Jaji Mfawidhi
JF-Expert Member
- Feb 20, 2016
- 14,047
- 20,412
andamana kama wale vijana 800, yatafika.Habari za usiku wapendwa katika bwana.
Leo nimepatwa na ajali iliyosababishwa na dereva wa JW aliyekuwa akiendesha gari aina ya hiace ndogo ivi yenye namba 1834 maeneo ya Ofisi za jiji Mwanza.
Nikiwa natokea maeneo ya maji haouse nikiendesha ki TVS changu, nilipofika yalipomataa pale maeneo ya jiji ghafla gari hiyo ili ni overtake upande wangu wa kulia kisha ikakata kona ya ghafla ili kuelekea maeneo ya seketure.
Gari iliniparamia ubavuni na kupelekea kuanguka pembeni, Nikiwa pale chini dereva wa gari husika aliliondoa kwa kasi kiasi cha kusababisha kuendelea kunisukuma zaidi.
Kwavile sikuwa na mwendo mkali sikuumia sana zaidi ya kupata maumivu mguu wa kulia na hii imesababishwa na vile alivyonipush akitokea upande wangu wa kulia, pia pikipiki imepata hitirafu kidogo.
Dereva wa gari husika hakutamka chochote pia hakushuka ndani ya gari, aliendelea na safari yake.
Naomba kufahamu ni vipi nitatoa malalamiko yangu kuhusu hili tukio ili ndugu zetu hawa wawe na nidhamu wanapokuwa barabarani, niende polisi au niende kambini kwao maeneo ya Airport.
Ang'ang'anie afu aambiwe amejaribu 'kuteka' gari la jw? Ungekuta yupo ndani saivi..
Aripoti polisi tu, huyo dereva atawasilishwa hapo fasta. Jw hawatetei uhalifu
Kesi ya nyani hii hakimu ngedere...usipoteze muda wako mkuu bureKama unaijua kambi yake nenda.
Wakikuzungusha MUACHIE MUNGU.
ungemrushia hata jiwe angesimama tu. Akileta za kuleta mnazichapa tu. ukiona anakuzid unamtia hata kitofa cha kichwa. Usawa huu hamna kumuogopa mtu mzee.
Kuna jamaa yangu wakati tuko chuo aliwahi kunichekesha sana. Wanajeshi wako safarini, wakakuta sehemu barabara ni mbovu haipitiki mvua ilikuwa imenyesha sana. Wakaamua kufanya opersheni pale pale, kulikuwa na mawe umbali kidogo ikabidi waanze kusomba mawe na kuyaweka barabarani kama hatua ya dharura. Wao wakaanza kufanya kazi hiyo halafu gari zingine zote zilizokuwa zinafika pale yakiwemo mabasi ya abiria, yaani ile basi linafika tu abiria wote mnashuka haraka sana na kunyoosha moja kwa moja kwenda kuchukua mawe. Wale kama akina makanyaga wanaopenda kuhoji hoji kila kitu na kujishauri shauri, walikuwa wanapata mkong'oto wa uhakika sana zikiwemo fimbo za mgongoni na baada ya hapo mtu anyoosha moja kwa moja kwenda kuchukua mawe bila kuongea au kuuliza maswali. Cheza na jeshi wewe!Daaah wajeda bwana kuna siku nilipita karibu na geti lao nikaona watu wanarushwa vichura chura. Walifanya? Hata kujua sikutaka nilipita kimya kimya kwa mwendo wa haraka maana wasinge kawia kugeuka na kuniita na mimi nikasomeshwe namba.
Afisa wa jeshi ni kuanzia mwenye nyota 1 kwenda juu,sio kila mwanajeshi ni Afisa.kwa kua kuingia kambini kwao ni ngumu maana watakuhoji na ukieleza shida zako wenzie wa getini watamlinda,nenda hapo pembeni ya mahakama pale bwalo la mgambo kuna viongozi wa kijeshi watakusaidia,ukienda traffic police wanaweza wakahisi usumbufu kumtafuta afisa wa Jeshi na wakakupotezea
Kuna gari ya binafsi yenye namba nne 1834? Natamani kujua elimu yako
Afisa wa jeshi ni kuanzia mwenye nyota 1 kwenda juu,sio kila mwanajeshi ni Afisa.
Kesi ya nyani hii hakimu ngedere...usipoteze muda wako mkuu bure
Wewe ni mwanajeshi wa miguu... Hahahaaaa...Mimi sio askari
Mimi ni raia tu mkuu
Pole mkuuHabari za mchana wapendwa katika bwana.
Nawashukuru nyote kwa msaada wa mawazo, yaliyopelekea kufanya maamuzi.
Lengo la kutaka kuripoti tatizo hili haikuwa kufidiwa pesa au kupata msaada, ila tu kuwakumbusha hawa ndugu zetu kuwa na uungwana wanapokuwa barabarani.
Ni jambo tu la kumshukuru Mungu niko hai na niko salama, vinginevyo saivi ningekuwa mlemavu au Mfu.
Nilimshirikisha mzee wangu na kuchanganya na mawazo yenu nikafikia uamuzi wa kuachana nalo ili jambo.
Mtu mmoja amenambia gari iyo japo haikuwa ambulance ila anahisi ilikuwa na mgonjwa aliyekuwa anawahishwa hospitali ya seketure.
Asanteni sana, na nimepata mwanga sasa namna nzuri ya kudeal na changamoto kama hizi.