Msaada: Mke wangu mvivu kupindukia!

Msaada: Mke wangu mvivu kupindukia!

Ukwel huyo mkeo anatakiwa kambiwa reality jinsi maisha yanavyokwenda coz cku hiz maisha ni mafupi sana. Hivyo bac hata kama utawaandalia watoto maisha yao ya baadaye atashindwa kuhandle familia vzr zaid ya kufuja mali. jaman maisha ni kusaidiana
 
Labda anakushake shake akuone upo vipi. Ila biashara na shule ni shauku/passion, hamu na kipaji. Sio kila mtu anaweza kufanya biashara.

Ingekuwa vyema kama utaongea naye kuhusu hali nzima na muelekeo wa maisha..kisha umuulize yeye kipi ambacho anaweza kufanya kuongeza kipato chenu.

Kusoma lilikuwa ni wazo lako au lake? Kama ni lako ulimshirikisha kiasi gani? Usikute ulikuja tu na fomu kisha ukwambia "kesho au jumatatu unaanza shule"!!
 
Dah Mkuu nimekukubali, mleta mada jaribu kufata ushauri wa huyu mkuu!

Ingawa huyo shemeji yetu anasemekana kuwa ni mvivu, nashawishika kuandika kwamba anayo mazuri pia hasa katika management ya familia. Hakuna kazi ngumu na muhimu kama kutunza familia kamanda.

Jukumu la msing la mke/mama ni kutunza familia, kama ataweza kulifanya hilo kwa ufanisi mkubwa zaidi kuliko sasa ni bora zaidi.

Masuala ya economics za familia ni yako kaka. Acha mawazo ya hovyo ya eti nikifa kesho...what if akifa yeye...utaweza kufanya kazi anayofanya leo ya kutunza familia?? au unajua kutafuta fedha tu na kuacha mezani...acha hizo...unaweza kuta hata tarehe ya kuzaliwa first borne wenu umeisahau...!!! na yeye aje huku kulalamika????

TAFAKARI
 
@Enterprenegro, wewe wasema kwamba mengine si makanisa
Nilisemea kwa habari ya huduma ya maombi
 
Ni suala dogo lako ukicompare kama mwanamke angekuwa malaya,anatembea nje ya ndoa.muweke awe manager katika biashara zako huku wewe ukiwa MD,asubuhi unaamka naye mnaondoka pamoja,ukifika ktk ofisi yako aone kukuru kakara za kugombana na madereva,kuibiwa mafuta,kupata ajali gari etc,
kama na hapo akishindwa fight watoto wako wazoeze mapema kuendesha biashara.coz kuna matajiri wengi wake zao ni wa nyumbani ila watoto ndio wanaokuja kurun business
 
Mkirua sasa unadandia treni kwa mbele. Wapi nimesema nyumbani ndio kuzuri? Usichanganye ulevi na pombe tafadhali.

Lakini kimojawapo ndicho kisababishi cha kingine. Sijui kama mwenzetu unaweza kulewa bila pombe.... Pili unaposema huku maofisini unapotaka kumleta sio kuzuri unamaanisha kuwa nyumbani aliko ndiko kuzuri in comparison. And if that is the case you are wrong.
 
Id yako inasadifu vya kutosha ulio yaandika... Sizani kama mwanaume mwenye misimamo thabiti na uzoefu na mkewe kwa muda wote uo, anaweza kuja lalamika juu ya jambo dogo kama hilo... Msimamo wa mwanaume na hamu ya kufanya maamuzi magumu ni funzo tosha kwa mwanamke yeyote yule hapa duniani.

hilo nalo neno.......
 
samahani kwa swali hili, mke wako ni kabila gani? na ametoka katika familia ya aina gani, wenye uwezo sana au kawaida?
 

Ingawa huyo shemeji yetu anasemekana kuwa ni mvivu, nashawishika kuandika kwamba anayo mazuri pia hasa katika management ya familia. Hakuna kazi ngumu na muhimu kama kutunza familia kamanda.

Jukumu la msing la mke/mama ni kutunza familia, kama ataweza kulifanya hilo kwa ufanisi mkubwa zaidi kuliko sasa ni bora zaidi.

Masuala ya economics za familia ni yako kaka. Acha mawazo ya hovyo ya eti nikifa kesho...what if akifa yeye...utaweza kufanya kazi anayofanya leo ya kutunza familia?? au unajua kutafuta fedha tu na kuacha mezani...acha hizo...unaweza kuta hata tarehe ya kuzaliwa first borne wenu umeisahau...!!! na yeye aje huku kulalamika????

TAFAKARI

soma post vzr msee nakuandika sana sio kwamba umesaidia....think twice.
 
is she good in bed?
anajipamba sawasawa yani ile wanja unakaa mahali pake?
ananukia full time?
WATU WENGINE WAMEZALIWA KWA AJILI YA KUWA MAHALAIT HASA!
ikubali tu hiyo species ya mkeo!
huwezi kumbadili sasa!
 

