mikatabafeki
JF-Expert Member
- Dec 29, 2010
- 12,772
- 4,641
sioni sababu ya huyo bwana kuendelea kushikilia kuti kavu
ila mwanaume akitoka kwenda kwenye kilaji mwanamke alikuwa anafuatilia kila baada ya dk kadhaa mara umekaa na nani unatoka saa ngapi na mwanaume asiposema muda halisi wa kurudi atashangaa mwanamke amefika anamjoin hata kama alikuwa na wenzake wanaongea
Na kweli hilo jini tena ndio mama wa hayo majini ya kile du!mmmmh! sio kila sketi/gauni uionayo barabarani ukahisi ni mwanamke wengine ni majini ya kike sasa uyo rafiki ako alikutana na jini la kike
Kesi za ndoa haziishi!
mambo ya fweza sio,mulllas...hahahakuna msemo...wen poverty enters thru the door love escaes thru the window...na hilo ndio lilimtokea jamaa yako hapa...akubali imekula kwake tuu hapa
labda ndo utaratibu wao wa maisha kaka. muulize rafiki yako wakati akia kwenye enzi yake ilikuwaje? kuna mwanaume akiulizwa na mkewe uko wapi,anasema rose garden.ukimuambia niko hapa sayansi nakuja mume wangu, anakuambia niko salender bridge! labda hawaambianagi ukweli,kila mtu ana mapenzi yake,na wanakua na sababu nzuri tu.
wanajamvi
nimekutana na mkasa huu nikaombwa ushauri nikaona nililete jamvini kupata mawazo zaidi..
Jamaa analalamika kuhusu mabadiliko ya tabia ya mkewe hasa makundi na ulevi . wameishi kwa kipindi cha miaka miwili tangu waoane ndoa ya kimila, mwanzo walikuwa na maelewano mazuri na hata mambo mengi walikuwa wanashirikiana katika kufanya na kuamua..
kama miezi 6 iliyopita jamaa alipata matatizo kazini yakapelekea yeye kuamua kuacha kazi ili kujinusuru na maswaiba mengineyo.. sasa mke amekuwa na makundi ya kike na kiume na kila mtu anasema n mfayakazi mwenzake , sometime anamwita jamaa awajoin kwenye kinywaji (pombe) but inakuwa in last minute.
Mke anaweza kukaa kwenye ulevi hadi saa sita usiku au nane usiku ndo anarudi nyumbani.
jamaa mwanzo alikuwa anapenda kumuuliza labda alipo anaishia kuambia yupo point A kumbe hayupo au akaambia niko njiani nakuja kuanzia saa 4 hadi 7 usiku ndo anaingia .. kwa sasa hawana maelewano mazuri ndani ya nyumba kwani jamaa ameshakuta msg hata za mapenzi kwenye simu ya mkewe na mkewe akashindwa kumshawishi jamaa na jamaa anaamua kukaa kimya maana alishawahi kutoa vipigo ila anaona kama dharau inazidi..
Ksasa hawaongei ni kama week ya tatu, mke anaweza kutoka hata kuaga hakuna na hata akirudi sometime hamsalimii jamaa na jamaa ameamua kusitisha hata huduma ya chakula cha usiku ..
Jamaa anafikiria kuachana nae ila anaumia kwani wana mtoto mchanga ana miezi 5 na mke alimwachisha ziwa mtoto akiwa na miezi 2..
Wana jamvi hili mwalionaje??
Lakini hata hivyo king'asti huyu dada hapa anamkomoa nani? mumewe au mtoto? mbona mtoto ni mdogo mno kuadhibiwa kisa eti baba alikua anapitiaga rose garden au sijui wapi wapi. Wakiachana halafu mtoto akalelewa na mama wa kambo huyo mama akianza kumtesa mnalaumu mama wa kambo. Wanawake na sisi bwana wakati mwingine
maty, ukiskiza kesi ya ndoa upande mmoja utaona jinsi hawa watu wako biased. ukiona simba amekimbia ameacha mtoto ujue ngoma imebamba. hapa anaonekana mbaya huyo mwanamke tu,unajua ukimpewa huyo baba unaweza ukamuua ukasahau kumrudisha kwa mkewe! siamini kaka mwanamke ana pumzi ya kunywa pombe kila siku na kurudi saa nane za usiku.manake hata hawa wanaume wanaojidai wanakunywa hadi saa nane usiku tunajua kabisa kuna mahali anapita kunyoosha mgongo na kupunguza usingizi ila kwa vile mkewe ana ushahidi basi tena kesi inapotelea hewani! huyo wivu tu unamsumbua,kwa vile hana kazi mkewe akirudi home kapita mahali mara mojamoja na washkaji akanywa bia 2 roho inamtoka. same as mwanamke ambae ni mama wa nyumbani,mume akirudi saa nne usiku kanywa bia 4 unajiskia kama analala nje manake toka atoke asubuhi unamsubiria aje upige nae michapo mpenzi wako. nimetaka kumpa mtoa mada majibu calm,ambayo huwa wanatupa sie tukilalamika na tukakasirika wanatuona wa ajabu. hahaha,nadhani umenielewa,lol
siku zikiisha ndio mwisho wa dunia..mambo ya kawaida vikombe vyenyewe vinagongana sembuse mijitu mizima????Kesi za ndoa haziishi!
Hilo limwanamke lake la rafiki yako lzm litakuwa na mapepo ya kutosha yaan jamaa kuacha kazi iwe nongwa,km vp ampige chini tu mwanamke gani hana hata huruma na mwanae mchanga hivyo?kiukweli amenitia hasira sana huyo sijui mwanamke au shetan.