Msaada: Mke wangu mvivu kupindukia!

Msaada: Mke wangu mvivu kupindukia!

Dah,hela unazompa zinamzingua anaona hakuna haja ya kujishughulisha kwa kweli sie wanawake muda mwingine majanga tu jaribi kumkalisha chini umweleze unavyokereka na tabia yake kwa kweli mi mtu mvivu namchukia kupita kiasi na nyie muwe mnachunguza kwanza uzuri wa mwanamke ni tabia siyo sura kuna mapungufu ya kuweza vumilia lakini siyo uvivu hata Mungu hapendi
 
poor choice pole sana, back to topic kata hela za matumzi kabisa na kuwa muwaazi kwake kwa nini anatakiwa kufanya kazi. kama hiyo ni ngumu kama unamiradi mikubwa bora hizo hela za kumpa mkeo fungua akaunti ya watoto weka hela huko kwa sababu leo haupo duniani watoto wako watapoteza dira kabisa,
 
Mkuu una akili sana,mke mwenza ndo dawa yake! Afu na hii mijike ya kuokota mitaani eti kasoma pumbafu sana! Mwaka wa kuoa naenda kwetu naongea na bibi nipate mwanamke mchapakazi,na adabu juu! Asa kama kazi hataki kwanini alisoma? Ningekuwa mie ligi tu hata mama asemeje simsikilizi maana huo ni ujinga
mtafutie mke mwenzake!
 
muulize yeye anataka nini katika maisha, nini anataka achive, mmpe black and white na mustakabali mzima wa maisha mtishie kuwa wewe unasafiri na magari ikatokea siku ukapata ajari? atufyekwa! may God forbid! yeye ataisheje? mpe challenge hadi atie akili then atafika point atasema kweli lakini!
 
Kufuatana na maelezo yako mkeo ni msomi.Kitu kinachomsumbua ni upweke. Na hii inatokana na kutokuwahi kufanya kazi alipomaliza chuo na kukaa sana nyumbani.Hii husababisa msongo wa mawazo. Kingine inaonyesha, kutokana na maneno yako unamdharau yeye na mawazo yake.Hili pia litamwongezea kutokujiamini na woga wa kujaribu.Kitu unachoweza kukifanya ni kumpa moyo badala ya kumbeza na kumdharau,mtafutie safari ya nje ya nchi ili kuona mazingira mengine.Hii inaweza kuwa kufanya kozi fupi 'Europe' za stadi za maisha ili awe 'exposed' zaidi. Baada ya hii atabadilika utashangazwa mwenyewe..
 
Haya mambo ni personal sana hayatuhusu!!

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
kumbe kuna kulipana mishahara ndani ya ndoa aiseee!!!
 
Pole sana ila tafuta suluhsho..ambapo unaeza kutumia peaceful means kama kukaa nae chn kuongea nae na kuonesha jinsi gani huo uvivu wake ulivo na madhara katk ndoa yenu,leo upo kesho ucpokuwepo je?hao watoto wataish vp?
Au unaeza kuongea na mama yako ambae nh rafk yake mkubwa,wew n mama yako mzaz atakuelewa tu,ebu ongea nae umwambie jinsi hlo jambo linavokuumiza aongee na mkeo...japo mkeo km c muelewa na anaipenda hyo tabia yake ya uvivu hatapendezwa na jambo la kuambiwa ukwel na mamake mkwe.
Kumbuka c katk matatzo yote peaceful means ina work out,ikshndkana onesha u mwamwanaume na unasay ktk familia,acha kumlipa huo mshahara maana hakuna kaz anafanya maana hzo shugul za nyumbani anafanya housegirl hzo za chumbani n wajbu wake,acha kumpa hela mfanye aone mambo yako hayako vzur,akimic izo pesa ataona umuhmu wakufanya kazi.
Ila mke wako bro kazd yan ni mvivu had kufikii,ndo maana wanaume wengne wanatafuta nyumba ndogo ila wewe uctafute nyumba ndogo ila hyohyo kubwa ibadilishe..
 
