MSAADA: Mama mkwe amenifungulia kesi ya uharibifu wa Mali

Status
Not open for further replies.

jovetha

Member
Apr 16, 2016
40
18
Naombeni msaada wa mawazo maana nahisi nitakufa kwa mawazo ila ninajikaza. Mimi ni mama wa miaka 30 Nina mtoto mmoja, nina ndoa ya kimila. Nampenda sana mme wangu lakini tumekuwa hatuna maelewano mazuri mimi na yeye kwa sababu ni mtu wakusikiliza ndugu na pia ni mtu ambaye anaona mawazo ya ndugu zake ndio mawazo sahihi especially his mum, mpaka ikafika hatua ya yeye kuhama nyumbani na kwenda kuishi kwa wazazi wake ambao hawako mbali na tunapoishi yapata mwaka sasa tangu aondoke vikao vya kifamilia tumeshakaa lakini hakuna suluhu mpaka Sasa ambayo imefanikiwa.

Sasa hapa ninapoishi tuna nyumba mbili, nyumba Moja ni mpya bado hatujahamia hivyo tumeifanya kama store pia tulikuwa tumeshaweka na vitu vingine kama makabati ili tuweze kuhamia, kutokana na migogoro yetu mpaka sasa hatujahamia.

Hivi karibini nilipoteza ufunguo wa hiyo nyumba mpya hivyo ikanibidi nimuite Fundi ili aweke kitasa kipya ili niweze kufanyia nyumba usafi maana hapa tunapoishi Kuna mchwa wengi hivyo nilazima kufanya usafi vitu visiharibiwe na mchwa. Baada ya kubadilisha kitasa nikamwambie dada apafanyie usafi, wakati dada akiendelea na usafi,

Mara shemeji akaja amkamfukuza yule mdada na kuchukua zile funguo za nyumba na baadae mama mkwe alifika nyumbani na rafiki yake akinigombeza kwanini nimevunja mlango wa nyumba, nikamwambia sijavinja nimebadikisha kitasa, akaniambia kwanini nabadilisha kitasa cha nyumba bila kumpa taarifa, nikamwambie, nyumba si yangu na mme wangu ndio maana sijawapa taarifa kama nimebadilisha kitasa na baada kama ya siku 10 kupita nikapigiwa simu nahitajika kituo cha police kufika pale nikaambiwa nimeshitakiwa na mama mkwe kwa uharibifu wa Mali na kesi ikapelekwa mahamani mind you kwenye kiwanja tulichojenga tulipewa na baba mkwe.

Naombeni msaada wa kisheria juu ya hii case
 
duh aisee pole, ila kwajinsi nilivyoelewa huo mgogoro wote utategemea sana mahusiano yako na mmeo, kama hamuelewani itakuwa ngumu sana maana hata hicho kiwanja unachosema mlipewa na mkwe anaweza akakana kama mzee aliwapa, hapo ukasema upambane kazi itakuwa kubwa ni heri uangalie namna gani busara itumike usije ukakosa kila kitu
 
Hamna kesi hapo. Jielezee kama ulivyojielezea hapa.

Uwe tu na uthibitisho kama ni mke halali kwa mujibu wa sheria na ni kweli funguo zilipotea.
Inaonekana wamejenga nyumbani kwa mume na mume hawalewani so hapo hata nyumba ukute ma mkwe anasema ni ya kwake na kwakuwa imejengwa kwake hapo kuna mtihani
 
So sad naogopa sana hadi hapo wewe ni virus kwenye hio familia na pamoja na mumeo hawakutaki na unajiamini nini mume ahame nyumbani na unaendelea kuishi hapo?
Mume kashatekwa ndio basi tena
 
Na mme yupo upande wa mama yake,wametafuta Hadi Mwanasheria Nia Yao kubwa ni Mimi wanifunge.
Wanataka utubu uombe kuondoka hapo na ndoa iwe basi, chagua uondoke hapo na ukiondoka hapo mtoto awe mali yako, hakikisha mjumbe, serikali za mitaa wanafahamu hilo na kwanini hujaita wazazi wako mpaka leo kukemea hilo na ukaondoka, jiamini una mikono na akili ondoka na hakikisha mtoto awe mali yako usimtambue baba ukiondoka
 
Na mme yupo upande wa mama yake,wametafuta Hadi Mwanasheria Nia Yao kubwa ni Mimi wanifunge.
Mkuu hapo naona we utakiwa so inatafutwa njia ya kukuondoa bila kupata chochote, hivyo vingine ni vitisho tu,
 
Naombeni msaada wa mawazo maana nahisi nitakufa kwa mawazo ila ninajikaza.Mimi ni mama wa miaka 30 Nina mtoto mmoja, nina ndoa ya kimila.Nampenda sana mme wangu lakini tumekuwa hatuna maelewano mazuri mm na yeye kwa sababu ni mtu wakusikiliza ndugu na pia ni mtu ambaye anaona mawazo ya ndugu zake ndo mawazo sahihi especially his mum,mpaka ikafika hatua ya yeye kuhama nyumbani na kwenda kuishi kwa wazazi wake ambao hawako mbali na tunapoishi yapata mwaka sasa tangu aondoke vikao vya kifamilia tumeshakaa lakini hakuna suluhu mpaka Sasa ambayo imefanikiwa.

Sasa hapa ninapoishi tuna nyumba mbili, nyumba Moja ni mpya bado hatujahamia hivyo tumeifanya kama store pia tulikuwa tumeshaweka na vitu vingine kama makabati ili tuweze kuhamia, kutokana na migogoro yetu mpaka sasa hatujahamia.

