Msaada: Nataka kuezeka nyumba hii

Msaada: Nataka kuezeka nyumba hii

Njaa

JF-Expert Member
Joined
Dec 6, 2009
Posts
1,022
Reaction score
412
Wanajamvi....

Nimefanikiwa kufika hapa kwenye mambo ya ujenzi pembezoni mwa jiji...., baada ya kusimama kwa muda sasa nimepata 4.2 milion kwa ajili ya kuezeka. Napenda sana zile bati za rangi zenye migongo midogo ingawa salio ndo hilo bovu. Naomba ushauri kwa haya yafuatayo:-
  • Je hizo hela zinatosha? please nipeni mchanganua kwa uzoefu wenu hasa idadi ya bati, mbao, misumari, ufundi na gharama zake...,
  • Ushauri wa bati nzuri na geji zake ila kwa kuzingatia hilo salio, sina zaidi.....
  • Kwa mwenye kunisaidia ku-design paa naomba anisaidie, nitamtoa kidogo (pm please)
  • Chochote unachoweza kunishauri nitashukuru
  • Kuna mtu ananishauri ninunue bati za jeshi, hii imekaaje wakuu
Nawakilisha



20131209_102854.jpg 20131209_101028.jpg 20131209_101020.jpg 20131209_101020.jpg
 
Sijuhi unaweka mbao za aina gani, namaanisha za kenchi, kama ni zile treated, hiyo pesa ni ndogo
 
Si kuna mdau alisema usinunue mbao treated nunua kawaida then nunua oil nadhain vijana wapake maana treated nyingi ni fake.Alafu uende na futi yako huko kununua mbao.Kuhusu mabati ya jeshini ni ya kawaida tu ya msouth ila ukipata kwa jeshi bei inakuwa pungufu sana.tafuta mjeda unayemjua akusaidie.hongera.
 
ni ngumu kupata mawazo ya moja kwa moja ya gharama mkuu!
ili kupiga gharama lazima mpigaji awe na uzoef wa aina ya bati unalotaka + aina ya mbao utayotaka kutumia, bila kusahau ukubwa wa nyumba. i think jarib kutafuta fundi mwaminifu wa paa mkapige gharama
 
Sijuhi unaweka mbao za aina gani, namaanisha za kenchi, kama ni zile treated, hiyo pesa ni ndogo

Nataka kuweka kenchi mkuu kwa mbao zile treated....
 
Si kuna mdau alisema usinunue mbao treated nunua kawaida then nunua oil nadhain vijana wapake maana treated nyingi ni fake.Alafu uende na futi yako huko kununua mbao.Kuhusu mabati ya jeshini ni ya kawaida tu ya msouth ila ukipata kwa jeshi bei inakuwa pungufu sana.tafuta mjeda unayemjua akusaidie.hongera.

Ndo nafuatilia mjeda fulani anisaidie, nae atataka cha juu kama kawa
 
ni ngumu kupata mawazo ya moja kwa moja ya gharama mkuu!
ili kupiga gharama lazima mpigaji awe na uzoef wa aina ya bati unalotaka + aina ya mbao utayotaka kutumia, bila kusahau ukubwa wa nyumba. i think jarib kutafuta fundi mwaminifu wa paa mkapige gharama

Wazoefu wanaweza kutoa mawazo fulani yakasaidia mkuu, ukubwa wa nyumba si huo kwenye picha? Japo kwa kupata general idea....
 
Mh. hiyo pesa kidogo poti. tuliza boli, tafuta nyingine kama hiyo ili ununuwe mbao, mabati, misumari, ulipe mafundi.
 
Mh. hiyo pesa kidogo poti. tuliza boli, tafuta nyingine kama hiyo ili ununuwe mbao, mabati, misumari, ulipe mafundi.

Au nitafute bati za bei poa?
 
Salio hilo mkuu halitoshi ongeza kidogo labda utumie bati za bei nafuu.
 
Achana na treated utaingia gharama zisizo za lazima, nunua za kawaida tu halafu zikiisha jengewa juu then nunua diesel zipake, utakuwa umeokoa gharama kubwa sana na pia ni uhakika, hakuna mdudu atasogea.

Bati nunua za kawaida gauge 28 nadhan zinauzwa kati ya 15,000 na 20,000.

Usi complicate chochote maana unaweza kushindwa kumaliza, na pia ezeka muezeko ambao hautatumia material nyingi, mafundi wanajua.

