Msaada: Ni ipi aina bora ya sola paneli?

Msaada: Ni ipi aina bora ya sola paneli?

Tafuta brand ya SUNPOWER, zinatoka US, zipo pia zilizotengenezwa Germany.

Ukipata monocrystalline ni nzuri zaidi ya polycrystalline, japo kwa technologia ilipofikia tofauti hiyo ni ndogo sana. Kwa hiyo bajeti ikibana chukua poly.
Kwa hapa MBEYA niende wapi kuwaona hao watu?
 
Matumizi ya mono, poly, ama amorphous solar panel yanategemea hali ya hewa ya sehemu alipo mtumiaji. Pia zipo zaidi ya aina tatu za solar panels ingawa nyingi bado zipo kwenye maabara kwa ajili ya utafiti.

Mono ni nzuri sana na ufanya kazi kwa ufanisi katika maeneo ambayo upata mwanga wa moja kwa moja kutoka juani bila kupitia kwenye mawingu (direct/beam solar radiation). Poly na Amorphous ni nzuri kwenye maeneo ambapo mwanga wa jua ni hafifu kutokana na ukungu ama mawingu (diffuse solar radiation).

Kwa hiyo, kumshauri mtumiaji wa Kibosho atumie Mono nikutaka kumfanya 'kuzika' hela zake za manunuzi ya panel. Wa Kibosho atumie amorphous ama poly panels. Hata hivyo mbali na bei kuwa haijachangamka kwa panels hizi zina changamoto zake zinazohimilika.
Kwa sisi wa MBEYA tutumie IPI?
 
kuna solar panel aina mbili, mono na poly, chukua Mono, utanishukuru baadae japo bei imechangamka, zigoogle kujua tofauti zake kimuonekano

kwa controller tafuta MPPT controller achana na PWM, mppt bei imechangamka ila hutajutia

Hivi mkuu solar za thin- film zinapatikana pia
 
Unazungumzia aina au brand? Maana ni vitu viwili tofauti.

Kama ni brand, basi chukua kampuni ya Suntench au Jinko. Ingawa jinko panel za watts ndogo hawana, nafikiri wanaanzia watts 200 na kuendelea na output volts ni 24+. Ukishindwa hizi nenda kwenye maduka ya steps solar, watakupa panel na controller zenye ubora kiasi.
"ubora kiasi". Duh!!!
 
Kuna Brand na Type, Drone drake amelezea swala la Type ila hivo vifaa vyako vyako kama Ni AC basi inverter haikwepeki na Victons ndo best sokoni
 
watafute eggy energy watakufanyia kila kitu na utalipia kidogo kidogo

nimefunga hapa nina miaka 14 kitu imetulia panel toka ujerumani na wakati wakifunga wanapima uelekeo gani panel ikae na inaungwa na simu yako

namba yao

0655220242
Hiyo namba haipatikani labda huenda mawasiliano si mazuri
 
Kwa sisi wa MBEYA tutumie IPI?
Kama muda mwingi huko Mbeya kuna ukungu na vipidi virefu vya mawingu mawingu na mvua tumia Poly ama Amorphous. Utazijua panel hizi kwa rangi. Amorphos ni nyeusi kama ubao wa darasani ikiwa na michilizi ya viwaya vyembamba. Poly ziina rangi mchanganyiko kama blue nyeusi na blue.
 
Kama muda mwingi huko Mbeya kuna ukungu na vipidi virefu vya mawingu mawingu na mvua tumia Poly ama Amorphous. Utazijua panel hizi kwa rangi. Amorphos ni nyeusi kama ubao wa darasani ikiwa na michilizi ya viwaya vyembamba. Poly ziina rangi mchanganyiko kama blue nyeusi na blue. Na idadi ya cells.
Nitaufanyia kazi ushauri huu
 
Nitaufanyia kazi ushauri huu
Ukifanikiwa kupata panel hizo hakikisha unapata fundi atakayekufungia panels hizo kwa kufuata uelekeo sahihi wa jua. Na iwekee stand yenye viwango vya kuwezesha panel kufanya kazi kama ilivyo designiwa. Mambo haya mawili ni muhimu kwani yakikosewa hushusha utendaji mzuri wa panels. Huko Mbeya nina imani kuna mafundi wanaoaminika na TAREA inawatambua.
 
Kwa anayehitaji Betri za uhakika zlizotumika kwenye minara ya simu anicheck Hz ni Betri imara mara Mia kuliko mpya ya Sundar au sjui Rita NK ninazo za 150ah umeme WA uhakika sana.
0629945110
 
kuna solar panel aina mbili, mono na poly, chukua Mono, utanishukuru baadae japo bei imechangamka, zigoogle kujua tofauti zake kimuonekano

kwa controller tafuta MPPT controller achana na PWM, mppt bei imechangamka ila hutajutia
Asipofuata huu ushauri basi tena hana shida huyo
 
Hapo naomba ufafanuzi,nimeshindwa kukuelewa!Unamaanisha nini kwa kusema vifaa hivyo ni DC?Mimi ni mshamba kabisa kwenye eneo hilo
DC ni umeme sawa na wa betri.
Umeme uko aina mbili AC usiochujwa utokao Tanesco bila kuchujwa kwa kutumia diodi na kapasita huu hupanda na kushuka.
DC ni ule uliochujwa kwa kutumia diodi na kapasita, mtiririko wake ni ulionyooka.
AC husafiri kwa karenti (nguvu itumikayo kwenye chombo) ndogo.
DC inakarenti kubwa, yaani betri ya gari voti 12 kuliko AC voti 12.
Hivyo sola inatumia voti ya DC.
 
Mkuu unaweza jaribu hizi solar za makampuni ninatumia zola mpaka nimepata umeme wako poa sana hasa ktk hii mitambo yao mipya.
 
Umeonaee!Jamani fafanueni kwa ile lugha ya wote!Nimeenda kwenye maduka ya pale Mwanjelwa,nimekuta wanauza Sundar solar ,sasa nimeshindwa kuelewa maana wafanyabiashara wanasifia kile wanachouza
Kiukweli Battery la pro solar lipo poa sana sema solar zao ndio ghali, chukua Battery N100 na solar sundar watt 150 uta enjoy maisha.
 
Back
Top Bottom