza kuibiwa. Hii itasaidia hata watu wa vyombo vya habari kuingia ndani zaidi kuwafuatilia watu wanaotumia vyombo vyao kutangaza kitu ambacho kumbe ni utapeli.


Lakini Pia sisi yametukuta wakati wenzetu wa Papai Phase1 na wengine wa Green Beans wameshalizwa na Kampuni hii. Kama hawa wenzetu wangeshtuka mapema na kupiga kelele watu tusingeendelea kuibiwa.
Asante
Uko sahihi kabisa kaka/dada... Natumaini mamlaka husika watafatilia hili, usichoke kupaza sauti kwa manufaa ya wengine. Be blessed!!
 
Yale yale ya Mr Kuku... yaani wewe ulipe hela watu wakulimie mapapai na wakuuzie kisha wakupe faida

Mkuu watu wanachekesha sana, sijui ni uvivu eti walipe pesa wao wafuge au walime kwa niaba yao na kampuni ya kilimo iko posta kweli maajabu hayaishi duniani
 
Mtapigwa sana na upumbavu wenu. Huwa tunawaambia hamsikii.

Kuna wengine wanalipa milioni tatu na laki mbili kwenye mradi wa sungura. Narudia 3.2M na unapewa sungura 20 ukafuge.

Hivi kweli mtu mzima na akili yako unauziwa sungura mmoja laki na nusu, amekuwa mbuzi huyo?
 
Mtapigwa sana na upumbavu wenu. Huwa tunawaambia hamsikii.

Kuna wengine wanalipa milioni tatu na laki mbili kwenye mradi wa sungura. Narudia 3.2M na unapewa sungura 20 ukafuge.

Hivi kweli mtu mzima na akili yako unauziwa sungura mmoja laki na nusu, amekuwa mbuzi huyo?
Asante mkuu
 
Asante mkuu
Wengi watakuvunja moyo...... Kudhulumiwa, kupata hasara kupo kwenye biashara.. Kikubwa ni kuminimize your loss...... Kuangalia investment ambayo ipo not too risk to put your money........ Yupo mtu atakutukana ila kila weekend bar anatumia laki 1 piga mara miaka 30 ya ulevi wake........ Jifunze kulingana na makosa.
Soma, tafiti fursa yeyote ile kabla ya kuingia, usifanye biashara ambayo huna uhakika nayo 100%.
Wekeza kiasi ambacho hata kikipotea hutafirisika.
Duniani tunazidi Kujifunza........ Wapo waliowekeza kihalali na miradi yao zaidi ya milioni 100 na zote zikapotea wakaanze tena upya.
Nakutakia uvumilivu na subira kwenye kipindi hiki kigumu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wengi watakuvunja moyo...... Kudhulumiwa, kupata hasara kupo kwenye biashara.. Kikubwa ni kuminimize your loss...... Kuangalia investment ambayo ipo not too risk to put your money........ Yupo mtu atakutukana ila kila weekend bar anatumia laki 1 piga mara miaka 30 ya ulevi wake........ Jifunze kulingana na makosa.
Soma, tafiti fursa yeyote ile kabla ya kuingia, usifanye biashara ambayo huna uhakika nayo 100%.
Wekeza kiasi ambacho hata kikipotea hutafirisika.
Duniani tunazidi Kujifunza........ Wapo waliowekeza kihalali na miradi yao zaidi ya milioni 100 na zote zikapotea wakaanze tena upya.
Nakutakia uvumilivu na subira kwenye kipindi hiki kigumu

Sent using Jamii Forums mobile app


Nashukuru mkuu
 
Ndugu zangu,

Naamini hapa jamvini watu wa aina mbalimbali na nyeti wanasoma jumbe hizi.

Kampuni ya Jog Agri-Consult & Solutiions (T) Ltd chini ya wakurugenzi wake Grace Mzoo (Mkurugenzi Mtendaji) pamoja na Jackson Bwire pamoja na Mhasibu wao Cecilia Bukukura imechukua pesa za wawekezaji wa Papai tangu mwaka 2017-2018.

