Msaada tafadhali, naachikaje?


Natamani kujua ni visa gani hivyo umevichoka kiasi hiki mpaka unaomba kuachika,kweli pesa si kila kitu😢😢
 

Hahahaha....hard to hold it,
 
Natamani kujua ni visa gani hivyo umevichoka kiasi hiki mpaka unaomba kuachika,kweli pesa si kila kitu😢😢

Hakuna kisa chochote,wanawake wengi wa sikuhiz sio wavumilivu tu,mimi kaka yangu alikuwa chapombe haswaaa kwa miaka kadhaa leo hii kaacha pombe na ana maendeleo haswa na Anampenda mke wake sanaa na kumsifia mara kwa mara kwani ndio kamfanya mpk akaacha pombe na bad companies.
 
Nilitaka kumwambia hivo na amesema hataki vikao wala nn najaribu kujiuliza hivi alitaftiwa huyu mme au la na jee hakumuona before kwamba n mlevi au vipi

Huyu ni kichwa maji mwacheni tu,kwani nani anapenda kuitwa mlevi? Huyo mwanaume naye angehesabu madhaifu ya huyu mwanamke je?
 
Mbona umesahau nyepesi ambayo inawezekanika, usimpe unyumba ama kama hakupi unyumba kwa zaidi ya miezi kadhaa waweza tumia hilo kuomba talaka maana umechoka kuishi kama kaka na dada, ama mnyime akuchoke akuache.

du!...kumbe hujielewi!..huyo Mungu uliemuomba awaepushe na "hili balaa" ameruhusu kuachana kwa aina ya 'makosa' ya huyo mumewe?
....aisee heri kuwa na akili kama za huyo mume kuliko kuwa na mwanamke mwenye akili matope kama wewe!
 
Jamaa anapesa asipopewa game anaenda kutafuta MAPAKA nje anajilia kiroho safi mkuu, agomee vingine lkn sio game
kiongozi game ya home inautamu wake, akiamua jamaa hata na pesa zake atatulia....
 

Ila kama anaumizwa na vitendo vya mmewe avumilie nini sasa?
Kati ya mapungufu niliyonayo ni uvumilivu kwa mambo yanayowezekana kubadilika kwaio sitoshangaa kwanini huyu Dada akipata mawazo ya kutaka kuachika
 
Nadhani umechukua uamuzi wa ghafla na hasira hujamchoka kwani ungemchoka yangekuwa mengine. Mbili, hakuna mwanaume anamwacha mwanamke bila visa ukiendelea kukaa kimya wala hata tambua kosa lake kamwe na ataendelea kupiga maji. 3 inaashiria uliingia kwenye mkenge kisa pesa na ni pesa hizo hizo zinakutesa sasa. Wazo: Kabla hamjaingia kwene ndoa mlikuwa na watu wa karibu ndugu jamaa na marafiki washirikishe. Likishindikana hili inakubidi uondoke nyumbani na kumpa nafasi ya kuona makosa yake kama kweli anakupenda atajutia na kujirekebisha. Ikishindikana haya yote basi kama alivyokushauri memba hapo juu unakwenda mahakamani na kufungua kesi kama kweli kuna haya yote utapata haki zako za kimsingi zote lakini kumbuka mahakamani watakushawishi na kukushauri mlimalize kifamilia kabla ya kupanda kizimbani kwani kuna adhari kwa wanafamilia wote hasa kisaikolojia na kijamii na hata kikazi. Ni hayo tu
 
Mkunde Original, uliapa kwa kinywa chako kuwa kifo ndio kiwatenganishe.., vinginevyo hakuna kuachika endeleza maisha kwa shida ama raha!

Vinginevyo sepa zako ukaanze maisha yako maana inaoneka hiyo ndoa ni zigo la misumari kwa upande wako.., japo huenda mumeo yeye ana amani ya kumtosha! Ila uwe unakumbuka kuwa hujaachika bado!!
 
Last edited by a moderator:
Yaani akaanzishe maisha yake mwenyewe halafu tena atambue kuwa haja achwa !!? Imekaaje hii mpendwa
 
Last edited by a moderator:
Tulia na ndoa yako wala usijali, pesa za deal zinaelekea kwisha hivyo lazima pombe na mengine yatakuwa na kipimo. Tulia tulia utaona maajabu Soon.
 

Hongera sana mkuu kwa nasaha nzuri
 

Ubaya wa mwenye nyumba....sio uzuri wa mpangaji
 
Unataka ujitawale!!!???
Mungu alimwambia Hawa.. "kwa tamaa zako siku zote utakuwa chini ya mme wako" wewe unataka kwenda wapi?
 
Unataka ujitawale!!!???
Mungu alimwambia Hawa.. "kwa tamaa zako siku zote utakuwa chini ya mme wako" wewe unataka kwenda wapi?

Kama mateso yamezidi afanyaje jamani.Mi nnachomshauri asiwaze sana kuachika ajaribu kumshirikiasha na Mungu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…