Msaada: Mwanangu amebakwa na aliyembaka amekimbia

Msaada: Mwanangu amebakwa na aliyembaka amekimbia

Dah hapo mkuu inabidi ufuatilie kwa kina kwa maelfu ya wanawake waliojaa leo mitaani halafu mtu afikie kufanya kitendo kama hiko kwa binti yako ujue sio bure.

Mimi nahisi hapo kama una uwadui na mtu au kikundi flani ulikosana nao basi itakua wameamua kukupa jeraha kwa kumtuma mtu.

Hivyo ili kumpata adui yako hapo inakubidi uanzie mbali kidogo ila ukichukulia papara utaipoteza haki ya binti yako.

Pole kwa masahibu mkuu!
 
Lazima aanze dose ya PEP kwani hata akipimwa leo UKIMWI hautaonekana,muhimu aanze dose ndani ya masaa 72 kama sikosei,vinginevyo imekula kwako.

Huyo mbakaji utamfuatilia baadae hakikisha mtoto anapata huduma kwanza, baada ya hapo ndo umsake huyo mbakaji kwa mbinu za kijasusi atapatikana.
 
mbna hujibu mwanao ana umri gani? Isije kuwa ndo hawa wa miaka 17, anajitongozesha afu akipigwa mimba mnageuza kesi na kuanza kusema kabakwa
 
Kwanza mkuu nikupe pole sana kwa maswahibu ya mwanao kubakwa. Japo nimechelewa kucomment lakini hope itakusaidia next time when u experience the same attack. Kwanza Dr wa zahanati yupo sahihi kwa upande wake akitaka kutokupoteza forensic evidence yaani ushahidi wa kimazingira wa tukio hilo, lakini kiafya sio nzuri.

Kwahiyo kama mtu huwezi kumhudumia ni bora umweleze aende sehemu nyingne taratibu za kimsingi kwa mtu aliyebakwa inapaswa apimwe ujauzito yaani UPT kuthibitisha kwanza hakuwa mjamzito wakati anaingiliwa ili apatiwe dawa za kuzuia kutunga ujauzito, zipo nyingi effectiveness yake ni within 72 hours mfano emergency contraceptive pills.

Pili, anatakiwa afanyiwe kipimo cha maambukizi ya UKIMWI yaani SD bioline kama akiwa negative ili apewe dawa za kumkinga na maambukizi yaan post exposure prophylaxis yaan PEP kwa maana status ya mtu aliyemuingilia haijulikani. Pia, afanyiwe vipimo vingine vya maradhi ya ngono yaani STI's kama atabainika hana apewe prophylactic antibiotics kumkinga. Hivyo, si busara kumwacha mpaka kesho kwa justification ya forensic medicine pekee japo ni muhimu when it comes to legal issues.
I stand to be corrected

Mihayo DP
 
Pole mzazi na binti. Huyo atafutwe na sheria ichukuwe mkondo wake. Anaweza kuwa kakimbia lakini anajulikana.
 
Ndugu, mzazi na mtoto wanahitaji faraja siyo lawama. They are victims.
 
Poleh sana, mpeleke hospitali kubwa ili waweze kumuangalia then watampima afya wajue hali yake ya maambukizi ya VVU. Akiwa yupo salama watamuanzishia PEP ni dawa ya kumkimnga mtu asipate maambukizi. Mtu yeyote anayekua exposed anapatiwa hii dawa ila ndani ya saa 72 hivyo wahi mapema.
 
Back
Top Bottom