Msaada: Nahitaji Bima ya Afya ya NHIF

Msaada: Nahitaji Bima ya Afya ya NHIF

Sikweli bima hizo inaazia 50400 kwawote sio watoto tu sasa utachagua mwenyewe uaze na kifurushi kipi na aina yatatizo ,ukiwa na mtoto mwenye shida yakutosha kiwango hicho hakikidhi ,labda kutibu kamasi na vipimo vya malaria ukishaingia kwenye kipimo kikubwa haisomi
50400/= ni kwa watoto na wanachuo tu.
 
Nahitaji Bima ya NHIF Mimi na watoto wangu wawili pamoja na Mama Mzazi.

Hiyo Bima iwe nation wide (nchi nzima)

Mimi sio mtumishi wa Umma Wala sekta binafsi nimejiajiri.

Wakuu Jambo la Pili nahiitaji ..Kupata mchanganuo wa gharama kwa mwaka Ahsante na Mchana mwema.

Muhaya original
Angalia hapa

Ova
20220601_160008.jpg
 
Nahitaji Bima ya NHIF Mimi na watoto wangu wawili pamoja na Mama Mzazi.

Hiyo Bima iwe nation wide (nchi nzima)

Mimi sio mtumishi wa Umma Wala sekta binafsi nimejiajiri.

Wakuu Jambo la Pili nahiitaji ..Kupata mchanganuo wa gharama kwa mwaka Ahsante na Mchana mwema.

Muhaya original
NHIF utopolo mkuu nenda bima za maana ukakate, tulio nhif tunataman kukimbia, kuna mabima yanatibu kila hospitali
 
NHIF utopolo mkuu nenda bima za maana ukakate, tulio nhif tunataman kukimbia, kuna mabima yanatibu kila hospitali
Mkuu kwani unaishi wapi, Mimi natumia NHIF hospital za private karibu zote Tena zenye ubora. Mtoto wangu alilazwa kwenye hospital nzuri Sana ya private NHIF hii ya 50400 ilimlipia Kila kitu.
 
50400/= ni kwa watoto na wanachuo tu.
Kifupi ni kuanzia watoto mpaka mwanafunzi wa Bachelor.

NHIF kuna vifurushi mbalimbali inategemea na uhitaji wako.

Kuna vya kufuatisha umri.! Na Vikundi pia Familia na Taasisi.

Kifamilia ni kama 1.5M jumla watu 6.

Umri kuna cha chini ya laki 2 mpaka laki sita hivi
 
NHIF ina ofisi zake na makao makuu yapo dsm.

Better tu uende hapo nijuavyo bima hii ipo juu kiasi na wana some conditions.

Huku huwezi pata unachotaka mia kwa mia
 
NHIF ina ofisi zake na makao makuu yapo dsm.

Better tu uende hapo nijuavyo bima hii ipo juu kiasi na wana some conditions.

Huku huwezi pata unachotaka mia kwa mia
Wafanyakazi wa pale Wana nyodo sio poa, ukifika unaonekana kama umekuja kuomba vile
 
Wafanyakazi wa pale Wana nyodo sio poa, ukifika unaonekana kama umekuja kuomba vile
Wanafanya kazi kama wanabembelezwa
Ila dawa yao ukifika pale ni kuwanyoosha tu

Ova
 
Nahitaji Bima ya NHIF mimi na watoto wangu wawili pamoja na Mama Mzazi.

Hiyo Bima iwe nation wide (nchi nzima)

Mimi sio mtumishi wa Umma Wala sekta binafsi nimejiajiri.

Wakuu Jambo la Pili nahiitaji ..Kupata mchanganuo wa gharama kwa mwaka Ahsante na Mchana mwema
Muhaya original
Watoto wakatiee bima wao kama wao , usiwaingize kwenye plan yako ,k2a kila mtoto utalipia 50,000
Baada ya hapo wewe na mkeo ndo mkate bima yenu, kwa baba na mama kutegemeana na hospitali urakazo tibiwa inaanzia laki sita hadi milioni na point kadhaa
 
Hivi hii ya Najali afya ya 192,000 inaweza kuwa sawa na ile ya mwanachuo 50,400? Ya mtoto au Ile ya wafanyakaz wa serikal, nahofia nawea kukata ya 192 ikawa na vikwazo kibao maana nilikuwa nayo ya chuo Kwa 50,400 service nyingi nilikuwa napata
 
Back
Top Bottom