BabaMorgan
JF-Expert Member
- Dec 18, 2017
- 4,059
- 10,514
Moja katika vitu ambavyo naomba visinikute na hata mtu nayemchukia sana visimkute basi ni hii moments ya kupata ajali na gari ya watu huku uwezo wa kulipa ukiwa wa tia maji.
Juzi nikiwa kwenye bus tulikutana na Harrier ya Transit imepata ajali Iyovi mbele pameharibika sana nikajaribu kujiweka kwenye position ya dereva yule kupitia fikra pekee nilifeel pain ambayo yule dereva anapitia.
Just imagine mtu ameagiza ndinga yake Japan kaisubiri kwa miezi mitatu mpaka sita hatimaye imefika bandarini kafanya clearance imetoka anapewa taarifa ipo njiani kwa shauku ya hali ya juu anaisubiria ghafla bin vuu anapata taarifa ndinga yake imepata ajali.. sio jambo jepesi kukubaliana na hii hali hususani kama mhusika ndio gari lake la kwanza.
Upande wa dereva lengo lilikuwa kupeleka gari ili apate kipato lakini kipato kinageuka na kuwa tatizo
Juzi nikiwa kwenye bus tulikutana na Harrier ya Transit imepata ajali Iyovi mbele pameharibika sana nikajaribu kujiweka kwenye position ya dereva yule kupitia fikra pekee nilifeel pain ambayo yule dereva anapitia.
Just imagine mtu ameagiza ndinga yake Japan kaisubiri kwa miezi mitatu mpaka sita hatimaye imefika bandarini kafanya clearance imetoka anapewa taarifa ipo njiani kwa shauku ya hali ya juu anaisubiria ghafla bin vuu anapata taarifa ndinga yake imepata ajali.. sio jambo jepesi kukubaliana na hii hali hususani kama mhusika ndio gari lake la kwanza.
Upande wa dereva lengo lilikuwa kupeleka gari ili apate kipato lakini kipato kinageuka na kuwa tatizo