Ingawa huyo shemeji yetu anasemekana kuwa ni mvivu, nashawishika kuandika kwamba anayo mazuri pia hasa katika management ya familia. Hakuna kazi ngumu na muhimu kama kutunza familia kamanda.

Jukumu la msing la mke/mama ni kutunza familia, kama ataweza kulifanya hilo kwa ufanisi mkubwa zaidi kuliko sasa ni bora zaidi.

Masuala ya economics za familia ni yako kaka. Acha mawazo ya hovyo ya eti nikifa kesho...what if akifa yeye...utaweza kufanya kazi anayofanya leo ya kutunza familia?? au unajua kutafuta fedha tu na kuacha mezani...acha hizo...unaweza kuta hata tarehe ya kuzaliwa first borne wenu umeisahau...!!! na yeye aje huku kulalamika????

TAFAKARI

wooord!
 
Anapenda kuzurura?
Anakutunzia mali yako ile...?
Analea watoto vyema?
Kama haya yapo sawa basi jaribu kumvumilia tu.
 
Mkuu mshukuru Mungu huyo mke wako anakutunzia watoto wako na wewe anakutimizia mahitaji kama mke. Huko maofisini unakotana kumleta mke wako si kuzuri, kuna mambo mengi tunayaona na kuwafanyia wake za watu yasiyostahili. Kama hana munkari wa kazi au biashara au shule haina maana ni mke kilaza. Tafuta kitu atakachofanya kitakachokuwa na interest kwake. Lakini usimhukumu after 7 years, lazima kuna mazuri uliyaona kwake. Wewe ndio baba na kidume kwenye familia, kutunza familia ni jukumu na wajibu wako. La msingi waandalie mazingira mazuri wanao endapo Muumba ataamua kukuita mbele ya haki wangali wadogo. Tusifananishe wake zetu na wake wa marafiki zetu kwani hujui wao wanaumiza vichwa kwa lipi.
bonge la ushauri kaka yaani mabo ninayo yaona huku ofisini wakifanyiwa wake za watu....kamwe mke wangu hatokuja kufanya kazi nitaendelea kumuweka akae ndani hivihivi kama sasa sina preshaaa yoyote
 
Pole sana aisee huwa nawasikitikia wanawake wenzangu wasiotaka kujishughulisha.Niunganishe nae nimpe darasa.Mie namshukuru Mungu alinipa hekima ya kujitambua na kufanya kazi zangu kwa bidii.Namshukuru Mungu kwa hilo Hata sasa Mme wangu katangulia mbele ya haki lakini Familia haijateteleka.Maana nilishazoea kujitafutia pesa yangu wenyewe.

Yaani akina mama jamani jamani fanyeni kazi siku mwenzio akitangulia mbele ya haki utalia adi uchanganyikiwe maana umezoea vya buree.
 
pole sana.. mwambie unataka kuoa mke mwingine ambaye atajishughulisha mtafute pesa ili msaidiane naye kumtumza yeye..si anataka kutunzwa??ili hata ukidondoka leo basi wife mdogo ataisaisaidia familia...hapo utaona km atalemaa!! subutu!!!!!
Habari,
Mimi nimeoa na ndoa yangu ina miaka 7 sasa na tuna watoto wa 2. Nlimuoa mwanamke aliyekuwa kamaliza degree ambaye alikuwa home tu at the time anatafuta ajira. Toka nimuoe hajawahi kufanya kazi yoyote ile yaani Goalkeeper mpaka leo na kutafuta kazi alisha acha. Mpaka leo hii mke wangu hajabadilika. Namlipa mshahara mwisho wa mwezi ambao ni sawa na kama 10k per day yaani (300k). Kila ninapojaribu kumtafutia kazi anafanya kidogo tu anaacha. Huwezi amini hata umlazimishe vipi ajishughulishe mzito ile mbaya. Mi ni mfanyabiashara(Magari Makubwa) nimemuanzishia vimiradi through the years vyote kala mtaji. Kuna kipindi alijaribu kusoma masters ya bussiness administration nkamlipia ada, nunua vitabu vyote alafu yeye akaamua kuacha baada ya mwezi tu Eti kuamka alfajiri hawezi. Nkaja nkamuomba basi asome chuo ambacho atakuwa anaingia mchana nacho alishindwa.

Tatizo rafiki yake mkubwa ni mama yangu mzazi hivo kuna kipindi nlikata mshahara wake ili kumlazimisha afanye kazi akakimbilia kulia manyanyaso nikalazimishwa hela yake isiguswe na wazazi wangu. Nkienda kazini namuacha nyumbani na home kwenyewe hafanyi chochote anaita tu housegirl. Yaani yupo yupo tu siku hadi siku. Nifanyaje ili hata nikianguka leo au kesho awe ni mama atakayeweza kusomesha watoto.

Alafu matumizi yake ya hela mabaya yaani hela yake mwenyewe ukimpa mwanzo wa mwezi kwenye tarehe 1 hiv basi ikifika tarehe 8 ujue alikuwa anaumwa. Ila ni hela yake na hainunui hata nguo ya mtoto hivyo hainihusu. Nifanyaje ajishughulishe?
 
Back
Top Bottom