Msaada: Nimetengwa kijamii

Msaada: Nimetengwa kijamii

God'sBeliever

JF-Expert Member
Joined
Sep 1, 2015
Posts
5,788
Reaction score
3,062
Habari za wasaa huu wandugu,

Nahisi siko vizuri kisaikolojia naombeni msaada nilitengwa kijamii. Sipati ushirikiano kutoka kwa ndugu, marafiki zangu na jamii yangu kwa ujumla.

Hali hii imenifanya niogope kujichanganya kwa kuhofia kukosa ushirikiano.

Hakuna mawasiliano kati yangu mimi na ndugu zangu nikipiga hawapokei wala hawajibu SMS.I am tortured i need help.

Nimeshindwa hata kusoma na kupata mafanikio sababu muda wote nipo mwenyewe tuu nyumbani. Nawaza hivi nikiumwa ghafla hapa nani atanisaidia?

Nilimgundua mbaya wangu alie block mawasiliano kati yangu mimi na ndugu zangu hawa nikaachana nae sina ubavu wa kumwadhibu.

Mimi kimsingi ni chadema na wengi walitamani niwe CCM ila sitaki hivyo basi sina mda na siasa za Tanzania ili kuepusha chuki na watu nitakapokua upande wangu. Kwa msimamo wangu huo mengi yametokea na moja wapo ni hili la kutengwa, habari zangu za siri kuwa public na kadhia nyingi sana.
Nadhani misimamo yangu hii ndio chanzo cha yote haya...

Note: Mimi sina baya lolote nililofanya so msinihisi vibaya bali ni hivo.

Naombeni ushauri wenu ili niweze kuepukana na hii hali.
 
Pole sana mkuu, Nini Kilisababisha utengwe na ndugu na jamaa? Funguka upate msaada wa mawazo
Mkuu mimi nilikua vizuri na jamaa zangu wala sina tatizo ila ni mambo makubwa siwezi kuyaweka hapa.
Kwa nilivyojieleza hapo waungwana natumai mtanielewa.
Siwezi kutajia mhusika kabisa.
 
We ndo unajitenga unaitaji msaada bado unamute information ,maisha ni kuchagua na utavuna ulichopanda
 
Mkuu kuna jambo nahis ni vigum kutengwa na ndugu, jamaa na marafiki nahic wewe utakuwa na matatizo kama umewakosea waombe msamaha ,Neno samahani ni dogo sana lakini lina nguvu sana siyo kawaida. Jitahd ujue chanzo na si vinginevyo kukusaidia lazima ujue ASILI ya TATIZO
 
Kwa namna moja au nyingine wewe ndio utakua una matatizo, haiwezekani ndugu zako wote wakutenge!!!

Labda ueleze nini kilichotokea kati yako ya hao ndugu zako!!
 
Mkuu mimi nilikua vizuri na jamaa zangu wala sina tatizo ila ni mambo makubwa siwezi kuyaweka hapa.
Kwa nilivyojieleza hapo waungwana natumai mtanielewa.
Siwezi kutajia mhusika kabisa.
Huwezi kufanyiwa matibabu sahihi kama unaogopa kutaja kiini cha ugonjwa.... Funguka usaidike...
Vinginevyo utakufa kisabuni, binafsi sijakuelewaa....
 
Back
Top Bottom