Msaada kuhusu utaratibu huu wa udahili wa NACTE kwa mwaka wa masomo 2017/2018

Password

JF-Expert Member
Feb 17, 2011
777
1,082
Habari wakuu.

Mimi ni mmoja wa wanaosubiria kufanya maombi ya kujiunga na elimu ya juu(vyuo vikuu),nimekuwa nikitembelea tovuti(website) yao Mara kwa Mara kuona kama kuna updates zozote juu ya nafasi za masomo kwa waombaji wa mwaka 2017/2018.

Hatimae,jana wametoa update moja inayosema kwamba "maombi yote ya nafasi za masomo yatafanyika moja kwa moja kupitia vyuo husika,isipokuwa kwa wale wanaohitaji kujiunga na kada za afya na ualimu,hao wanaweza kutuma maombi kupitia website ya NACTE yenyewe.Mimi ninahitaji kujiunga na kada ya uhandisi nikianzia ngazi ya diploma,hivyo nikaamua kutembelea website ya DIT,

Lakini kwenye website hiyo kitengo cha kutuma maombi na wao wanasema maombi yote yafanyike kupitia website ya NACTE via CAS(Central Admission System) lakini pia DIT hawajatoa update za mwaka wa masomo 2017/2018 wao bado wanayo maelezo ya mwaka wa masomo 2016/2017,

Nikaamua kutembelea website ya MUST(Mbeya University of Science and Technology) huko pia mambo yapo kama DIT bado hawana update za mwaka wa masomo 2017/2018 na wao bado wapo 2016/2017 ila hawa hawajaeleza pia update zifanyike wapi.

Najua humu ndani kuna kuna wazoefu wengi na pengine wahusika wa system mpo humu,ninaomba ufafanuzi zaidi na pia ushauri nifanye nini baada ya hapo.Ninatanguliza shukrani za dhati kwa wote mtakaotoa muda wenu kujibu na kunishauri juu ya hili,Asanteni.
 
Chuo kikuu cha Iringa Tawi la Amani Njombe kinatangaza Nafasi za masomo kwa ngazi ya cheti na diploma kozi zinazo tolewa ni 1.Maendeleo ya jamii 2.usimamizi wa biashara 3.Ushauri nasihii 4.Tehama 5.sheria
NB:sifa za muombaji kwa kwa cheti awe amehitimu kidato cha nne na kufauru angalau masomo manne kwa alama D na diploma awe amemaliza kidato cha sita na kufauru angalau masomo mawili kwa Alama D na S Maombi yote yatumwe chuoni. NACTE wamerudisha utaratibu chuoni wa kudahiliMwisho wa kupokea maombi ni tarehe 20/08/2017.
kwa mawasiliano zaidi piga Simu 0753580894.
 
Ni kwamba utaratibu baada ya kubadirika bado vyuo havija update information zao kwenye website.
 
Ni kwamba utaratibu baada ya kubadirika bado vyuo havija update information zao kwenye website.
Huu utaratibu mpya utakuwa umekuja ghafla kwa vyuo vingi, kama udahili unaanza 15.5.2017 ungetegemea wangekwisha anza kujitangaza. Hivyo ni kuwa wavumilivu na kutembelea web site zao. Tuombe watoe taarifa kamili zinazo weza kumsaidia muombaji kufanya maamuzi yanayptakiwa. NACTE wangetoa guide ya kuwasaidia waombaji waweze kutambua vyuo na program wanazotoa na website ya vyuo hivyo ili waombaji wapate taarifa haraka. Heri na fanaka.
 
utaratibu huu sio mzuri hasa kama watafanya hivi na kwa vyuo vikuu coz mtu 1 anaweza chaguliwa vyuo 5! mwisho wa sku anaenda kimoja lkn pia baadhi ya vyuo vitachukua wanafunzi wenye ufaulu mkubwa(ie div 1 & 2) tu na vingine ufaulu mdogo tu! lkn CAS iliondoa hy madaraja.pia Kupitia CAS taarifa za vyuo vyote zilikua pamoja now utalazimika kuingia kila website ya chuo.
 
Kwa mfano chuo cha maji pale ubungo wao tayar wamesha update na applicatiom form tayari zipo kwenye website yao na pale chuoni,ila kwa kweli utaratibu huu sio mzuri kwa kuwa unamuongezea mwombaji gharama kwa mfano atalazimika kulipa ada ya form kwa kila chuo anachoomba na mara nyingi ada huanzia 20000 na kuendelea vp kama mtu amefanya maombi vyuo vingi?? Utaratibu wa CAS ulikua mzuri kiukweli.
 
huu utaratibu ndio utakaotumika kwa ngazi zote za elimu ni utaratibu mzuri unaompa mwanafunzi fursa ya kuchagua chuo anachokitaka kulingana na ufaulu wake pia italeta ushindani mkubwa sana wenye lengo la kuboresha elimu kila chuo kitajitahidi sana kurekebisha mapungufu yake ili kuwavutia wateja zaidi
 
Huu utaratibu mpya utakuwa umekuja ghafla kwa vyuo vingi, kama udahili unaanza 15.5.2017 ungetegemea wangekwisha anza kujitangaza. Hivyo ni kuwa wavumilivu na kutembelea web site zao. Tuombe watoe taarifa kamili zinazo weza kumsaidia muombaji kufanya maamuzi yanayptakiwa. NACTE wangetoa guide ya kuwasaidia waombaji waweze kutambua vyuo na program wanazotoa na website ya vyuo hivyo ili waombaji wapate taarifa haraka. Heri na fanaka.
Nenda chuoni moja kwa moja maana vyio ndio vimepewa mamlaka ya kudahili wanafunzi
 
huu utaratibu ndio utakaotumika kwa ngazi zote za elimu ni utaratibu mzuri unaompa mwanafunzi fursa ya kuchagua chuo anachokitaka kulingana na ufaulu wake pia italeta ushindani mkubwa sana wenye lengo la kuboresha elimu kila chuo kitajitahidi sana kurekebisha mapungufu yake ili kuwavutia wateja zaidi
Hapo nyuma kidogo,ndo utaratibu uliokuwa unatumika. Ni utaratibu mzuri.
 
Wakuu nahitaji form za kujiunga na vyuo vya kilimo. Nimeambiwa niingie kwenye website ya wizara lakini sijafanikiwa kuziona. Msaada ktk hili
 
utaratibu huu sio mzuri hasa kama watafanya hivi na kwa vyuo vikuu coz mtu 1 anaweza chaguliwa vyuo 5! mwisho wa sku anaenda kimoja lkn pia baadhi ya vyuo vitachukua wanafunzi wenye ufaulu mkubwa(ie div 1 & 2) tu na vingine ufaulu mdogo tu! lkn CAS iliondoa hy madaraja.pia Kupitia CAS taarifa za vyuo vyote zilikua pamoja now utalazimika kuingia kila website ya chuo.
mkiambiwa msome hamtaki kutwa kushinda social network we kama hauna div 1 na 2 sahau udsm na muhimbili
 
Kuna wengine mkuu hata hivyo vyuo vyenyewe hawavijui, na vyuo vyetu ni wavivu wa kutangaza.
ahaaa vyenye majina si vinajulikana sasa chuo kipo newala ndani uko nani ampeleke mwanae ... uko akaliwe:D:D:D:D:p:p:p:p:p
 
Back
Top Bottom