Kaa na fundi mjadiri gharama na material zote kabla ya kuanza ili usiishie njiani.

Hongera sana kwa hiyo hatua na nakutakia kila la heri.
 
Ndo nafuatilia mjeda fulani anisaidie, nae atataka cha juu kama kawa

Kaa chonjo sana na hao wajeda.. hakaikisha ni mtu wa karibu na unayemwamini kuna jamaa yangu alipigwa na hao wajeda, aliwapa hela wakamnunulie sementi wakaila na ukiwadai wanakupa vitisho.. so be careful sio kila mjeda unaweza kumtumia
 
0757435193.....Call me ntakwambia cha kufanya...
 
Piga simu hii number 0717726524. Ni fundi wangu mzuri sana atakusaidia.
 
Nataka kuweka kenchi mkuu kwa mbao zile treated....

Mbao nyingi zinazouzwa ambazo ni treated tayari huwa wanatumia dawa feki. Nakushauri fanya hivi
1. Kama inawezekana nakushauri nunua mbao zako zinazohitajika,
2. nunua dawa zifanyie treatment wewe mwenyewe (weka vijana wafanye kazi huku unasimamia hata nao wanaweza kukuibia dawa au hizi mbao).

Pia kuhusu makadirio ya bati na mbao tafuta fundi mzuri akupigie hayo mahesabu.
NB:
Hakikisha manunuzi ya kila kitu unayafanya mwenyewe usimpe hela mtu akusaidie.
USIMAMIZI WAKO UKIWA MZURI hela yaweza kutosha au kupelea kidogo tu ila kwa bati la kawaida (gauge 28)
 
Mbao nyingi zinazouzwa ambazo ni treated tayari huwa wanatumia dawa feki. Nakushauri fanya hivi
1. Kama inawezekana nakushauri nunua mbao zako zinazohitajika,
2. nunua dawa zifanyie treatment wewe mwenyewe (weka vijana wafanye kazi huku unasimamia hata nao wanaweza kukuibia dawa au hizi mbao).

Pia kuhusu makadirio ya bati na mbao tafuta fundi mzuri akupigie hayo mahesabu.
NB:
Hakikisha manunuzi ya kila kitu unayafanya mwenyewe usimpe hela mtu akusaidie.
USIMAMIZI WAKO UKIWA MZURI hela yaweza kutosha au kupelea kidogo tu ila kwa bati la kawaida (gauge 28)

kwa mwonekano wa nyumba kwa makadirio ina upana wa kama 30ft na urefu kama 50ft. Bati ya 28 gauge na mbao treated 4m inaisha, atafute pesa ya fundi.
 
Mkuu JF ni sehemu ya kupeana ujuzi na uzoefu hiyo pesa 4.2m ni nyingi sana na chenji inabaki,tafuta mbao za minazi na utafute mtu wa kukata mbao za mnazi kwa nyumba hiyo minazi 16 inatosha zunguka sehemu mbali mbali hapa dsm ukikuta wanaangusha mnazi waombe huo mnazi,kukata kwa mashine mnazi mmoja kuchonga mbao ni sh 4000 kwahiyo gharama za mbao za minazi 64,000/= Kuna wengine wanauza mnazi kwa 10,000 wengine hawauzi ukikuta wameukata wanatoa bure so tuassume total 220,000/=plus usafiri 80,000/= Nunua bati za ALAF zile ngumu za 20,000/= kwahiyo nyumba yako nlivyoangalia zinaingia kama 60 tuassume 80 kwa design yeyote(Total 1.6m) kuna mafundi wazuri sana wa bei rahisi design yeyote ya paa na ufundi kujenga wanafanya kwa 600k) mpaka sasa tushatumia 2.5m tuweke 100k ya usafiri 2.6m! Hapo utabidi uongeze matofali kama 100 kwa ajili ya kuzungusha juu,utahitaji waya kwa ajili ya kushikia fenzi tuassume makolokolo yote hayo laki4 pamoja na kununua ndoo za rangi kwa ajili ya kupaka hayo mabati yalete muonekano mzuri ila rangi ya bati uipake baada ya miezi kama miwili hivi baada ya kuzijengea then 1.2m inabaki kwa mambo mengine humu JF kuna wengine wanakatisha tamaa na bei za ajabu ajabu! Mbao ya mnazi ni miaka 100 hailiwi na mdudu yeyote! Na ndio maana kitanda cha mbao ya mnazi bei yake haishikiki 77 walikuwa wanauza 1.2m
 
Back
Top Bottom