Nakushari kwanza Badilisha Avatar,unaitwa NJAA?
Kuna majina mengine mungu hupenda kuyapa yanachokiamini.
Sasa kama upepo utapitia kwako,basi umaskini hadi unaingia kaburini.
Ni mtizamo wangu tu huo,ndio maana maandiko yanasema,wapeni watoto wenu majina mazuri.
Humu kuna ujumbe wa mungu ndani yake.
Tukija kwenye issue ya kuezeka.
Kwanza nakupongeza kwa kuzichanga,maana nikiiangalia nyumba itakuwa ilisimama si chini ya miaka miwili.
Nimependa sana ulivyokuwa makini katika ujenzi wa madirisha makubwa,nime Appreciate sana hilo.
Halafu kuwa makini sana na hao wanajeshi,naungana na jamaa hapo juu,wengi siku hizi nao wasanii maana wanajua watu wanawakimbilia wao,labda ukifanikiwa kupata jeshi wa kike.Ungekuwa huku Znz ningekuunganishia mdada mmoja.
Pili,kuna watu humu wameanza Pms nyingi,pia kuwa makini,Maana wewe umeomba tu ushauri na sio mambo ya Pm,huko watakuletea usanii pia,maana humu namo matapeli wamo kibaoo.
Ushauri wa Kingkong:-
Mnazi watu wanaudharau sana,lakini ni mbao zinadumu kwa muda mrefu sana.
Kwa watu wa mikoa ya pwani ikiwemo Zanzibar wanaijua Minazi ilivyo.Thamani nyingi sana za majumba zimetengenezwa kwa minazi.Na hata mahoteli ya Coast hapa ukitembelea bado mnazi umesanifiwa kwa hali ya juu sana huwezi kuamini kama ni mnazi.
Fanya uwezavyo ili uweke gharama chini,then ukitaka anasa utafanya wakati mwingine.Jiji hilo kupanga ni kama jela.Ikikaribia muda wa kulipa kodi mtu unakonda.
Huku Zanzibar kuna watu wengi sana kwa kukataa adha hiyo wamejenga nyumba nusu,kisha mtu anahamia na anaimalizia yumohumohumo ndani,na mtu akikuambia alihamia ikiwa nusu huwezi kuamini kwa jinsi ilivyo bomba.
Mbao treated ni uzushi tu,mie hapa ninapoishi fundi alisema ni treated,ila yale madudu baada ya miezi sita tu yalianza kula mbao kama wazim,kuna jamaa ndio akanipa dawa ya kupata,ila ni msiri wala hakuniambia ni nini,mie alinipa tu,maana ni mtu wa mitishamba,ila ilikuwa kama mti fulani aliusaga na kuuloweka kama wiki kisha akaniambia paka,basi hata sisimizi hasogelei.
Mie pia ni miongoni mwa wanaoamini kwamba zinatosha,cha msingi tumia basic roof set up itakusaidia,ila kama unataka anasa kwa kuweka paa na bati za kisasa hiyo utaishia njiani.Fuata ushauri wa fundi na sio wewe kufanya kujua kuliko yeye.
Ushauri kwa wana Jf:Kila mwenye familia ajaribu kujitolea kumsomesha ndugu yake yoyote VETA au sehem yoyote ya ufundi wa aina yoyote.Au hata kumsomesha Kijana unaemuona mtaani anakipaji cha ufundi hata kama sio ndugu yako nahana uwezo..
Mie wakati na jenga chanika sikupata shida,maana Fundi wa Nyumba ni Mjomba wangu,so hapa nilisave sana,na kuezeka ni mwanae,hapa pia nilisave sana gharama.Umeme alinifanyia Collegemate mwenzangu.
Yaani kuna vitu vingi sana Familia lazima iwe navyo katika miomboni kwa members.
Mfano wa Pili ni Upande wa Biashara yangu ya Carry,nikwamba Drivers wawili ni ndugu zangu yaani upande Mama yangu Mdogo,na pia kwanza walianzia kupitia Gerage miaka kibao,kwahiyo hapo sina gharama ya Fundi na gari zinatuzwa vizuri sana.Na ndio maana inanipa hamasa pia nihamishe mmoja kwenye Daladala nikiipata.
Wife pia taalum yake ni kushona,na pia nilimpeleka kozi za kutengeneza Udi,Sabuni,Ice Cream,mwezi ujao nampeleka Sido kujifundisha Kusingika asali ambapo ndio up comming project yetu.
Mtu kujifunza sio lazima ufanye kazi hiyo,ila ujuzi kuwa nao ni muhim sana.Maana huwezi amini mie Wife ni Standard Seven tu lakini she kwows much kuliko mie.Na baadhi ya vitu inabidi nipigwe shule.Please wenzangu naomba tusidharau hivi vikozi vidogo na kuona kama ni vya watu wa elim za chini,nyingi ni muhim sana na huko ipo njia ya mafanikio katika famila zetu.
Ni mtizamo wangu tu,kuna vitu vingi tunaingia gharama kubwa sana bila sababu ya msingi.