A
Anonymous
Guest
Habari!
Napenda kuleta kero yangu ili mnisaidie kufikisha kwa wahusika wa Chuo cha DIT. Kuna kero kubwa hususani kwa wanafunzi waliopata mkopo kupitia Bodi ya mkoppo ya elimu ya juu (HESLB) pale wanapokuwa wanaanza mwaka wa masomo huitajika kulipa ada kwanza kabla ya kufanyika usajili, wanafunzi hao hulipa ada halafu baada ya muda HESLB hupeleka fedha hizo vyuoni.
Inapotokea pesa ya ada imezidi iliyotakiwa kulipwa, kiutaratibu inabidi mwanafunzi husika arudishiwe pesa iliyozidi. Lakini kumekuwa na maelezo kutoka kwa uongozi wa chuo kuwa Mwanafunzi hatorudishiwa pesa hadi pale atakapomaliza masomo yake yaani baada ya miaka minne au itatumika (transferred) kwa mwaka mwingine wa masomo kitu amabacho si sahihi kwa kuwa kila mwaka wa masomo unajitegemea ndio maana kunausajili kila mwaka mpya wa masomo unapoanza.
Je, ni halali Chuo kukaa na pesa ya mwanafunzi kwa muda wa miaka minne? Na ni sababu gani inasababisha baada ya miaka minne ndio pesa iweze kutoka na ishindikane kutoka ndani ya muhula wa masomo aliolipa hiyo pesa? Chuo hakioni kinatakiwa kulipa interest kwa kukaa na pesa za wanafunzi kwa muda mrefu?
Je, Chuo hakioni kinatengeneza mazingira magumu kwa wanafunzi ambao wanahitaji kutumia pesa hiyo kwenye mahitaji yao binafsi?
Je, Chuo hakioni kinatengeneza mazingira ya wanafunzi kuacha pesa kwa kusahau kwa kuwa ni vigumu kukumbuka na kutunza vielelezo vya malipo kwa muda wa miaka minne?
Asante.
Napenda kuleta kero yangu ili mnisaidie kufikisha kwa wahusika wa Chuo cha DIT. Kuna kero kubwa hususani kwa wanafunzi waliopata mkopo kupitia Bodi ya mkoppo ya elimu ya juu (HESLB) pale wanapokuwa wanaanza mwaka wa masomo huitajika kulipa ada kwanza kabla ya kufanyika usajili, wanafunzi hao hulipa ada halafu baada ya muda HESLB hupeleka fedha hizo vyuoni.
Inapotokea pesa ya ada imezidi iliyotakiwa kulipwa, kiutaratibu inabidi mwanafunzi husika arudishiwe pesa iliyozidi. Lakini kumekuwa na maelezo kutoka kwa uongozi wa chuo kuwa Mwanafunzi hatorudishiwa pesa hadi pale atakapomaliza masomo yake yaani baada ya miaka minne au itatumika (transferred) kwa mwaka mwingine wa masomo kitu amabacho si sahihi kwa kuwa kila mwaka wa masomo unajitegemea ndio maana kunausajili kila mwaka mpya wa masomo unapoanza.
Je, ni halali Chuo kukaa na pesa ya mwanafunzi kwa muda wa miaka minne? Na ni sababu gani inasababisha baada ya miaka minne ndio pesa iweze kutoka na ishindikane kutoka ndani ya muhula wa masomo aliolipa hiyo pesa? Chuo hakioni kinatakiwa kulipa interest kwa kukaa na pesa za wanafunzi kwa muda mrefu?
Je, Chuo hakioni kinatengeneza mazingira magumu kwa wanafunzi ambao wanahitaji kutumia pesa hiyo kwenye mahitaji yao binafsi?
Je, Chuo hakioni kinatengeneza mazingira ya wanafunzi kuacha pesa kwa kusahau kwa kuwa ni vigumu kukumbuka na kutunza vielelezo vya malipo kwa muda wa miaka minne?
Asante.