Deleted_account
JF-Expert Member
- Nov 1, 2008
- 3,385
- 3,702
UHabari zenu wadau, nilikuwa nahitaji TV nikawa naperuzi mitandaoni kutafuta wauzaji na nikapata hawa wanajiita Electronic Dealers wanauza TV kwa bei nafuu toka Zanzibar na pia wanasafirisha kuja dar na mikoani,nikapata TV kwa 320,000. Jamaa nikaongea naye akasema nitume hela yeye anitumie mzigo,nikamwambia natuma nusu kwanza kiasi cha 200,000 halafu nikipokea mzigo nakamilisha hela. Bahati mbaya siku hiyohiyo kabla sijapokea mzigo nikapata tatizo la ghafla(msiba) na kutakiwa kusafiri haraka nikamwambia tuahirishe zoezi kwanza maana nina tatizo akasema haiwezekani ila nikimaliza mambo yangu nikamilishe hela anitumie.Baada ya siku mbili tatu nikarudi mjini na nikaongea naye akasema poa nimtumie kiasi kilichobaki na anitumie TV kwenye boti ya Azam ya asubuhi mapema kesho yake. Nikatuma hela kiasi kilichobaki 125,000 na ya kutolea ila kuanzia hiyo kesho yake akawa hapokei simu na muda mwingi ipo busy na baadaye ikawa haipatikani kabisa hadi leo hii. Imepita week nzima sasa.
Hela yote imekamilika(nilituma 325,000 jumla) na ushahidi wa msg upo. Sasa katika uchunguzi wangu nikakutana na matangazo kama yaleyale ya mwanzo ya TV yamefanana kila kitu kuanzia jina la kampuni, uandishi wa tangazo,location(ZNZ) na hadi bei za TV ila namba ndio tofauti. Nimepiga jana usiku aliyepokea akasema nipige leo asubuhi akiwa ofisini,leo wanasema haifahamu hiyo namba nyingine.
Hapa chini ni link la tangazo lake la awali ambalo nilinunua hiyo TV na namba ipo 0715606457,
Samsung 32 Inches Led HD Tv Zanzibar Central/South 86869875
na hii nyingine ni link ya tangazo jipya kwa namba nyingine Samsung Led 32 Inches Flat Screen Zanzibar Central/So883087
Naomba anayewafahamu hawa watu anisaidie namna ya kuwapata ili niweze kupata TV au kiasi changu cha fedha 325,000.
Nitaweka screenshot ya msg tulizokuwa tunawasiliana.
UPDATE:
Jamaa leo amepatikana kwenye simu anasema alikuwa safarini. Ameniblock, nikitumia simu nyingine anakata.
Hela yote imekamilika(nilituma 325,000 jumla) na ushahidi wa msg upo. Sasa katika uchunguzi wangu nikakutana na matangazo kama yaleyale ya mwanzo ya TV yamefanana kila kitu kuanzia jina la kampuni, uandishi wa tangazo,location(ZNZ) na hadi bei za TV ila namba ndio tofauti. Nimepiga jana usiku aliyepokea akasema nipige leo asubuhi akiwa ofisini,leo wanasema haifahamu hiyo namba nyingine.
Hapa chini ni link la tangazo lake la awali ambalo nilinunua hiyo TV na namba ipo 0715606457,
Samsung 32 Inches Led HD Tv Zanzibar Central/South 86869875
na hii nyingine ni link ya tangazo jipya kwa namba nyingine Samsung Led 32 Inches Flat Screen Zanzibar Central/So883087
Naomba anayewafahamu hawa watu anisaidie namna ya kuwapata ili niweze kupata TV au kiasi changu cha fedha 325,000.
Nitaweka screenshot ya msg tulizokuwa tunawasiliana.
UPDATE:
Jamaa leo amepatikana kwenye simu anasema alikuwa safarini. Ameniblock, nikitumia simu nyingine anakata.