Ivi karibini nilipoteza ufunguo wa hiyo nyumba mpya hivyo ikanibidi nimuite Fundi ili aweke kitasa kipya ili niweze kufanyia nyumba usafi maana hapa tunapoishi Kuna mchwa wengi hivyo nilazima kufanya usafi vitu visiharibiwe na mchwa. Baada ya kubadilisha kitasa nikamwambie dada apafanyie usafi,wakati dada akiendelea na usafi,Mara shemeji akaja amkamfukuza yule mdada na kuchukua zile funguo za nyumba na baadae mama mkwe alifika nyumbani na rafiki yake akinigombeza kwanini nimevunja mlango wa nyumba,nikamwambie sijavinja nimebadikisha kitasa,akaniambia kwanini nabadilisha kitasa Cha nyumba bila kumpa taarifa,nikamwambie,nyumba si yangu na mme wangu ndo maana sijawapa taarifa kama nimebadilisha kitasa na baada kama ya siku 10 kupita nikapigiwa simu nahitajika kituo Cha police kufika pale nikaambiwa nimeshitakiwa na mama mkwe kwa uharibifu wa Mali na kesi ikapelekwa mahamani mind you kwenye kiwanja tulichojenga tulipewa na baba mkwe.Naombeni msaada wa kisheria juu ya hii case
Na je ni mfanyakazi una elimu gani au mama wa nyumbani tu bila kazi nje na ulezi wa mtoto?
 
I wish ningeweza kufanya hivyo,but nawaza nitaanzia wapi saivi na kipindi Cha Corona nilipoteza kazi yangu mpaka Sasa sina kazi.I wish ningekuwa na kazi ningeweza kulipa Kodi na kumood mahitaji mengine madogo madogo
Elimu yako please na uko mkoa gani, wilaya na specific mtaa
 
Ni kweli kabisa, na hizi nyumba mbili zote zipo kwenye fance Moja na mm ndo nakaa hapa pekee yangu.Sina cheti Cha ndoa lakini ninazopicha za mahali
aah km ni hivyo hawawez kukudhulumu hapo, ht km huna cheti cha ndoa still una haki, mmeishi kwa muda gani na huyo mmeo? ila dada mpk mme anakimbia nyumba anakuachia shida nn? maana ni maamuz magum hayo usikute naye kaenda omba msaada kwa nduguze, ila haijalishi mmegombana nn au kuna nn kila mtu anastahili hak yake, watafute wale wanajiita wasaidizi wa kisheria
 
For now i am not ready cz am not stable financially, Siogopi kwasabu namwamini Mungu
wazazi wanasemaje na uko umbali gani na kwenu hapo ulipo, je mama mkwe si mshirikina au ana nguvu gani ya kipesa au nini hasa,
 
Naombeni msaada wa mawazo maana nahisi nitakufa kwa mawazo ila ninajikaza.Mimi ni mama wa miaka 30 Nina mtoto mmoja, nina ndoa ya kimila.Nampenda sana mme wangu lakini tumekuwa hatuna maelewano mazuri mm na yeye kwa sababu ni mtu wakusikiliza ndugu na pia ni mtu ambaye anaona mawazo ya ndugu zake ndo mawazo sahihi especially his mum,mpaka ikafika hatua ya yeye kuhama nyumbani na kwenda kuishi kwa wazazi wake ambao hawako mbali na tunapoishi yapata mwaka sasa tangu aondoke vikao vya kifamilia tumeshakaa lakini hakuna suluhu mpaka Sasa ambayo imefanikiwa.

Sasa hapa ninapoishi tuna nyumba mbili, nyumba Moja ni mpya bado hatujahamia hivyo tumeifanya kama store pia tulikuwa tumeshaweka na vitu vingine kama makabati ili tuweze kuhamia, kutokana na migogoro yetu mpaka sasa hatujahamia.

Ivi karibini nilipoteza ufunguo wa hiyo nyumba mpya hivyo ikanibidi nimuite Fundi ili aweke kitasa kipya ili niweze kufanyia nyumba usafi maana hapa tunapoishi Kuna mchwa wengi hivyo nilazima kufanya usafi vitu visiharibiwe na mchwa. Baada ya kubadilisha kitasa nikamwambie dada apafanyie usafi,wakati dada akiendelea na usafi,Mara shemeji akaja amkamfukuza yule mdada na kuchukua zile funguo za nyumba na baadae mama mkwe alifika nyumbani na rafiki yake akinigombeza kwanini nimevunja mlango wa nyumba,nikamwambie sijavinja nimebadikisha kitasa,akaniambia kwanini nabadilisha kitasa Cha nyumba bila kumpa taarifa,nikamwambie,nyumba si yangu na mme wangu ndo maana sijawapa taarifa kama nimebadilisha kitasa na baada kama ya siku 10 kupita nikapigiwa simu nahitajika kituo Cha police kufika pale nikaambiwa nimeshitakiwa na mama mkwe kwa uharibifu wa Mali na kesi ikapelekwa mahamani mind you kwenye kiwanja tulichojenga tulipewa na baba mkwe.Naombeni msaada wa kisheria juu ya hii case
Huyo mama mkwe Hana mume wake? Mwambie akapambane na ndoa yake
 
Elimu yako please na uko mkoa gani, wilaya na specific mtaa
7003063.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
I know,maana walianza case ya Talaka ilivyofika kipengele Cha chumo la pomoja wakawithdral case na ndo baadae kifungua hii
You have a good point here kesi iko mahakama ileile au ingine, sifahamu sheria hivi mahakimu sip walezi wetu kwamba yule wa talaka uombe kuonana nae atakusaidie pia katika hili na hio kesi ya talaka iwe baseline
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom