msaada; meno ya arusha.

Going Concern

JF-Expert Member
Jul 25, 2011
1,071
1,211
heshima kwenu ndugu zangu!!!
namchumba wangu toka pande za arusha, nampenda sana, na kama mungu akipenda very soon atakua mama watoto, ila anameno ya arusha(yameungua). sio kwamba yananiboa ila kama kuna dawa ningependa mnisaidie coz ata yeye anapenda sana meno meupe. shukrani ndugu zangu.
 
Mkubwa kwani wewe una makazi hapa A town?????????????

Bila shaka vitengo vipo kwani pale Njiro kuna hosptali moja ya kanisa ila inafanyaga kazi isipokuwa jumamosi tu na hata pale Kwa Ngulelo kabla ya kufika ile ofisi ya wale mafsadi wa sisiem mkono wa kushoto kama unatokea mjini Arusha na bila shaka utakuwa umepata huduma utakayo mkubwa wangu:
 
Nenda SDA njiro au Hapo Mbele ya kwa mrefu kama unaingia town.

Dakika sifuri tu yatakuwa meupe
 
Natafuta sehemu watakayobadili yangu meupe yawe kama ya kiarusha.
Nayapenda sana mie
OTIS
 
Meno Chiki si arusha tu bali hata geita,singida na mikoa mingine yenye madini flani hivi.
 
Kichwa ngumu kuelewa au dhihaka?

Nilikuwa sielewi yanatambulika vipi,ila nimeshangaa kuona muanzisha thread kayaita meno ya Arusha na kila mtu kayatambua; kama hii thread ningekuanimeanzisha mimi ningeyaita meno yaliyoathirika na maji ya arusha. usinielewe vibaya
 
Back
Top Bottom