Mkuu mshukuru Mungu huyo mke wako anakutunzia watoto wako na wewe anakutimizia mahitaji kama mke. Huko maofisini unakotana kumleta mke wako si kuzuri, kuna mambo mengi tunayaona na kuwafanyia wake za watu yasiyostahili. Kama hana munkari wa kazi au biashara au shule haina maana ni mke kilaza. Tafuta kitu atakachofanya kitakachokuwa na interest kwake. Lakini usimhukumu after 7 years, lazima kuna mazuri uliyaona kwake. Wewe ndio baba na kidume kwenye familia, kutunza familia ni jukumu na wajibu wako. La msingi waandalie mazingira mazuri wanao endapo Muumba ataamua kukuita mbele ya haki wangali wadogo. Tusifananishe wake zetu na wake wa marafiki zetu kwani hujui wao wanaumiza vichwa kwa lipi.

Amemaliza mkuu hapo' kiufupi no comment fuata ushauri huo!!
 
Habari,
Mimi nimeoa na ndoa yangu ina miaka 7 sasa na tuna watoto wa 2. Nlimuoa mwanamke aliyekuwa kamaliza degree ambaye alikuwa home tu at the time anatafuta ajira. Toka nimuoe hajawahi kufanya kazi yoyote ile yaani Goalkeeper mpaka leo na kutafuta kazi alisha acha. Mpaka leo hii mke wangu hajabadilika. Namlipa mshahara mwisho wa mwezi ambao ni sawa na kama 10k per day yaani (300k). Kila ninapojaribu kumtafutia kazi anafanya kidogo tu anaacha. Huwezi amini hata umlazimishe vipi ajishughulishe mzito ile mbaya. Mi ni mfanyabiashara(Magari Makubwa) nimemuanzishia vimiradi through the years vyote kala mtaji. Kuna kipindi alijaribu kusoma masters ya bussiness administration nkamlipia ada, nunua vitabu vyote alafu yeye akaamua kuacha baada ya mwezi tu Eti kuamka alfajiri hawezi. Nkaja nkamuomba basi asome chuo ambacho atakuwa anaingia mchana nacho alishindwa.

Tatizo rafiki yake mkubwa ni mama yangu mzazi hivo kuna kipindi nlikata mshahara wake ili kumlazimisha afanye kazi akakimbilia kulia manyanyaso nikalazimishwa hela yake isiguswe na wazazi wangu. Nkienda kazini namuacha nyumbani na home kwenyewe hafanyi chochote anaita tu housegirl. Yaani yupo yupo tu siku hadi siku. Nifanyaje ili hata nikianguka leo au kesho awe ni mama atakayeweza kusomesha watoto.

Alafu matumizi yake ya hela mabaya yaani hela yake mwenyewe ukimpa mwanzo wa mwezi kwenye tarehe 1 hiv basi ikifika tarehe 8 ujue alikuwa anaumwa. Ila ni hela yake na hainunui hata nguo ya mtoto hivyo hainihusu. Nifanyaje ajishughulishe?

Pole na hapo ulidondoka pasipo, ilopo jaribu kuwashirikisha wazazi wake uwasikilize na wao watasema je kuhusu binti yao
 
Mkuu mshukuru Mungu huyo mke wako anakutunzia watoto wako na wewe anakutimizia mahitaji kama mke. Huko maofisini unakotana kumleta mke wako si kuzuri, kuna mambo mengi tunayaona na kuwafanyia wake za watu yasiyostahili. Kama hana munkari wa kazi au biashara au shule haina maana ni mke kilaza. Tafuta kitu atakachofanya kitakachokuwa na interest kwake. Lakini usimhukumu after 7 years, lazima kuna mazuri uliyaona kwake. Wewe ndio baba na kidume kwenye familia, kutunza familia ni jukumu na wajibu wako. La msingi waandalie mazingira mazuri wanao endapo Muumba ataamua kukuita mbele ya haki wangali wadogo. Tusifananishe wake zetu na wake wa marafiki zetu kwani hujui wao wanaumiza vichwa kwa lipi.

Kweli huko maofisini hakufai ila kitendo cha kukung'uta mtaji nacho kinauma na mbaya zaidi ni mtu aliyeelimika
 
Back
Top Bottom