Msaada: Mdogo wangu yupo darasa la 6 ila jina limetoka kwenye matokeo ya darasa la 7 ikidaiwa jina lake liliuzwa

Ushauri wangu .naomba ufuatilie sasa usipofuatilia alafu ukakuta hilo jina ni la mdogo wako. Tatizo kubwa Moja litatokea mwakani wakati anasajiliwa ili afanye mtihani was taifa drs la 7 ni kwamba itahitajika matokeo yake ya mtihan wa taifa drs la 4 na necta kule itaonekana jina Hilo limeshamaliza drs la 7 hivyo dogo hataruhusiwa kufanya mtihani. Siku hizi hakuna udanganyifu necta wapo kidigital mzee hakuna uhuni uhuni.
 
Wakuu habari zenu? Mmeshindaje?

Sasa Wakuu kuna shida kidogo nahitaji ushauri wenu kuna mdogo wangu alikuwa anasoma Arusha shule ya msingi sasa kule kulitokea shida kidogo akaamishwa shule akaletwa Ukerewe.

Wakati anaamishwa alkuwa darasa la sita lakini shuleni alipohamia Mwalimu Mkuu akakataa kumpokea mpaka arudishwe darasa la tano, basi ikawa hivyo dogo akarudi darasa la tano.

Sasa maajabu yameibuka leo baada ya matokeo kutoka dogo bado yupo darasa la sita mwakani anamaliza darasa la saba lakini jina lake limetoka kwenye matokeo kwamba amefaulu kwa daraja B.

Baada ya hapo nikafanya kuulizia marafiki wakadai Mwalimu Mkuu aliuza jina kwa mrudiaji. Sasa nahofia hatima ya mdogo wangu mwakani atakapofika darasa la saba itakuwaje?.

Kwa wanasheria ebu mnishauri nifanye nini kwa mjibu wa sheria, maana kinachoniuma ni mtu mwingine kumiliki jina la ukoo wetu.

Wanasheria na wakuu naomba kuwasilisha
Acha papara mdogo wako yuko darasa la sita na aendelee na darasa la sita,aliyekwambia jina ni mali ya mdogo wako ni nani? Majina hufanana,mdogo wako atafanya mtihani mwakani period.
 
Ushauri wangu .naomba ufuatilie sasa usipofuatilia alafu ukakuta hilo jina ni la mdogo wako. Tatizo kubwa Moja litatokea mwakani wakati anasajiliwa ili afanye mtihani was taifa drs la 7 ni kwamba itahitajika matokeo yake ya mtihan wa taifa drs la 4 na necta kule itaonekana jina Hilo limeshamaliza drs la 7 hivyo dogo hataruhusiwa kufanya mtihani. Siku hizi hakuna udanganyifu necta wapo kidigital mzee hakuna uhuni uhuni.
Mtoto akirudia darasa taarifa zinaenda mamlaka husika na anapata kibali.Kama utaratibu ulifuatwa hakuweza kuwa na tatizo.Ushauru,mleta mada kamuone mwalimu mkuu wa shule anayosoma sasa mdogo wako ndo atakupa majibu mujarabu,ikishindikana nenda halimashauri kwa Afisa Elimu.
 
Mzee baba jina ambalo halina hata cheti cha la7 liuzwe kwa faida gani!? Acha mawazo potofu....


Majina hata manne yanaweza fanana! Matatu kitu gani?
 
ww umejuaje kama walicheza mchezo mkuu.
Usijazwa upepo mkuu mambo mengine sio ya kukurupuka, kumbuka jina halina dhamana yeyote anaweza kujiita kadili anavyopendezwa.
.


hapana mdogo wangu hakuwa mtoro kabisa isipokuwa walimu walicheza mchezo haram
 
Wakuu habari zenu? Mmeshindaje?

Sasa Wakuu kuna shida kidogo nahitaji ushauri wenu kuna mdogo wangu alikuwa anasoma Arusha shule ya msingi sasa kule kulitokea shida kidogo akaamishwa shule akaletwa Ukerewe.

Wakati anaamishwa alkuwa darasa la sita lakini shuleni alipohamia Mwalimu Mkuu akakataa kumpokea mpaka arudishwe darasa la tano, basi ikawa hivyo dogo akarudi darasa la tano.

Sasa maajabu yameibuka leo baada ya matokeo kutoka dogo bado yupo darasa la sita mwakani anamaliza darasa la saba lakini jina lake limetoka kwenye matokeo kwamba amefaulu kwa daraja B.

Baada ya hapo nikafanya kuulizia marafiki wakadai Mwalimu Mkuu aliuza jina kwa mrudiaji. Sasa nahofia hatima ya mdogo wangu mwakani atakapofika darasa la saba itakuwaje?.

Kwa wanasheria ebu mnishauri nifanye nini kwa mjibu wa sheria, maana kinachoniuma ni mtu mwingine kumiliki jina la ukoo wetu.

Wanasheria na wakuu naomba kuwasilisha
Je, jina la mdogo wako kutoka limefaulu mwaka huu, linamzuia yeye kuchaguliwa kuendelea na masomo mwakani kama atafaulu? Aliyefaulu kwa jina hilo achana naye, wala usiwe na kinyongo naye
 
Majina yanafanana, umejuaje ni la mdogo wako.
Unaweza fananisha majina matatu maana mtu anatambulika kwa jina lake la baba na la ukoo kwahyo yote yafanane au umetoka kuchambia pilipili umekuja kutafuta unga wa ngano tukakusugue
 
Back
Top Bottom