Wakuu habari za Leo, naomba msaada kuna Rafiki yangu alikuwa na biashara ya kuuza Vinywaji vya Jumla lakini baadae akapatamatatizo (aliibiwa) Hivyo kw amuda mrefu hakuweza kufanya biashara tena.
Badae alirudi kwenye biashara lakini alibadilisha aina ya biashara na mtaji pia mdogo hivyo hajafikia viwango vile vya Kutumia mashine ya EFD maana sasa ana Duka Genge tu.
Muda mrefu hajatumia mashine yake, hivyo anauliza Je kuna utaratibu gani wa Kurudisha hiyo machine? Je akiednelea kubaki nayo hawezi kuja kuhesabiwa kwamba amekwepa Kodi?
utaratibu kwa Ujumla kisheria ukoje kuirudisha au kuomba Kuisitisha hadi biashara itakapokuwa tena.
Biashara ikifilisika unaenda TRA na mashine yao ikiwa ni pamoja na vielelezo ulivyofungulia biashara.
Wao watafanya tafiti zao ikiwa ni pamoja na kutuma mtu wao kujiridhirisha , baada ya hapo watasitisha Mashine yao
Biashara ikifilisika unaenda TRA na mashine yao ikiwa ni pamoja na vielelezo ulivyofungulia.
Wao watafanya tafiti zao ikiwa ni pamoja na kutuma mtu wao kujiridhirisha , baada ya hapo watasitisha Mashine yao