Umenikumbusha stori ya Mzee Jackson Makweta alichofanywa na hao jamaa kwa kuwa alikuwa na nyota ya kuwa Mukulu...
Mzee mpaka dakika ya mwisho alikufa analia Tanzania yangu, Tanzania yangu.
Yeye aliipenda Tanzania ila "wazee wa kamati ya ufundi" wa nchi walimpenda zaidi.
Nimewahi kukutana na jamaa wa kaliba yako Musoma huko, yeye naye "wazee wa kamati ya ufundi" walimfanyia kitu mbaya.
Wakamchomoa ndani wakampeleka ofisi kubwa akawa mtumishi wa bila malipo, mule ndani wakamuweka mzungu akaendelea kula msuli UDSM.
Dogo ana masters kali kwa sasa, ukimuona utadhani aliishia darasa la nne.
Alinisimulia vitu vingi sana.
Ila kizito ni kuwa "wazee" walikuwa wanaitumia nyota yake kwenye mambo ya "Public Administration" pale jumba jeupe.
Walipoona nyota imewanogea wakaamua kumnyofoamo mazima.
Hapa JF ni vigumu kupata msaada kwa kuwa wengi mambo ya kiroho yamewapita kando sana.
Ila vita uliyo nayo ni kubwa aisee.
Jitadi kusali sana, mana inaonekana wameshindwa kukuondoa ili wajimilikishe nyota yako sasa wanataka uwauzie ulicho nacho lakini umekuwa mgumu kufikia bei.
Siku utakapo kula tu kiapo cha kuingia chama jekundu, ndio utakuwa umejirestisha in pisi mazima.
Ni hayo tu mkuu.