Kampuni ilijinasibu sehemu mbalimbali ikiwa ni pamoja na kwenye makanisa, kwenye vyombo vya habari (Televisheni za Tz pamoja na Radio - mara ya mwisho Jackson Bwire alisikika Clouds akinadi kampuni). Jog chini ya Wakurugenzi wake imejinasibu kuwa inapokea pesa (Tzs million 9 kwa ekari moja) kutoka kwa mkulima/mwekezaji yoyote yule kwenye eneo la Papai halafu itafanya yafuatayo:

- Kukodisha ardhi
- Kuweka miundo mbinu yote (ikijumuisha drips pamoja na kuchimba visima vya kumwagilia papai)
- Kununua Pembejeo (mbolea za organic na dawa zote zinazohitajika
- Usimamizi wa kitaalam (ukijumuisha kupima udongo katika maabara Nairobi, kuweka vibarua nk)
- Kusaidia wawekezaji/wakulima kupata bima ya mazao
- Tayari wana mkataba na mnunuzi kutoka nchi za nje na kwa hiyo papai zikishakomaa watanunua kwa Tzs1000 kwa papai kutoka shambani na hivyo kumlipa kila mwekezaji
- Na mengineyo mengi

Watu na vikundi mbalimbali wakiwemo wajane, wastaafu, wajasiriamali, vikundi vya ujasiriamali/uwekezaji/fellowship walijiunga na kulipa fedha (Jumla ni Zaidi ya Tzs milioni 200) kwa kampuni ya Jog chini ya wakurugenzi waliotajwa hapo juu lakini hadi leo hii ninavyoandika ni zaidi ya miaka miwili (2) hakuna aliyelipwa na ukipiga simu zao hawapokei, ukienda ofisi zao pale Mwalimu House zimefungwa.

Juhudi za kufuatilia zimefanyika kama ifuatavyo;-
- Kuwapigia simu na kutuma sms (hakuna anayepokea simu wala kujibu ujumbe)
- kwenda ofisini kwao Mwalimu House - tukakuta ofisi imefungwa na wameweka namba za simu ambazo ndio hizo hawapokei
- Kwenda kwa Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga - Alikiri kupata malalamiko kutoka kwa watu wengine pia kuhusu Jog lakini akashauri tukaripoti DSM ambako Kampuni imesajiliwa
na Wakurugenzi wanaishi
- Kuripoti Polisi Mkoa wa Ilala/Kariakoo
- Kuutafuta uongozi wa Wilaya ya Ilala labda watatusaidia (hatujafanikiwa)

Tunaomba Uongozi wa Mkoa wa Dar es Salaam utusaidie kwani watu wengi walichukua mikopo Benki ili kuwekeza lakini wameshindwa

Asanteni
Daaah watu wanapigwa kizembe sana,mimi pesa zangu utazisubiria ahera
 
Wengi wetu tulikuwa tayari na mashamba na mitaji lakini hatukuwa na utaalamu pamoja na masoko. Tulipoenda kuomba huduma ya consultancy ndio tukapewa huo mradi tukaona labda utafaa na masharti yao lazima walime wao ili kudhibiti ubora.

Tulienda hadi shambani Mkuranga kijiji cha Kimazichana na tulikuta matrekta na excavators ziko site zinangóa visiki pamoja na vibarua wengi tu.

Mara ya mwisho kwenye kikao na Mkurugenzi Grace Mzoo tuliambia kuwa anasafiri ili kwenda kutafuta pesa ya kuturudishia lakini tulivyofuatilia huyu mama yupo Dar na anaonekana Kanisani Anglican Church Ukonga. Ndio tukaona hapa tunaibiwa. Tukipiga simu hazipokelewi, Ofisini wameweka namba za simu zilezile

Asante
Huyo mama ningemchukua na kumalizana nae kimenomeno bila police na pesa angerudisha na riba,mnapigwa na wajinga kwa kuchotwa akili ya faida kubwa
 
Asante sana.

Kumkamata mtu pia inahitaji msaada ukiona mpaka tumekuja hapa jamvini mambo yamesuasua mahali fulani ndugu yangu.

Nashukuru kwa ushauri wako
Huyo mama ningempa kesi ya mbaya mpka astuke marinda yote yameisha
 
Hivi Bashite mnamuamini vipi nyie. Bashite hana uwezo wa kutafuta suluhu yenu. Nendeni mahakamani.
 
Tulienda mpaka shambani ndugu yangu. Shamba tulionyeshwa na matrekta yalikuwa kazini pamoja na vibarua, na viongozi wa kijiji pale Kimazichana walikuwepo kutuonyesha kuwa mwekezaji wanamfahamu. Tulipenda tulime kwenye mashamba yetu lakini Swala linakuja kwamba wenyewe walisema hawaruhusu ulime shambani kwako kwa ajili ya kudhibiti ubora.

Lakini nashukuru pia kwa jibu lako
Wajinga ndio waliwao
Milioni 9 yako umeshinda kuingiza shambani kwako?
 
Back
Top Bottom